Makapuku Forum

Watoto watatu kutoka Shule ya Msingi Itubukilo B, Kijiji cha Pugu, Kata ya Itubukilo Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu wamefariki dunia baada ya mkokoteni waliokuwa wakisafiria baada kuchota mchanga Mtoni kusombwa na maji ukiwa unavutwa na ng’ombe sita.

Waliofariki ni Maleki Legi (16), Isaka Njile (14) na Wille Njile ambao ni Watoto wa familia moja huku Watoto wawili wakinusurika.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Simon Simalenga @official_simalengatz akiwa ameambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya hiyo amefika katika eneo hilo na kujumuika na Wananchi ambapo pamoja na kuwapa pole Wafiwa amewaasa Wazazi juu ya umuhimu wa kuzingatia malezi ya Watoto hususani kipindi hiki cha mvua kubwa.

“Ndugu zangu Wanakijiji cha Pugu kwa niaba ya Serikali nimesikitishwa na kusononeshwa na tukio hili la kusikitisha na kusononesha limekatisha maisha ya Watot wetu hawa ambao walitakiwa kuwa nyumbani wakati huu wa msimu wa mvua”

“Poleni sana Wazazi, Ndugu na Wanakijiji wote, nawasihi sana tuwe makini katika malezi ya watoto hususani katika kipindi hiki cha mvua, ni jambo la kusikitisha kusikia Watoto hawa wadogo walipewa jukumu la kwenda Mtoni kuchota mchanga tena wakiwa na mkokoteni uliokuwa unavutwa na ng’ombe 6 tofauti na umri wao”

Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji Mkoa wa Simiyu Inspector Faustine Mtitu amewataka Wananchi kuendelea kuchukua tahadhari pindi wavukapo Mito na madimbwi kwani kumekuwa na maji mengi ambayo yanaweza kuleta maafa.
 
Majeruhi watano kati ya sita waliopelekwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa baada ya kupata ajali wamefariki, Watu hao walipata ajali jana Aprili 25, 2023 katika eneo la TRM, Kihesa Kilolo, Manispaa ya Iringa iliyohusisha gari, bajaji na bodaboda.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa, Alfred Mwakalebela amesema majeruhi mmoja bado anaendelea kupatiwa matibabu ili kuokoa uhai wake “Watatu walifariki tangu jana vifo viwili vimetokea leo wakati wa matibabu yakiendelea kufanyika, mpaka sasa majeruhi mmoja anaendelea kupatiwa matibabu bado hajajulikana jina lake na Ndugu hawajatokea”

"Inasemekana kuna Kijana haonekani anafanya kazi ya kukatisha tiketi Kihesa, sasa nashauri Watu jirani wangekuja wamuone Kijana huyu huenda akawa ni yeye”

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa,Allan Bukumbi amesema wanaendelea kufanya uchunguzi zaidi juu ya chanzo cha ajali hiyo.

Hata hivyo baadhi ya Mashuhuda wamesema bodaboda iliyoingia barabarani ghafla ndiyo sababu ya ajali hiyo.
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo ametoa msamaha kwa Wafungwa 376 ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 59 ya Muungano wa Tanzania, taarifa hiyo imetolewa leo na Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni.

Wafungwa sita kati ya walionufaika na msamaha huu wataachiliwa huru leo tarehe 26/04/2023 na Wafungwa 370 watabaki gerezani kumalizia sehemu ya kifungo kilichobaki baada ya kupewa Msamaha huu.

“Ni mategemeo ya Serikali kwamba watarejea tena katika Jamii kushirikiana na Wananchi wenzao katika ujenzi wa Taifa letu na kwamba watajiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena gerezani”
 
Kamishna Jenerali wa Magereza, Mzee Ramadhani Nyamka amezindua Sare mpya za Wafungwa Wanawake katika Gereza Kuu la Wanawake, Kingolwira Morogoro, Sare hizo zitatumiwa na Wafungwa wote Wanawake wanaotumikia viifungo vyao Magerezani.
 
Naibu Katibu wa Chadema-Zanzibar, Salum Mwalimu akichangia mada nini kifanyike kuimarisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar amesema, mimi ni muumini wa Muungano ninaupenda nipo tayari kuutetea na kulinda, una faida zake. Nitakuwa wa kwanza kupiga kura ya Muungano huu uendelee.

Tatizo kubwa la Muungano sio kero za kodi au masuala mengine. Tatizo kubwa ni muundo wetu, tunaweza kupunguza kero kama tutakaa na kujadili muundo wa Muungano wetu ili kuwa imara na endelevu. Adui yetu ni yule anayesema Muungano uvunjwe.

Zamani Wazanzibari tukizungumza malalamiko tuliokena tunataka kujitenga, sasa hivi manung'uniko yamehamia hadi Tanzania bara. Sasa hivi ikitokea Wazanzibar wamepata nafasi kwenye Muungano watu wa bara wanalalamika wanapendelewa.

Wakati umefika wala siogope tukubali ili tuwe na Muungano wa muundo wa Serikali tatu. Itampa nguvu kila mmoja kuamua mambo yake, tukiendelea kuogopa Muungano utaendelea kulindwa kwa mitutu au hofu.

Tunapaswa kulinda Muungano kwa Watanzania kuufurahia na kuwa mioyo safi. Muundo wa sasa naona ugumu mtu kutoka Zanzibar kuwa Rais wa Jamhuri Muungano wa Tanzania, kwa sasa imeshazoeleka anatoka bara na Zanzibar inatoa makamu wa rais.

Mimi ni Mzanzibar nimesoma na kukulia huku, lakini maisha yangu yanaendelea Tanzania bara.
 
Watu watatu wa familia moja kati ya wanne waliofariki juzi baada ya gari walilokuwa wamepanda kusombwa na mafuriko, akiwemo mama, mtoto na mtoto wa kaka yake, wanatarajiwa kuzikwa Ijumaa Aprili 28, 2023 katika eneo la Ilboru, Wilaya ya Arumeru Mkoa wa Arusha.

Tukio hilo lilitokea jana Aprili 25, 2025 asubuhi katika eneo la King’ori wilayani humo, ambapo mbali na hao waliofariki, wawili walinusurika, wakati tukio hilo lilipotokea wakiwa safarini kwenda Kilimanjaro kwenye mahafali ya kidato cha sita.

Leo Jumatano Aprili 26, 2023 akizungumza na waandishi wa habari msibani hapo, Mwenyekiti wa ukoo na msemaji wa familia hiyo Mchungaji Edgad Metili, alisema waliofariki ni Matha Metili (40) na mtoto wake Lisa Metili (8), Colin Lymo (16) mwanafunzi wa Ilboru, aliyekuwa anakwenda kwenye mahafali ya dada yake Shule ya Sekondari Mwika na jirani yao Brenda Amani (25).
 
CITY WANAKANDA KIBINGWA

.
FT: MAN CITY 4-1 ARSENAL
07’—
️ de Bruyne
45’—
️ Stones
54’—
️ de Bruyne
86’—
️ Holding
90’—
️ Haaland

 
Huyu FRANK LAMPARD kila mtu anajipigia !!
.
FT: CHELSEA 0-2 BRENTFORD
️ Aziplicueta (Og)
️ Mbeumo
.
Lampard tangu arejee kuinoa Chelsea hajashinda hata mechi moja.

 
BACCA: YULE BANGALA ACHENI TU
.
Beki wa kati wa Yanga Ibrahim Abdullah ‘Bacca’ amesema anafurahi kucheza na mabeki wote waliopo Yanga kutokana na kila mmoja kuwa na aina yake ya uchezaji huku akisisitiza kuwa anafurahi zaidi akicheza na Bangala kama namba sita.
.
“Mabeki wote nimepata nafasi ya kucheza nao wana uwezo na ni viongozi wazuri kiwanjani lakini nafurahi zaidi nikicheza na beki mwingine kati na Bangala akawa juu kama namba sita ni mtu makini sana na anapenda kuzungumza mimi namuita beki kiongozi;
.
“Mkicheza uwanjani kwa kukumbushana majukumu mchezo wa mpira ni mwepesi na makosa mengi yanapungua tuna nahodha Mwamnyeto anazungumza ana kila sifa ya kuwa kiongozi lakini kuna Bangala hapendi timu ifungwe kizembe.” alisema.
 
.
“Kutakuwa na mabadiliko ya kikosi, tunakwenda na tahadhari kubwa kwa kuwa wapinzani watakuja tofauti na walivyocheza hapa nchini, lazima tukubali tunatakiwa kwenda kwa umakini mkubwa. Maandalizi
yetu, yanaonyesha tunaweza kufanya mambo makubwa ugenini.

- Kocha Robertinho.
 
Shaffih Dauda

SIFA GANI ZINAMFANYA MCHEZAJI KUWA NAHODHA BORA?

Naohodha ni kiongozi, suala la umri lina nafasi yake lakini pia tusisahau kuna watu wamezaliwa wana karama ya kuongoza/uongozi bila kujali umri.

Kwa hiyo kuna nyakati mchezaji anaweza kupewa unahodha wa timu kutokana na karama yake ya uongozi.

Wakati mwingine umri unazingatiwa kwa sababu kunaweza kutokea migongano kati ya wachezaji kambini kwa hiyo nahodha kama kiongozi wa timu anapaswa kusimamia na kumaliza tofauti hizo.

Makocha wengine wanaangalia nani ni nyota wa timu na inabidi kumlinda na makosa madogomadogo ndani ya kiwanja. Mfano mchezaji ambae anapenda kulaumu baada ya mwamuzi kuchukua hatua.

Mwamuzi anaweza kuchagua kutomuadhibu kutokana na kukosoa baadhi ya matukio uwanjani akiamini ni kiongozi wa wachezaji wenzake.

Wengine wanapewa unahodha wa uwanjani kutokana na rekodi za matukio mabaya wawapo uwanjani. Kwa hiyo kumpa unahodha kunamfanya kuhisi tayari amebeba majukumu ya timu hivyo anapaswa kuwa mfano kwa wenzake uwanjani. Kwa hiyo anapewa kitambaa kumtuliza.

Kwa hiyo suala la unahodha makocha huwa wanalitazama kwa picha kubwa. Ndio maana wakati mwingine huwa kuna nahodha kiongozi na hapati sana nafasi ya kucheza mara kwa mara.
 
Shaffih Dauda

Siku moja ndugu yangu @amrikiembatz alikuwa anasimulia story ya fundi Haruna Moshi ‘Boban’ kwamba ni miongoni mwa wachezaji wastaarabu sana na waungwana lakini unapobidi kumkabili mchezaji/wachezaji au kiongozi pia anaweza!

Luambano akastuka na kuuli hivi Boban anaongea mbele za watu? Aliuliza hivyo kwa sababu mara nyingi Boban si mtu wa kuzungumza sana.

Kiemba akasema Boban ni mzungumzaji mzuri sana mkiwa wachezaji wenyewe kwa wenyewe lakini panapokuwa na mtu ambaye hahusiki unaweza usimsikie akizungumza.

Kiemba anasema Boban ni mchezaji ambaye anaweza sana kumhamasisha mchezaji ambaye anaonekana hata kukata tamaa na akamrudisha kwenye ari ya kucheza.

Lakini vilevile ni mtu ambaye anamudu kumkabili mchezaji kwa kumshambulia ‘kuchana makavu’ pale anapoona mambo hayaendi sawa.

Vilevile Boban anaweza kupigania haki ya mchezaji mwingine. Mfano imetoka Bonas halafu baadhi wanataka kugawa kwa kuwaonea wengine, Boban atawapambania wote wapate kadiri wanavyostahili.
 
Shaffih Dauda

“Mashabiki wa mpira wa miguu wa mataifa ya Kaskazini mwa Afrika wakijaa uwanjani kuna athari wachezaji wa timu pinzani wanaipata!

“Kwa namna mashabiki wa Tanzania wanavyoshangilia wakiwa uwanjani, hata uwanja ukiwa nusu mashabiki wa timu ya Tanzania halafu nusu mashabiki wa timu ya Kiarabu hatuwezi kuwafunika.”

“Mashabiki wa timu za mataifa ya kiarabu wakiwa uwanjani sio watu wa kukaa na kupiga-selfie, kazi yao inakuwa moja, kushangilia tu!

“Wenzetu tayari wana nyimbo za klabu ambazo sio za kujifurahisha, zinagusa hisia na zinakuwa na historia na jambo kwa hiyo zikiimbwa kila shabiki anahisi kuguswa.”

- Amri Kiemba [@amrikiembatz] via @cloudsfmtz
 
Shaffih Dauda

“Msiba ukiwa na watu wengi sisi ndio tunafurahi kwa sababu wanapata muda wa kubembelezana, wingi wa mashabiki wa Wydad Casablanca uwanjani kwao ni faida kwetu kwa sababu wao ndio wenye presha.”

“Wydad tangu wameanza kushiriki Ligi ya Mabingwa msimu huu, hawajakutana na timu aina ya Simba. Tayari wana adabu zao huko waliko.”

“Kwa hiyo mashabiki wa Wydad wajae wawezavyo uwanjani, hii mechi [Wydad Casablanca vs Simba] itawatoa machozi na kuwapasua mioyo watu wa Morocco.”

- Ahmed Ally [@ahmedally_] kuhusu Wydad Casablanca kuuza tiketi zote za mchezo dhidi ya Simba.
 
Farhan Jr

KWANINI CAF WANASEMA SIMBA WANAPAMBANIA NUSU FAINALI YAO YA KWANZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA NA SIO NUSU YA KWANZA YA MICHUANO AFRIKA?

Okay! Mwandishi kazi yake ni kuelimisha, kuburudisha na kuhabarisha! Vyote vitatu ni kazi ya Mwandishi, nadhini sisi tujikite kwenye KUELIMISHA kisha wengine KUBURUDISHA, its okay! Fair and Legit!

Ni hivi michuano ya klabu barani Afrika ilianza 1964 ambapo michuano mikubwa zaidi ilikuwa inatambulika kama AFRICAN CUP OF CHAMPIONS CLUBS, ambapo michuano hii ilipigwa mpaka 1997 kabla ya kuboreshwa (Rebranded).

Kwahiyo tangu 1964 mpaka hivi sasa wale wote waliotwaa ubingwa wa michuano hii wanaorodheshwa kama Mabingwa na ukienda kwenye website ya CAF mabingwa wote wapo kuanzia 1964 mpaka 2022, kwakuwa kilichobadilika ni jina na muundo tu.

SIMBA alicheza nusu fainali ya AFRICAN CUP OF CHAMPIONS CLUBS mnamo 1974 wakati huo haitambuliki kama LIGI YA MABINGWA AFRIKA lakini ipo kwenye orodha kuwa Simba walicheza nusu fainali ya michano mikubwa Afrika.

Kwanini?? Ukienda kwenye website ya CAF kupitia bando la @tigo_tanzania wanajua kuwa CAF CHAMPIONS LEAGUE awali ilitambulika kama CHAMPIONS CUP, hivyo wanawatambua tangu 1964 mpaka 2022 kama Mabingwa WINNERS OF PREMIER CAF COMPETITION, kwakuwa walibadili tu jina, hivyo wanaposema nusu fainali ya kwanza ya CAF CHAMPIONS LEAGUE ni sahihi kwakuwa Simba alicheza CLUBS CHAMPIONS CUP.

Bingwa wa Afrika 1974 ambapo Simba alicheza nusu fainali alikuwa ni CARA Brazaville ya Kongo! Hatua ya nusu fainali SIMBA VS GHAZL EL MEHALLA na CARA BRAZAVILLE VS ASC Jeanne De Arc, fainali ilawa Cara vs Mehalla.

Ukienda kwenye website ya CAF Bingwa wa 1974 ndie huyo kawekwa na nusu fainali ndizo hizo na Simba alicheza hii michuano!

Kwanini michuano ilibadilishwa? Ilikuwa muundo wa kidunia ambapo Ulaya walihama kutoka European Cup na kuita CHAMPIONS LEAGUE 1992 huku timu zikiendelea kutambulika ni Mabingwa wa Ulaya hata kama walibeba kabla ya 1992.

Issa Hayatou 1997 akabadili pia Afrika na kuita CAF Champions League huku mfumo ukibadilika kutoka knockouts mpaka hatua ya awali, makundi kisha Knockout stages! Simba alishafanya hivyo kabla ya hii format mpya.

Thats the logic! A very simple logic!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…