Makapuku Forum

HAYA ndio maajabu ya Stephane Aziz KI. Wakati ambao wadau na mashabiki wa Yanga wamekuwa wakiona kiwango chake kimeshuka kwa vipindi tofauti, nyota huyo wa Kimataifa kutoka Burkina Faso amekuwa akiibuka na kuwashangaza kwa kufanya makubwa.

Ni nani ambaye alijua atauwasha vile kwenye mchezo uliopita wa Yanga wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar? Unakumbuka kilichotokea dhidi ya Club Africain kule Tunisia wakati wakipigania nafasi ya kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika na vipi kuhusu mchezo wa kwanza wa dabi msimu huu kwenye Ligi.

Akizungumzia kurejea kwa kiwango cha Aziz KI, kocha Nabi alisema kikao ambacho walifanya na mshambuliaji hiyo kimechangia juhudi kubwa za kutaka kukuona anarudi katika kiwango chake.

Nabi alisema Aziz KI anatakiwa sasa kuendeleza moto wa kufunga na kucheza vizuri.

"Tulifanya juhudi kubwa ya kuongea naye na kumuelewesha jinsi anavyotakiwa kurudi katika kiwango chake, mimi binafsi niliongea naye lakini pia wasaidizi wangu na hata viongozi nao walikuwa wakifanya hizi juhudi," alisema Nabi.

"Tulikuwa tunaumia mioyo yetu kumuona anakuwa katika wakati mgumu licha ya jina lake kubwa, nafikiri sasa amepata sehemu ya kuanzia na kuendeleza makali yake ili azidi kufanya makubwa zaidi."

 
MBINU ZA KIBABE
.
Timu zote mbili zimekuwa zikipendelea kutumia mfumo wa 4-2-3-1 lakini zimekuwa zikitofautiana katika aina ya wachezaji zinazowatumia katika mfumo huo.
.
Wakati Simba ikiwatumia viungo wawili asilia kati ya wachezaji watatu wanaocheza nyuma ya mshambuliaji wake wa kati ambao ni Saido Ntibazokinza na Clatous Chama, Yanga yenyewe imekuwa ikitumia mawinga asilia kati ya wachezaji watatu wanaocheza nyuma ya straika wao.
.
Yanga imekuwa ikitumia zaidi winga yake ya kulia na beki wa kushoto kutengeneza mashambulizi wakati Simba imekuwa ikiwatumia zaidi viungo wake washambuliaji kutimiza jukumu hilo.
 
ukimkumbuka shunie nenda makapuku utamkuta tele...


alisikika mlevi mmoja...

sema mkuu umeadimika.. au siku hizi huji majukwaa mengine
 
KOCHA NABI KUHUSU FOMU YA AZIZ KI
.
“Tulifanya juhudi kubwa ya kuongea naye na kumuelewesha jinsi anavyotakiwa kurudi katika kiwango chake, mimi binafsi niliongea naye pia wasaidizi wangu na hata viongozi nao walikuwa wakifanya hizi juhudi,”
.
“Tulikuwa tunaumia mioyo yetu kumuona anakuwa katika wakati mgumu licha ya jina lake kubwa, nafikiri sasa amepata sehemu ya kuanzia na kuendeleza makali yake ili azidi kufanya makubwa zaidi.”

 
HISTORIA YA DABI KATIKA LIGI KUU
.
Historia ya mechi za nyuma baina ya timu hizo, inaonyesha kuwa Yanga ndio watemi wa mechi za Kariakoo Dabi ingawa Simba wameonekana kujitutumua ili kusawazisha hali ya mambo.
.
Yanga inaongoza kwa kupata ushindi katika mechi nyinyi za ligi Kuu dhidi ya Simba ambao katika mechi 109 walizocheza kabla ya kesho, wameibuka na ushindi mara 38, Simba wakishinda 31 na zimetoka sare mara 40.
.
Upande wa pointi, Yanga imekusanya pointi 154 na Simba imekusanya pointi 133 katika mechi baina yao huku Yanga ikiwa kinara kwa kufunga idadi kubwa ya mabao ikiwa nayo 113 na Simba imepachika mabao 101.

 
MANULA HATIHATI DERBY
.
Habari ya kushtua ni kwamba kipa namba moja wa Simba, Aishi Manula anaweza asisimame langoni kesho saa 11:00 jioni dhidi ya Yanga katika pambano la Kariakoo Derby.
.
Manula alikosa mechi iliyopita ya Ligi Kuu dhidi ya Ihefu baada ya kutolewa uwanjani kwenye pambano la robo fainali ya Kombe la ASFC pale Simba ilipovaana na Ihefu haohao na kushinda mabao 5-0.
.
Kipa huyo namba moja wa timu ya taifa, Taifa Stars ambaye bado hajaanza mazoezini hadi jana jioni ila kukiwa na makipa wenye viwango vikubwa Beno Kakolanya na Ally Salim kunaleta ahueni.

………………
 

nimeamini adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzake
 
Maana halisi ya mpira wa miguu, maana halisi ya mchezo pendwa, maana halisi ya wema wa huu mchezo na maana halisi ya Watani wa jadi na sio Mahasimu.

Football ya Tanzania inaweza kukupa picha nyingi sana, inaweza kukupa stori nyingi sana ila itakupa picha chache sana za maktaba kama hizi.
 
#KariakooDerby | Kuna mambo mengi sana unayajumuisha pamoja unapoelekea kwenye mechi, matarajio ya mashabiki, wajibu wa viongozi, wachezaji na benchi la ufundi kila mmoja anatakiwa kutimiza majukumu yake inavyotakiwa.

Wakati mwingine kinachosababisha hizi mechi [Simba vs Yanga] zinakuwa ngumu ni viongozi na wenyewe kuingia kucheza mechi. Badala ya kuacha umakini mkubwa kwenye idara ya ufundi badala yake focus inahamia kwenye tathmini binafsi na hisia za mashabiki.

Ikishatokea hivyo, kuna vitu vya msingi vinakuwa havipewi kipaumbele kwenye maandalizi. Mimi ningekuwa kiongozi wa hizi timu wiki moja kabla ya mechi ya watani ningeomba viongozi tuwaachie benchi la ufundi kila kitu.

Kwa sababu kila inapokaribia mechi hizi unakuta viongozi karibu wote wanataka kuhudhuria mazoezi, hii wakati mwingine inasababisha presha kwa wachezaji.
 
Farhan Jr

Who is the man between the sticks tomorrow? Ni Ally Salum au Beno Kakolanya kesho kwenye Derby?

- Beno Kakolanya ni jibu la kimbinu na kiufundi, ana uzoefu na derby na pasi na shaka Mabeki hawatofanya kazi ya ziada au kuwa na hofu sana kutokana na aina yake ya uchezaji.

Kwanini kuna maswali mengi? Kama nilivyoripoti mapema asubuhi kuwa Beno ameshamalizana na Singida BS, hivyo kuna ‘siasa’ ya mpira hapo kati kuelekea derby, nje na hapo hakuna sababu ya Beno kutosimama langoni.

Kutoka kwa vyanzo vyangu ni kuwa kuna vikao vya hapa na pale kati ya Waandamizi wa Msimbazi na Beno, huku wakiamini ndio jibu pekee na sahihi kimfumo kesho aanze.

- Ally Salum is always ready, under any given circumstance basi the Goalie is up to the challenge.

 
Kuna uwezekano mkubwa Aishi Manula akakosekana kwenye derby kutokana na changamoto ya majeraha ambapo huenda akafanyiwa upasuaji wiki mbili baada ya hivi sasa.

Uwezekano mkubwa ni Ally Salum akasimama langoni kesho kutokana na ukweli kwamba Beno Kakolanya ameshamalizana na Singida Big Stars na tetesi zikisema atajiunga nao msimu ujao.

 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…