Makapuku Forum

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Sixtus Mapunda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga.

Samia amefanya uteuzi huo leo Machi 09, 2023 ambapo Mapunda amechukua nafasi ya Jane Nyamsenda ambae uteuzi wake umetenguliwa.

 
Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) leo Machi 9, 2023, imepokea meli nyingine ya kimataifa iliyobeba watalii 125 kutoka nchini Ufaransa.

Meli hiyo ya utalii ijulikanayo kama Le Jacques - Cartier Ponant, imebeba watalii watatembelea Hifadhi ya Urithi wa Utamaduni wa Dunia Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara kwa ajili ya kufanya utalii wa Malikale na fukwe.

Baada ya kutembelea maeneo hayo pia meli hiyo inaendelea na safari katika visiwa vya Pemba na Unguja.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…