Farhan Jr
ERIK TEN HAAG, heshima kwa Vinyozi wote wanyoa vipara kisha heshima kwa Makocha wote wenye vipara! Ni muda wa kulitambua darasa maarufu, The Class of Upara alikuwepo Pep Guardiola, Zinadine Zidane, Jorge Sampaoli, Luciano Spaletti na Prof Nabi! Lakini mpokeeni rasmi mgeni mpya Erik Ten Haag.
God created the world, Dutch created Holland! FIFA made football, Erik Ten Haag teaches Football! Ni mistari mipya ianze kutumika baada ya usiku huu pale Wembley, ni wasaa wa kuanza kumpa heshima yake ETH, kazi ngumu kwa sura rahisi, vitu vigumu kwa namna rahisi, United kubeba ndoo haikuwa rahisi.
Wangindo wanasema utu uzima dawa, Waluguru walisema nazi haishidani na jiwe lakini sio kwenye kamusi ya Erik Ten Haag! Amepiga Mwalimu wake Guardiola, amempiga Mikel Arteta ambaye ni Mwanafunzi mwenzake na bado Kompany na Xavi! They either hate or get motivated, ila ETH anagawa darasa la bure kabisa.
Aliongea mbele ya kipaza kuwa anaziheshimu City na Liverpool lakini zama hufika mwisho!