Makapuku Forum

Makapuku Forum

Bondia Mtanzania Seleman Kidunda amekuwa Bingwa wa mkanda wa WBF Intercontinental uzito wa Super middle weight (76KG) kwa kumpiga Bondia Erick Katompa Raia wa Congo DR kwa point katika pambano la round 9 lililochezwa usiku huu katika uwanja wa Majimaji Songea.
Screenshot_20220731-041450_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Innocent Bashungwa ameagiza kusimamishwa kazi na kuhojiwa na Taasisi Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) watumishi watano kutokana kuisababishia hasara Halmashauri ya Wilaya Kiteto Mkoani Manyara.

Bashungwa amesema “Ukifanya ubadhilifu na kuhamia Halmashauri nyingine au Taasisi yoyote ya Serikali, nitakufuata huko huko niseme na wewe, bora kufia site kuliko kumuangusha Rais wetu Samia Suluhu Hassan”

Watumishi hao ni aliyekuwa Mweka Hazina, Nassoro Mkwanda na Mhasibu wa Mapato, Christopher Mwigani, Kaimu Mwanasheria wa Halmashauri Joseph J. Hoza, Kaimu Mweka Hazina Hadija Boffu pamoja na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi Nakaji Mollel.

Kati ya hao ni Nassoro Mkwanda aliyehamishiwa Mafinga Mji, Khadija Bofu aliyehamishiwa Songea Manispaa na Christopher Mwigani ambaye amestaafu, wote wanatuhumia kuhamisha fedha na kuweka kwenye akaunti ya amana isiyo na vifungu vya matumuzi na wanatakiwa kurejeshwa kwenye Halmashauri hiyi kujibu tuhuma hizo.

Pia Kaimu Mkuu wa kitengo cha manunuzi Nakaji Melateki Mollel ambaye aliidhinisha Sh milioni 191.9 kwa ajili ya kununua vifaa vya ujenzi bila kufauta taratibu sambamba na Sh milioni 235.5 alizolipa mkandarasi wa kuchimbia visima bila kuzifanyiwa tathimini na Khalfan Hinga aliyetoa kazi hiyo bila kufanyika tathimini.
Screenshot_20220731-041744_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa, amempongeza Mwanariadha Mtanzania Alphonce Felix Simbu kwa kushika nafasi ya 2 katika mbio ndefu za Jumuiya ya Madola na kupata medali katika mashindano hayo nchini Uingereza.

Bashungwa amesema “Simbu umetuheshimisha Tanzania, Asante sana Rais wetu Samia Suluhu kwa kuleta mageuzi ya haraka kwenye maendeleo ya michezo nchini, hongereni sana Waziri Mchengerwa, Katibu Mkuu Dkt. Abbas, Mkurugenzi Singo, Bi. Neema Msitha- BMT na Shirikisho la Riadha kwa kumsaidia Rais kwa dhamira yake ya kuendeleza michezo, mmeupiga mwingi na mpira mkaondoka nao”

Mwanariadha Mtanzania Felix Simbu amefanikiwa kumaliza nafasi ya pili katika mbio ndefu (marathon) za Jumuiya ya Madola na kushinda medali ya fedha katika mashindano hayo yanayofanyika Birmingham Uingereza.
Screenshot_20220731-041846_OGInsta%2B.jpg
 
Jiji la Hanover nchini Ujerumani limepiga marufuku matumizi ya maji ya moto katika majengo ya umma na mabwawa ya kuogelea ili kupunguza matumizi ya nishati ya gesi ikiwa ni baada ya Urusi kupunguza mtiririko wa gesi nchini humo kwa asilimia 20.

Marukufu hiyo imeelezwa kuathiri mabwawa ya kuogelea, hoteli na kumbi za michezo ambapo wakazi wa jiji hilo watalazimika kutotumia maji ya moto pindi wawapo katika majengo ya umma.

Meya wa jiji hilo Belit Onay ametangaza kuwa wakazi wanapaswa kupunguza matumizi ya nishati kwa asilimia 15 kutokana na uhaba wa nishati ya gesi uliopo kwa sasa.

"Hali haitabiriki, kama siku chache zilizopita tunapaswa kuchukua tahadhari, tunaona ni jukumu letu na hatuna budi kusonga mbele, kila saa ya kilowati inabidi kuhifadhiwa ili kulinda hifadhi ya gesi”

Hanover inakuwa ni Jiji la kwanza nchini Ujerumani kutoa marufuku hiyo baada ua Urusi kupunguza usambazaji wa gesi kwa asilimia 20 nchini humo.
Screenshot_20220731-041955_OGInsta%2B.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Mahakama nchini Misri imetoa hukumu ya kunyongwa kwa Mtuhumiwa Mohamed Adel (21), huku akionyeshwa kwenye Televisheni nchini humo baada ya kupatikana na hatia katika kesi ya mauaji iliyokuwa ikimkabili.

Mohamed Adel alipatikana na hatia ya kumuua Mwanafunzi mwenzake wa kike Nayera Ashraf nje ya Chuo Kikuu cha Mansoura kaskazini mwa Misri mwezi uliopita baada ya binti huyo kumkatalia ombi lake alipomtongoza.

Mahakama imeliandikia barua bunge la Misri kuruhusu kunyongwa kwa Mohamed kurushwe moja kwa moja kupitia matangazo ya televisheni nchini Misri ili kuzuia matukio ya kihalifu kama hayo kutojirudia tena.

Tukio la mauaji ya mwanafunzi Nayera lilisambaa kupitia video katika mitandao ya kijamii na kuzua hasira nchini humo huku mamlaka zikilaumiwa kwa kutochukua hatua kali dhidi ya vitendo vya kiunyanyasaji dhidi ya wanawake.

Shirika la Amnesty International lilitoa ripoti mwaka jana kwamba polisi nchini Misri kutochunguza vya kutosha unyanyasaji wa kingono na kijinsia kwa wanawake na mahakama hazitoi adhabu za kutosha.
Screenshot_20220731-042050_OGInsta%2B.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee
MANE KAFANYA YAKE !!
.
HT: RB LEIPZING 0-3 BAYERN MUNICH
[emoji460]️ Musiala
[emoji460]️ Mane
[emoji460]️ Pavard
Screenshot_20220731-042547_OGInsta%2B.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee
[emoji599] BREAKING: SENZO ASEPA YANGA
.
Klabu ya Yanga imethibitisha aliyekuwa Mtendaji Mkuu, Senzo Mazingisa ameomba kuondoka.
Screenshot_20220731-042821_OGInsta%2B.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee
DAH!! Kipara kazingua
.
FT: LIVERPOOL 3-1 MAN CITY
21’—Arnold [emoji460]️
71’—Alvarez [emoji460]️
84’—Salah (pen) [emoji460]️
90+4’—Nunez [emoji460]️
.
Liverpool inafanikiwa kutwaa Ngao ya Jamii [emoji1017]
Screenshot_20220731-042921_OGInsta%2B.jpg
 
JESUS KAPIGA HAT-TRICK [emoji145]
.
10'—Saka [emoji460]
13'—Jesus [emoji460]
15'—Jesus [emoji460]
19'—Saka [emoji460]
77’—Jesus [emoji460]️
.
ARSENAL 5-0 SEVILLA*
Screenshot_20220731-043008_OGInsta%2B.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee
MASTRAIKA WAMVURUGA ZORAN
.
Kocha Mkuu wa Simba, Zoran Maki, ameonekana ni kama hajaridhishwa na mastraika walioko na badala yake ametaka kuongezewa washambuliaji wengine ili kikosi chake kiwe tishio katika msimu ujao.
.
Zoran amesisitiza anataka atafutiwe washambuliaji wawili akiwamo namba tisa wa ukweli kutokana dili na Cesar Manzoki kuonekana kukwama na kusubiriwa kuongezwa katika dirisha dogo, jambo litakaloifanya timu isiwe na straika wa kutegemewa.
.
Awali, ilitarajiwa dili la Manzoki likamilishwe kwa Simba kutuma kigogo kwenda kuzungumza na uongozi wa Vipers ya Uganda inayommiliki mchezaji huyo, lakini mambo yamekwama kwa sababu klabu hiyo ya Uganda inataka ilipwe Dola 200,000(Sh 466 milioni) kwa miezi miwili iliyobaki ya mkataba wake.
Screenshot_20220731-043209_OGInsta%2B.jpg
 
ZORAN AMKOMALIA BOCCO
.
Kocha Zoran Maki ameendelea kugawa dozi kwa wachezaji wa Simba huku akimkomalia Bocco, akimtaka kuchagua moja kati ya kucheza mpira na kubakishwa kambini au awafuate kina Kagere, Mugalu na Thadeo Lwanga waliofyekwa Misri.
.
Inadaiwa Bocco amekuwa akitegea sehemu ya mazoezi ya timu na inadaiwa imemfanya kocha huyo kukaa naye na kumtaka achague kucheza au kama anasumbuliwa na majeraha basi atafutiwe matibabu haraka kabla ya kufanya uamuzi wa kubaki naye Msimbazi au kufyekwa kama alivyofanywa kwa kina Mugalu waliorejeshwa nchini.
Screenshot_20220731-043327_OGInsta%2B.jpg
 
BANGALA ANASIKILIZIA KAMA MAYELE
.
Mchezaji Bora wa msimu uliopita Yannick Bangala akiwa pia ndiye Kiungo Bora wa Ligi Kuu alitua Yanga msimu uliopita kutoka Far Rabat ya Morocco kwa mkataba wa miaka miwili na ameshatumikia mwaka mmoja hadi sasa, huku ikielezwa alikuwa akitaka kuboreshewa maslahi kabla ya kusaini mkataba mpya.
.
“Jamaa kesharudi na juzi alikutana na viongozi ili kujadilia ishu zake za mkataba mpya, lakini hawakupata muafaka na sasa anamsikilizia GSM, ili kuweka mambo sawa”
.
“Nadhani kila kitu kitaenda sawa kama ilivyokuwa kwa Fiston Mayele ambaye anatarajiwa kusaini mkataba mpya Agosti, ingawa wamekubaliana na kigogo (GSM) kila kitu ikiwamo kuongezewa mshahara kutoka ule wa awali ,” Chanzo makini ndani ya Yanga.
Screenshot_20220731-044156_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji599] Manchester City ina mpango wa kuachana na mchakato wa kuiwania saini ya beki wa kushoto wa Brighton, Mhispania [emoji633] Marc Cucurella mwenye umri wa miaka 24, katika dirisha hili.
.
Man City inataka kufanya hivyo baada ya Brighton kugoma kushusha bei. Timu hiyo inahitaji kiasi kisichopungua Pauni 50 milioni ili kumuuza.

…………….
Screenshot_20220731-044325_OGInsta%2B.jpg
 
PIQUE AAMBIWA AONDOKE TU BARCA
.
Kocha wa Barcelona, Xavi amemwambia Gerard Pique itakuwa vyema kama ataondoka tu mwenyewe kwenye timu hiyo baada ya klabu kumsajili beki mwingine, Jules Kounde, imeelezwa.
.
Pique, 35, amepoteza namba kwenye kikosi cha Barcelona kutokana na kuwa na mambo mengi nje ya uwanja na kuonyesha lugha ya picha ya kutohitaji kucheza alipopewa nafasi.
.
Kwa mujibu wa Sport, Xavi amemwambia Pique, ambaye walicheza pamoja kabla ya kuwa kocha kwamba itakuwa uamuzi wa busara sana kama ataamua kuondoka kwenye timu hiyo katika dirisha hili la uhamisho.
.
Kuja kwa Kounde kutamfanya Pique kuwa chaguo la tano la Xavi katika beki ya kati baada ya Kounde, Andreas Christensen, Ronald Araujo na Eric Garcia.
Screenshot_20220731-044423_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578] Juma Ayo

Niliwahi kuandika miezi kadhaa nyuma kuondoka kwa senzo.
Wasiojua walinitukana sana..anyway kila la kheri senzo kesho nitaandika kinachomuondoa Senzo.
Screenshot_20220731-044810_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20220731-044850_OGInsta%2B.jpg
 
Hakuna maelekezo mapya, kama umekuja EPL kwa kushawishiwa [emoji3]
Screenshot_20220731-045110_OGInsta%2B.jpg
 
SELEMAN KIDUNDA BINGWA WA WBF INTERCONTINENTAL [emoji599]

Amemchapa Tshimanga Katompa kutoka Kongo
Screenshot_20220731-045219_OGInsta%2B.jpg
 
Benny McCathy amejumuishwa kwenye bench la ufundi la Manchester United akiwa ni Kocha wa timu ya kwanza huku kazi yake ni kufundisha washambuliaji

Kutoka Amazulu nchini Afrika Kusini mpaka kumfundisha CR7
Screenshot_20220731-045310_OGInsta%2B.jpg
 
Back
Top Bottom