[emoji3578] farhan Jr
Ilikuwa lazima uwe na Mwanamke kama Kajala ili kupenya kwenye masikio ya Bongo Movies ambapo kuna fan base kubwa
Ilikuwa lazima awe na Kajala ili kutrend na kusikika kila uchwao kupitia online medias na electronic media, kwakuwa Kajala alikuwepo mjini wakati Harmo yupo Kusini
Kwakuwa Harmo tayari alikuwa na timu yake ya watu wake walioshibana sana, timu ya Wana ambao sio tu wafanyakazi wenzake, hapo ana uhakika ramani ya vita haiuzwi kirahisi
Umenielewa Mtu wangu? Anachokifanya Harmo ndicho alikuwa anakifanya Bro ake Diamond, alihakikisha ana Wema kisha akawa na Rommy Jons na Ricardo ambao ni Ndugu kulinda ramani ya vita
Ndicho Harmo anakifanya kwa uzuri mnoo, hajakosea hata kitu kimoja ana Jabulant ana Chopa ana DJ Seven wote hao ni Wana since wayback wanamfahamu kama Rajabu na sio Harmonize
Kitu cha mwisho ni HIT SONGS, Harmonize kwasasa anatoa HITS tena kali sana, Harmo anatunga sana, anaimba kila aina ya mziki, kapiga Gospel, singeli, Hiphop mpaka Pop, anasikika sehemu zote
Kwa muda mchache tayari ana hits kama 30, hii ni moja kati ya talent kubwa sana, binafsi namuelewa sana ana kitu tena kikubwa mno na anazidi kupenya
Kaisikilize ngoma yake ya MISS BANTU pale Youtube au digital platforms ni banger[emoji119] binafsi namuona ana njaa na huu mziki, njaa ambayo Diamond aliwahi kuionesha miaka 10 nyuma, ilikuwa usiku na mchana ni mziki
Ni njia zile zile, njaa ile ile na script ile ile sema kwasasa ni mtoto wa Mtwara