Makapuku Forum

Makapuku Forum

𝗧𝗢 𝗧𝗛𝗘 𝗦𝗘𝗠𝗜𝗦! [emoji3504][emoji736] AL AHLY

Wanafuzu nusu kwa mara ya tatu mfululizo, wakifukuzia pia kombe la tatu mfululizo

FT| RAJA 1-1 AHLY
AGGREGATE: 2-3
Screenshot_20220423-062548_OGInsta%2B.jpg
 
Safari ilienda vizuri, wachezaji wote wapo salama. Changamoto pekee tuliyokutananayo ni ya kiusalama, timu inapofika ugenini kitu cha kwanza ni ulinzi na usalama. Tulinyimwa escort wakati tunawasili kwenda hotelini na tumenyimwa tena escort wakati tunaenda mazoezini

Tukaamua kupambana kwa kushirikiana na wadau akiwemo Balozi wa Tanzania na tumeamua kukodi gari la ulinzi. Lazima uwe na ‘Plan B’ kwa hiyo kama klabu tumefanikiwa kwa yale ambayo tulikuwa tumepanga kufanya tukiwa huku.

Tunataka kufuzu, kama tutapata matokeo ya sare au ushindi japo hatujui mwalimu amepanga nini, kwenye eneo hilo tumemwachia yeye.

- Barbara Gonzalez Mtendaji Mkuu Simba
Screenshot_20220423-062736_OGInsta%2B.jpg
 
Baraza la Seneti katika Jimbo la Tennessee nchini Marekani, limepitisha sheria ambayo itahitaji Mtu aliyepatikana na hatia ya kuua kwa ajali ya gari kutokana na ulevi, kulipia matumizi ya Mtoto ikiwa Mtu huyo atamuua Mzazi wake.

Sheria hii mpya iliwasilishwa mwezi mmoja kabla ya kuhukumiwa kwa Janet Hinds, ambaye alikuwa akiendesha gari akiwa amelewa pale alipomgonga na kumuua afisa wa polisi wa eneo la Chattanooga, Nicholas Galinger mnamo Februari 23, 2019.

Tangu Mtuhumiwa atoroke kwenye eneo la tukio, mamlaka haikuweza kubaini kiwango cha pombe katika damu yake wakati huo lakini picha za camera za usalama zilizopatikana kutoka kwenye baa aliyotembelea kabla ya kuingia kwenye gari, zinaonesha alikunywa vinywaji tano, ambayo ni sawasawa na pack moja ya bia sita na shots za pombe kali, kwa mda usiozidi saa masaa manne.

Hinds alitiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha miaka 11 jela, Familia ya Polis huyo ambae alikuwa na Watoto wawili, ilifungua kesi dhidi ya Hinds, taasisi iliyomhudumia, na jiji la Chattanooga. Walikuwa wakidai $25 milioni, baada ya Hinds kuhukumiwa, familia iliashiria dhamira yao ya kuongeza ombi lao kwa mara mbili, ili kukidhi mahitaji yao.
Screenshot_20220423-063216_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wafanye ziara kwenye masoko na maduka ili kupata hali halisi ya bei za bidhaa na wachukue hatua kudhibiti upandaji holela wa bei hizo.

Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo Ijumaa, Aprili 22, 2022 wakati akizungumza na viongozi wa mikoa na wilaya kuhusu maendeleo ya maandalizi ya Sensa ya Watu na Makazi kwenye kikao kazi alichokiendesha kwa njia ya mitandao (video conference) kutokea ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma.

“Tumepata malalamiko kutoka kwa wananchi kwamba bidhaa nyingi zimepanda bei, ninyi ni Wenyeviti wa Kamati za Bei na Kamati za Kodi kwenye mikoa na wilaya zenu, upandaji wa bei sasa umekuwa holela, ni jukumu lenu kufanya ufuatiliaji wa bei za mazao katika masoko yenu"

Waziri Mkuu amesema ziko bidhaa ambazo zinazalishwa nchini kama vile nondo au saruji ambazo hazipaswi kupanda bei hasa baada ya kutolewa tamko na Waziri wa Fedha na Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara kwamba wameshaongea na wenye viwanda na wakakubaliana kuwa bidhaa zote za ndani zinapata nafuu ya kodi.

“Sasa iweje hali iendelee kuwa vilevile?”, vyakula vinavyozalishwa nchini kama mchele, Shinyanga mchele mwingi, Tabora mchele mwingi, Mbeya nako mchele mwingi kuna sababu gani ya kupadisha mchele wakati unazalishwa nchini?, kama ni mahindi au mihogo inalimwa huko kwenu, umbali wa mazao yanakolimwa mnaujua, iweje bei zipande? mpite kwenye masoko na kwenye maduka mpate bei za kila siku za maeneo yenu"
Screenshot_20220423-063319_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa Bungeni Dodoma leo amewatoa wasiwasi Watu wanaopata changamoto ya kuomba ajira zilizoidhinishwa hivi karibuni na Rais Samia, kwa njia ya mtandao na amesema mfumo unashughulikiwa ili ukawe sawa.

"Mfumo wa kuomba ajira online siku ya mwanzo kwasababu wanaoomba ni wengi kuna changamoto ya mtandao lakini timu yangu inafanya kazi kwa jithihada kubwa kuhakikisha wanaoomba kwa mtandao inaenda vizuri na Mimi nikitoka hapa naenda wanapofanyia kazi kujiridhisha marekebisho yanafanyika ili wanaoomba waombe kwa urahisi kupitia mtandao"

Juzi Waziri Bashungwa alitangaza Bungeni leo kwamba Rais Samia ametoa idhini ya ajira za Watumishi wa Sekta ya Elimu na Afya 17,412 ambapo nafasi 9,800 ni za Walimu na 7,612 ni za kada za afya ambao wataajiriwa katika mwaka huu wa Fedha 2021/22 na aliwataka wenye sifa waombe nafasi hizo.
Screenshot_20220423-063413_OGInsta%2B.jpg
 
Back
Top Bottom