BAKARI MWAMNYETO TRANSFER UPDATE
Ni kweli kuwa Kitasa Bakari Mwamnyeto anaelekea mwisho wa mkataba wake pale Yanga Afrika, mwishoni mwa msimu huu
Yanga bado wanahitaji huduma ya nyota huyo na tayari walishafanya mazungumzo na Wakala wake Kassa Mussa (ambaye pia ni Shemeji yake) anaeishi nchini Italia
Wakala wa Bakari atawasili nchini mnamo mwezi wa tano kwa ajili ya mazungumzo na klabu ya Yanga kuhusu mkataba mpya wa Bakari Nondo na ofa zilizopo mezani
Klabu ambazo tayari zimeulizia huduma ya Bakari Nondo ni za nchini Misri, ambazo ziliamua kusubiri mpaka amalize mkataba wake kuepusha gharama kubwa za usajili
Kipingamizi kikubwa ni ‘offer matching’ ikiaminika upande wa Bakari utatazama kile ambacho Yanga wataleta mezani na kile ambacho klabu za Misri zitaleta mezani, ndipo maamuzi yatafanyika
Taarifa za uhakika kabisa ni kuwa SIMBA hawajatuma ofa yoyote kwa Wakala wa Bakari Nondo kuhusu kuinasa saini yake wala Simba hawajaonesha interests zozote kwa siku za hivi karibuni
Kama kuna uwezekano wa Simba kuanza mchakato basi ni mwishoni mwa msimu ila mpaka sasa hakuna mpango wowote
Hali ilivyo mpaka sasa kuna uwezekano mkubwa wa Bakari kuongeza kandarasi makutano ya Twiga na Jangwani, anatazamwa kama Mchezaji muhimu kikosini na Project ipo pembeni mwake