

Shaffih Dauda
JE SIMBA NI BORA AU LIGI NI BORA? -
THE FIRST PARAMETER - FANS (MASHABIKI)
Jana wakati natoa hoja yangu kuhusu uwakilishi wa Tanzania kwenye soka la kimataifa ngazi ya klabu, nilijibu swali kuwa sio kwamba Ligi yetu ni bora bali Mwakilishi wetu ambaye ni SIMBA yeye ndie bora
Nikaja kwenye argument kuhusu nini kifanyike ili wengine wafike kwa Simba? Kwangu ni kuwa sio mchakato wa muda mfupi, sio mchakato wa kulala na kuamka bali hapa unahitaji ujasiliamali wa muda (Entrepreneurship of time)
Simba walianza kwenye sehemu nane, leo nitawaambia kitu kuhusu MASHABIKI NA WANACHAMA
Hapa kuna vichwa vitatu muhimu, huko nyuma Simba walikuwa na Mashabiki wao ila incorporation ya Mashabiki moja kwa moja karibu na brand yao ilikuwa kazi nzuri ya Bwana @football_senzo , @hashimbaga na @hajismanara
Investment ambayo Simba amefanya kwenye kitengo cha Mashabiki ni bajeti ya klabu nyingi tu nchini, massive investment ili upate matokeo
YEES! Format ya Simba kwa Mashabiki wao ndio ile inayotumika Afrika Kusini kwa klabu kubwa kama Pirates, Amakhosi na Mamelodi Sundowns, kupitia Idara ya Mashabiki na Wanachama with close link na Habari, hichi wamefanikiwa sana
Kuna muda Simba ilimgeuza Shabiki wake kuwa mteja wa klabu, ikaleta Utamaduni wa kununua merchandise, kuifuatilia klabu kwa kila kitu, hii iliiuza bidhaa yao ndio maana wana numbers nzuri kwenye social networks mpaka mauzo ya jezi
Transformation ya Shabiki kuwa Mteja inatengeneza demand kubwa ya timu kupata matokeo na kukimbizana na malengo yake, specifying mfano ni Real Madrid, Barcelona, Chelsea, Bayern na wengine wengi, popular demands ni popular investments with results
Brand yao inazungumzika, inafanya klabu iwe na project imara, leo hii Simba hata ukiwaambia mechi ni saa sita usiku watu watafika uwanjani, leo hii Simba hata utoe jezi tofauti mara nne kwa msimu bado Mashabiki watanunua
Simba ameifanya bidhaa yake iwe hitaji, amevuna sana, hii ndio silaha yake kubwa kuwa na Mchezaji wa 12, tukifanya utafiti miaka miwili ijayo Simba huenda ikawa na Mashabiki wengi zaidi nchini, kwa kutumia kigezo cha POPULATION PYRAMID kwa wingi wa vijana
I rest my case for today, tumeanza 1/8
WHEN DIGALA SPEAKS, YOU LISTEN
View attachment 2178208