Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220311-074355_Opera%20Mini.jpg
 
KISINDA: TUNATAKA POINTI KWA MKAPA
.
Winga wa RS Berkane, Tuisila Kisinda amesema: “Tunafahamu mechi ya Jumapili, itakuwa ngumu pengine zaidi ya kule kwao ila tunachohitaji kupata ni pointi.
Screenshot_20220311-113506_Instagram.jpg
 
POCHE KUTI KAVU PSG
.
Imethibitisha kwamba watu ambao wana asilimia 80 za kufukuzwa kwenye viunga vya PSG ni kocha Muargentina Mauricio Pochettino sambamba na mkurugenzi wa michezo wa timu hiyo, Leonardo.
.
Inaelezwa kuwa lengo la Pochettino kusajiliwa kwenye kikosi hicho ilikuwa ni kwenda kuipa taji hilo la Ulaya ndio maana wakasajiliwa wachezaji wengi bora ili kumpa nguvu ya kufanikisha suala hilo, hivyo kushindwa kwake ni sababu itakayomfanya kuondolewa yeye na mkurugenzi wa michezo.
.
Baada ya mechi, Rais wa PSG, Nasser Al-Khelaifi, alionekana kuwa na hasira sana kwa mujibu wa mwandishi wa habari aliyekuwa karibu naye. Inadaiwa tajiri huyo alichukua hadi jukumu la kwenda kwenye vyumba vya kubadilishia waamuzi kwa lengo la kuwalaumu kwamba hawakuitendea haki timu yake.
.
Huenda Pochettino akarudi England ila mara hii kuifundisha Man United.
Screenshot_20220311-113832_Instagram.jpg
 
VIGOGO wa Manchester United wamemuweka kwenye rada zao straika wa Bayern Munich na Poland, Robert Lewandowski, 33, ili kuipata saini yake katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi.

Mkataba wa sasa wa fundi huyo unatarajiwa kumalizika mwaka 2023, na Munich imeonekana kuwa tayari kumuachia ikiwa timu yoyote itaonyesha nia ya kutaka kumsajili kwa sababu staa huyo ameshawasilisha maombi ya kutaka kuondoka.

Lewandowski ameomba kuondoka mwisho wa msimu ambapo mbali ya Man United kumekuwa na timu nyingine kutoka England kama Man City na Chelsea ambazo amekuwa akihusishwa nazo sana.
Screenshot_20220311-114717_Instagram.jpg
 
WIKI moja kabla ya KMC iingie uwanjani kucheza na vinara wa Ligi Kuu Yanga, Kocha Mkuu wa timu hiyo, Thiery Hitimana amewaingiza chimbo wachezaji na kuwapa mbinu tofauti ili kuhakikisha wanashinda mechi hiyo.

Akizungumza na Mwanaspoti, Hitimana alisema kuwa mchezo na Coastal walihitaji kushinda ili kuwapa wachezaji morali kabla ya kuikabili Yanga lakini ilishindikana na sasa ameingia kambini kuijenga timu kuanzia saikolojia hadi mbinu ili kuhakikisha inashinda.

“Tumeamua kufanya hivyo ili kuwajenga zaidi wachezaji wetu. Tunajua ukubwa wa Yanga lakini tunahitaji kushinda dhidi yao hivyo tutakaa vizuri na wachezaji tuwaweke sawa kiakili ili waweze kuwa na hali ya kujiamini katika mechi hiyo,” alisema Thiery

Screenshot_20220311-114917_Instagram.jpg
 
Kiungo wa Aston Villa, Philipe Coutinho ameonyesha kiwango bora sana toka arudi katika Ligi Kuu ya Englan baada ya kutokuwa na msimu mzuru Barcelona.
Katika michezo nane aliyocheza toka ajiunge na Villa amefunga mabao 4 na kutoa Assist 3.
Screenshot_20220311-115354_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom