PIGO: Mwakinyo, Ibra Class Wavuliwa Mikanda
.
Habari mbaya kwa mabondia bora nchini, Hassan Mwakinyo na Ibrahim Class ni kuvuliwa kwa mataji ya ubingwa wa WBF.
.
Mabondia hao wamevuliwa mikanda hiyo ya ubingwa na Shirikisho la ngumi za kulipwa la dunia la WBF. Taarifa iliyotolewa na WBF imeeleza kuwa mabondia hao si mabingwa tena wa mikanda ya WBF kwenye uzani wa super welter na super feather ambayo walikuwa wakiishikilia Mwakinyo na Class hivyo iko wazi.
.
“WBF tumeumizwa na hiki kilichotokea, lakini kwa mujibu wa kanuni, hawa si mabingwa wetu tena baada ya kushindwa kutetea ubingwa kwao kwa wakati,”