Polisi mijini Free Town nchini Siera Leone wamekesha kulinda nyuma ya mshambuliaji wa timu ya Taifa ya nchi hiyo Kei Kamara aliekosa penati kwenye mchezo dhidi ya Equatorial Guinea.
Mashabiki hao walitaka kuichoma moto nyumba hiyo kwasababu tu mchezaji huyo alikosa penati na kusababisha timu yao ya Taifa kutolewa kwenye michuano ya AFCON huko nchini Cameroon.
CONFIRMED: POLISI, YANGA KUPIGWA ARUSHA
.
Uongozi wa timu ya soka ya Polisi Tanzania umethibitisha kupeleka mchezo wao dhidi ya Yanga katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.
.
Mchezo huo ulipangwa kupigwa Jumapili katika uwanja wao wa Ushirika lakini siku moja kabla ya mchezo yani Jumamosi kutakuwa na tamasha la Utamaduni Mkoa wa Kilimanjaro ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan hivyo imeilazimu uongozi wa timu hiyo kuhamishia mechi hiyo Arusha.
.
Inaweza kuwa ni habari njema kwa Yanga kwani wenyewe tayari wameweka kambi Arusha kujiandaa na mchezo huo.
Wachezaji wa Simba, Jonas Mkude na Kibu Denis hawatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kitakachosafiri kuelekea Morogoro kwa ajili ya mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar, Siku ya Jumamosi kufuatia kuwa majeruhi.
Wachezaji hao walipata majeraha katika mechi dhidi ya Mbeya City ambapo walishindwa kuendelea na mchezo kipindi cha pili.
Taarifa ya Klabu ya Simba imeeleza kuwa, nyota hao wanaendelea vizuri na wamepumzishwa iii hali zao zirejee katika utimamu na wanatarajia kuwepo katika michezo itakayofuata.
PIGO: Mwakinyo, Ibra Class Wavuliwa Mikanda
.
Habari mbaya kwa mabondia bora nchini, Hassan Mwakinyo na Ibrahim Class ni kuvuliwa kwa mataji ya ubingwa wa WBF.
.
Mabondia hao wamevuliwa mikanda hiyo ya ubingwa na Shirikisho la ngumi za kulipwa la dunia la WBF. Taarifa iliyotolewa na WBF imeeleza kuwa mabondia hao si mabingwa tena wa mikanda ya WBF kwenye uzani wa super welter na super feather ambayo walikuwa wakiishikilia Mwakinyo na Class hivyo iko wazi.
.
“WBF tumeumizwa na hiki kilichotokea, lakini kwa mujibu wa kanuni, hawa si mabingwa wetu tena baada ya kushindwa kutetea ubingwa kwao kwa wakati,”
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.