

Farhan Jr
USIKU WA ABUNUASI NA NDOTO ZAKE
Ilikuwaje alipoamka ule usiku wa manane baada ya ndoto ndefu ya kutisha? Najua alipoamka mlimpa maji na kumwambia ajikaze awasimulie
Anasema mwisho wa gili yetu aliona Braza wetu wa jeans kuchanika akishangilia, aliona 'wakazi' wakifurahi kwa nderemo na vifijo, ama kweli mwaka wao huu
Anasema ndotoni aliwaona wakiripoti kwenye chiko lenye rangi ya theluji, mwanzo walifika kusalimia, baadae wakaja kuleta shida zao
Siku ya tatu wakasaidiwa shida na siku ya nne walipaswa na wao kusaidia kutatua shida! Kwani Mwalimu historia si alisema There's no free lunch in capitalist system
Anasema ndotoni alimuona Dada mmoja mrembo sana tena na niwami yake usoni, wengine wanasema Dada kamind kuhusu ile clip ya leyema Wachezaji wakishangilia inaonekana wameipenda, we si ndio unapenda Uafrika na kuutukuza Uzungu
Lakini shida nini? Watu wamesahau the game is fair play?? Tena kwenye ndoto anasema hata wale Wazee wa habari kiganjani huenda wakala pin wasifike mazoezini, ni hatari lakini salama, bwana we ndio hatari ya degree za 'Michuu' kuongoza mpira
Nasikia aliota kwa muda mrefu, kipi kingine tena? Nasikia yule Mnyama BIG FIVE mbugani anaitaka ndoo ya tano tena! Lakini katika hali ya kawaida, kibinadamu na kiungwana wetu wa 'Kiafrika' nadhani haiwezekani
Shida nini kwani? Hakuna shida ila ni ngumu chapati kuchomwa tu upande mmoja, ndoto inasema raha ya chapati ichomwe pande zote, Ili tupate KURA hapana sorry, namaanisha KULA
Kwahiyo?? Nasikia mzigo tayari umewekwa! Kwani ndoto inasemaje?? Ndoto inasema Kuna akaunti maalum, ile faida ndio inaenda kwa Mnyama BIG FIVE, lakini sina uhakika maana ni ndoto tu
Kumbuka wewe Mtoto Bado Mdogo ujue?? Basi tu naomba ufahamu Wangindo sisi tunasema "Ndumba ya mtoto Mkubwa anakula, Ndumba ya Mkubwa na Mtoto anakula"