Makapuku Forum

Screenshot_20211203-044924_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20211203-045015_Opera%20Mini.jpg
 
Mfalme wa Bongofleva Alikiba amethibitisha kwamba atakuwepo kwenye show ya Bata la Dar, Mama ongea na mwanao Jumamosi hii Leaders Club Dar es salaam, mbali na Alikiba Wasanii wengine kama Profesa J, G Nako, Lord Eyes, Country Wizzy, Ibrah na Angela kutoka Konde Gang na Dulla Makabila ni sehemu ya Wasanii 50 watao-kuwepo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla ndio ataongoza Bata hili kwa Wakazi wa Dar na Wageni Jumamosi hii, kula, kunywa na kugonga cheers kwenye show hii kubwa ya kufungia mwaka.
Screenshot_20211203-051320_Instagram.jpg
 
Mamlaka ya usimamizi wa dawa nchini Uingereza imeidhinisha dawa zinazozalishwa na kampuni ya GlaxoSmithKline, GSK kutibu kundi lililo hatarini kupata dalili mbaya za maambukizi ya COVID-19 huku mzalishaji huyo akisema dawa yake imeonekana kuwa na ufanisi wa kukabiliana na kirusi kipya aina ya Omicron.

Kampuni hiyo ya GSK imesema takwimu ya kitiba za wali zimeonyesha kwamba tiba ya sotrovimab hudhoofisha nguvu ya kirusi hicho kujibadilisha na kuongeza kuwa majaribio bado yanaendelea ikitaraji kutoa matokeo kamili ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Dozi moja ya dawa hiyo ilionekana kupunguza hatari ya wagonjwa kulazwa hospitalini na vifo kwa asilimia 79 kwa watu wazima walio katika hatari kubwa ya kupata kuambukizwa COVID-19.
Screenshot_20211203-051448_Instagram.jpg
 
CloudsFM leo December 2 2021 imetimiza miaka 22 tangu kuanzishwa kwake, miaka 22 ya ubunifu na mapinduzi kwenye burudani nchini Tanzania, miaka 22 ya kuwafungulia dunia Vijana ambao hawakuwa wanapata nafasi kwenye Radio nyingine.... miaka 22 ya kusambazia Watanzania michongo isiyoisha.

Mkurugenzi wa Clouds Media Group Joseph Kusaga amesema "Shukrani kubwa sana kwa Mungu, kwa Familia yangu, Wanafamilia nzima wa Clouds, Watanzania wote waliotuamini, Rais wetu Mama Samia kwa kutuamini, kutusaidia na kutuongoza, shukrani zangu nyingine ziende kwa Rais wetu wa Znz Dr. Hussein Mwinyi, Hayati Benjamin Mkapa, Hayati Dr. Magufuli na Mzee wetu Dr. Jakaya Kikwete"

Sherehe hizi za miaka 22 ya Clouds zimenogeshwa na michongo mitatu mikuu iliyotangazwa leo asubuhi na Mwenyekiti wa Kamati ya Michongo Seba Maganga ambapo ni mchongo wa zawadi zenye thamani ya milioni 250, mchongo wa kurejesha tabasamu kwa Watanzania waliokwama kwenye changamoto pamoja na mchongo mkuu wa pesa cash wa milioni 500 kupitia package ya Mchongo Pesa.
Screenshot_20211203-051752_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

SIMU YA PROFESA, SIMBA VS GEITA

Kwanza kabisa lile ni goli la wazi kabisa ambalo Geita wamenyimwa na LINE 1, sio kosa la Mwamuzi wa kati bali LINE 1

Baada ya mpira kuwekwa tu kimiani, Mwamuzi wa kati aligeuka kuonesha Kati kabla ya LINE 1 Kigoma kuwa ni faulo, ila Mwamuzi wa kati alipitisha kuwa ni goli ila shida ya Msaidizi wake

Turning point ya mchezo wa leo ni baada ya kumtoa Rally Bwalya, hauwezi kuwa na timu ya Mzamiru, Mkude, Kibu wote ndani bila kuwa na Mpishi mmoja ambaye ni Bwalya

Ikawa ni rahisi sana kwa Geita kuwazidi Simba eneo la Kati, ndipo hapo Yusuph Kagoma na Nashon Naftali walipopata nafasi ya kucheza mpira wao kirahisi sana

Nimemtazama vyema sana John Bocco, changamoto yake leo ni ya kimfumo Wala sio kwamba ameisha hivyo! Simba inacheza zaidi kutokea pembeni na setpieces

Nilikuwepo uwanjani, nikawa namtazama Bocco wakati timu inafanya transition, mara nyingi alijikuta off position ama mpira anapewa kwenye Watu! Bocco sio holder mzuri wa mpira, anahitaji kusimama huduma zije

Defense ya Simba leo ilivuja sana na ndio ilikuwa inakaribisha mashambulizi, shukrani kwa mikono ya Aishi Manula! Shida ya kwanza ni mstari Kati ya Banda na Gadiel, Kulikuwa na gap kubwa sana

Shida nyingine ni beki ya Kati! Onyango na Juma wazuri sana ila wanamkosa Kiongozi mmoja, kuna muda walikuwa wanafuatana sana na kufanya uwanja uwe mkubwa sana

Hata pale waliposhambuliwa sana walistick bado kwenye pass fupi ama kubutua, ile akili ya Pascal Wawa inahitajika mapema, uwezo wa pass na kusoma Mchezo ila tu juu yake awepo Onyango au Juma

Peter Banda ni exceptional talent kama nisemavyo siku zote ijapo mlinitukana sana ila muda utaongea
Screenshot_20211203-061612_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Mkataba wa Bernard Morrison na Simba unafikia tamati Agosti 2022, ulikuwa ni mkataba wa miaka miwili

Pande zote mbili, Simba na Morrison hawajaanza mazungumzo ya mkataba mpya mpaka sasa

Ila pande zote mbili hazina shaka yoyote juu ya mazungumzo ya mkataba mpya na Morrison kuongeza kandarasi yake

Simba kwasasa wanawaza zaidi kutetea ubingwa wao na kufanya vyema kwenye michuano ya Afrika, vivo hivyo kwa Morrison mwenyewe

Simba wameendelea kusisitiza kwamba Mchezaji yoyote muhimu na tegemeo ndani ya Simba hawezi kuondoka kuelekea timu yoyote nchini

Wachezaji wote ambao mikataba inaelekea mwisho na bado wanahitajika kwa mapendekezo ya Mwalimu basi watasalia
Screenshot_20211203-061842_Instagram.jpg
 
Mamlaka ya usimamizi wa dawa nchini Uingereza imeidhinisha dawa zinazozalishwa na kampuni ya GlaxoSmithKline, GSK kutibu kundi lililo hatarini kupata dalili mbaya za maambukizi ya COVID-19 huku mzalishaji huyo akisema dawa yake imeonekana kuwa na ufanisi wa kukabiliana na kirusi kipya aina ya Omicron.

Kampuni hiyo ya GSK imesema takwimu ya kitiba za wali zimeonyesha kwamba tiba ya sotrovimab hudhoofisha nguvu ya kirusi hicho kujibadilisha na kuongeza kuwa majaribio bado yanaendelea ikitaraji kutoa matokeo kamili ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Dozi moja ya dawa hiyo ilionekana kupunguza hatari ya wagonjwa kulazwa hospitalini na vifo kwa asilimia 79 kwa watu wazima walio katika hatari kubwa ya kupata kuambukizwa COVID-19.View attachment 2031054
Na sisi tutengeneze kirusi chetu...

Tufanye biashara ya chanjo...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom