Makapuku Forum

Makapuku Forum

View attachment 1969816
Screenshot_20211010-054344_Opera%20Mini.jpg
 
Wakulima wa Korosho katika Kata ya Nachunyu Halmashauri ya Mtama Mkoani Lindi leo October 09,2021 wamegoma kuuza korosho zao Tani 1,895 na kilo 579 kwenye mnada uliofanyika ghala la chama cha ushirika Natam Amcos kutokana na kutoridhika na bei ndogo ya Wanunuzi ambapo bei ya juu ni Tsh. 2275 na ya chini Tsh 2010.

Mnada wa kwanza wa korosho kwa msimu wa 2021/2022 ulifanyika Jana katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Newala Mkoani Mtwara chini ya Chama Kikuu cha Ushirika cha TANECU ambapo Wakulima walikubali kuuza korosho zao kwa bei ya juu ya Tsh. 2445 huku bei ya chini ikiwa ni Tsh. 2231 ambapo Kampuni zilizojitokeza kununua ni 15 na jumla ya tani 1486 ziliuzwa. View attachment 1969807
Sisi wakulima tulio chama cha msingi Masasi wala hatuna noma msimu huu, hatukopwi
 
Msimamo wa Kundi J la Taifa Stars lilivyo kwa sasa katika kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar, bado Stars imebakiza michezo miwili vs Madagascar ugenini na Congo DR nyumbani, Tanzania inatakiwa kumaliza kinara ili icheze play off ya kufuzu Kombe la Dunia.
Screenshot_20211011-042818_Instagram.jpg
 
Mamlaka ya Taliban jana, Jumamosi imeionya Marekani kuwa isiwavuruge, hayo yamejiri wakati wa mkutano kati ya Taliban na Marekani ukiwa ni mkutano wa kwanza wa ana kwa ana kufanyika tangu Marekani iondokea katika ardhi ya Afghanistan, huku kuongezeka kwa mauji ya kimadhehebu kukizusha maswali juu ya kushika kwao madaraka.

Baada ya mazungumzo hayo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Taliban, Amir Khan Muttaqi aliliambia shirika la habari la Afghanistan kwamba waliwaambia wazi kabisa Marekani kujaribu kuivuruga Serikali ya Afghanistan haina tija kwa yeyote na kwamba uhusiano mzuri kwa Taifa hilo ndio litakuwa jambo jema kwa pande zote.

Waziri huyo ambae pia alinukuliwa na Shirika la Habari la Ufaransa AFP aliongeza kusema kuwa hakuna sababu ya kuidhoofisha Serikali iliyopo nchini Afghanistan, kwakuwa hilo litasababisha matatizo kwa umma wa Watu.

Wakati Taliban ikitafuta kutambuliwa Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imesema ujumbe wa Marekani utaushinikiza utawala wa Taliban kuhakikisha Magaidi hawaweki kambi zao nchini Afghanistan.
Screenshot_20211011-043225_Instagram.jpg
 
Kaimu Mkurugenzi wa Magonjwa yasiyo ya kuambukiza kutoka Wizara ya Afya Shedrack Makubi amesema takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonesha Watanzania milioni saba wana matatizo ya afya ya akili huku akiutaja Mkoa wa Dar es salaam kuwa kinara kwa kuwa na Watu wengi wenye matatizo hayo.

Makubi amesema hayo Jijini Dodoma kwenye siku ya maadhimisho ya afya ya akili duniani yanayoadhimishwa Oktoba 10 kila mwaka.
Screenshot_20211011-043401_Instagram.jpg
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Magonjwa ya Akili Mirembe Dkt. Paul Lawale amewaasa akina Mama kuacha matumizi ya vilevi wanapokuwa wajawazito ili kuwanusuru Watoto walio tumboni kuzaliwa wakiwa na matatizo ya afya ya akili.

Dkt. Lawale amesema hayo Jijini Dodoma wakati akisoma tamko la siku ya maadhimisho ya afya ya akili duniani yanayoadhimishwa Oktoba 10 kila mwaka kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima.

Amesema Mama mjamzito anapokunywa pombe anamuweka hatarini mtoto atakayezaliwa kwani inaweza kumsababishia athari katika ukuaji wa ubongo kwa mtoto aliye tumboni na hivyo kumsababishia tatizo la afya ya akili pindi atakapozaliwa.

“Tunapoangalia ongezeko la watu wenye matatizo ya afya ya akili, lazima tuangalie tangu mtoto anapokuwa tumboni, wapo akina mama wengi wanatumia vilevi wanapokuwa wajawazito hii ina athari kwa mtoto aliye tumboni” ——— Dkt. Lawale.

Ameongeza kuwa Mama mjamzito anapotumia vilevi inasababisha ukuaji wa ubongo wa Mtoto kuathirika na kusababisha Mtoto kuzaliwa na matatizo ya afya ya akili na kuendelea kuongeza idadi ya wagonjwa wenye matatizo ya afya ya akili nchini.
Screenshot_20211011-043528_Instagram.jpg
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais ( Muungano na Mazingira), Selemani Jafo amepiga marufuku uingizaji, uzalishaji, usambazaji na matumizi ya mirija ya plastiki inayotumika kwenye unywaji wa maji na vinywaji baridi baada ya miezi sita kuanzia October 11, 2021 pia amesema Serikali inaelekeza wazalishaji bidhaa hizo wajielekeze kuzalisha mirija iliyo rafiki kwenye mazingira na kuepuka matumizi ya mirija ya plastiki ambayo haiwezi kurejelezeka.

"Katika kutunza na kuhifadhi mazingira, Serikali inaelekeza wenye hoteli, migahawa na maduka mbalimbali yanayotumia mirija ya plastiki katika kunywa maji na vinywaji mbalimbali, kuanza kutumia mirija ambayo ni rafiki wa mazingira ikiwemo mirija iliyotengenezwa kwa kutumia mali ghafi kama vile mirija iliyotengenezwa kwa karatasi, miti, nk."

"Baada ya miezi sita kuanzia October 11 , 2021, itakuwa ni marufuku kwa wenye hoteli, baa, na maeneo mengine ya kibiashara kuendelea kutumia mirija ya plastiki kama chombo cha kunywea vinywaji"——— JAFO
Screenshot_20211011-043758_Instagram.jpg
 
[emoji471] 2021 UEFA Nations League

[emoji471] 2018 World Cup
[emoji471] 2003 Confederations Cup
[emoji471] 2001 Confederations Cup
[emoji471] EURO 2000
[emoji471] 1998 World Cup
[emoji471] EURO 1984
Screenshot_20211011-050429_Instagram.jpg
 
[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

Captain Hlompho Kekana wa Mamelodi Sundowns alijumuishwa kwenye kikosi cha AFCON 2019 cha Bafana Bafana ila bahati mbaya hakuwa akianza kwenye kikosi

Swali la kwanza la Wanahabari ni kuwa mbona muda wote alikuwa mtiifu sana mazoezini na alikuwa anahamasisha sana wenzake? Licha ya kwamba hapati nafasi kikosini

Kekana aliwajibu kuwa kuna Kekana wawili ndani ya nafsi moja! Kuna Kekana Mcheza mpira na kuna Kekana Raia wa Afrika Kusini ambaye ni Shabiki mkubwa wa taifa lake

Captain Fantastic alimaliza maneno yake ni ilikuwa rahisi kumuelewa, kama hatoanza kama Mchezaji basi atakaa kwenye bench na kuwashangilia na kuhamasisha wenzake kwa kofia ya Uzalendo na Ushabiki kwa Taifa lake

Well leo nilitulia kwenye mechi nzuri sana kati ya Taifa Stars dhidi ya Benin! Awali ya yote nilivutiwa sana na picha iliyopostiwa na kurasa rasmi za @tanfootball , macho yangu yalinasa kwa Idi Seleman Nado

Alisimama mbele zaidi kapiga goti na umakini mkubwa akimsikiliza Kocha Kim Poulsen, ni ngumu kuamini kuwa Iddi mwenyewe anajua haanzi au hatopata nafasi ila nafsi na roho yake zipo tayari kwa ajili ya taifa lake

Ananikumbusha pia alipoulizwa David Silva kwanini alikuwa makini sana kumsikiliza Kocha Del Bosque, nae akasema ni bahati kufundishwa na Kocha kama huyo pale Hispania, kama hatoanza mbele ya wakina Iniesta na Xavi basi anapata elimu ya kwenda nayo Valencia

Tukio la pili la Iddi Seleman Nado ni pale Stars inashambuliwa, nilikuwa nastream live kupitia FIFA TV! Licha ya kuwa hachezi ila sasa yeye ndie Shabiki mkubwa wa Taifa lake wakiwa ugenini, hajasomea Ukocha ila alisimama kutoa maelekezo peke yake

Alisimama kuwakumbusha wenzake, licha ya kuwa hachezi ila walau maneno yake yatawasaidia kwenye mapambano kule Benin, bila kinyongo kwakuwa anafanya kwa ajili ya taifa lake

Nilipenda passion yake nilipenda mahaba yake kwa taifa lake hongera sana nado
jr_farhanjr-20211011-0001.jpg
 
"Kikao cha kamati kuu ya Chama kimeketi jana Oct 10, 2021 kwa njia ya kidigitali na kilikuwa na agenda kadhaa mojawapo ilikuwa hali ya siasa nchini, katika agenda hiyo pamoja na mambo mengine kamati kuu ilijadili kuhusu vikao ambavyo vimealikwa na Ofisi ya Msajili"

"Kuna kikao ambacho tumealikwa leo kupitia Baraza la Vyama vya Siasa, kimeanza leo saa tano asubuhi, Dodoma pia kuna kikao tumealikwa kinaitwa Kikao cha Wadau kitakachofanyika Oct 21-22,2021 Dodoma, mambo haya yalijadiliwa na Kamati Kuu na kuyaazimia"

"Serikali imezuia shughuli halali za vyama vya siasa na hivyo inakuwa imevunja sheria no. 5 ya Vyama vya siasa ya 1992, Kamati Kuu ya CHADEMA tumeazimia kuwa ili tukutane na Msajili wa Vyama vya Siasa ni sharti kwamba zuio la mikutano ya vyama vya siasa liondolewe"

"Hatuwezi kwenda kwenye kikao na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini wakati ambao Vyama vya siasa vimezuiwa kufanya shughuli zao za kisheria, Mwenyekiti wetu Mbowe na Wanachama wetu mamia kwa mamia wakiwa ndani" ———Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA - Bara
Screenshot_20211011-151857_Instagram.jpg
 
Gavana wa jimbo la California Gavin Newsom amesaini sheria inayopiga marufuku uvuaji kondomu bila makubaliano, hii ni baada ya kuwasilishwa kwa muswada ulioitwa "stealthing".

Sheria hii mpya inaifanya California kuwa jimbo la kwanza nchini Marekani kuidhinisha uvuaji wa kondomu bila makubaliano kuwa kosa linaloadhibiwa kisheria ambapo Mtu anaweza kumfungulia kesi Mtu akatakayevua kondomu bila makubaliano yao wakati wa tendo.
Screenshot_20211011-152945_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom