Makapuku Forum

Makapuku Forum

BARAZA ANATAKA NAFASI ZA JUU

Kocha wa Kagera Sugar Francis Baraza amsema malengo yao msimu huu ni kushika nafasi tano (5) za juu kwenye msimamo wa NBC Premier League kutokana na usajili waliofanya.

“Malengo na mipango yangu msimu huu nikiwa Kagera Sigar ni kumaliza katika tano bora na kuifanya timu iwe bora kwenye ligi ya Tanzania kutokana na vijana wanavyocheza.”

“Muunganiko wa timu na vile wanavyocheza unanifurahisha, mimi kama kocha kazi yangu ni kuwaunganisha vijana waweze kucheza vile ninavyotaka.”
Screenshot_20211012-112733_Instagram.jpg
 
Kwenye wale watatu wa mwisho pale Liverpool, Kocha hivi sasa amepata ahueni ya kufanya rotation tofauti na misimu miwili nyuma

Mane + Firmino + Salah

Hivi sasa alipo Firmino kuna Diogo Jota ameingia vyema sana, imebaki kusubiri kama Mohamed Salah ataongeza mkataba ama tofauti ila mpaka sasa mbele wamebalance
Screenshot_20211012-112824_Instagram.jpg
 
Moja wapo ya eneo ambalo Mbwana Samatta amepevuka zaidi ni namna ya kuhimili presha ya mitandao na media, wengi huwa wanateseka

Ulitegemea nini kutoka kwa Mbwana baada ya kuambiwa na Mwandishi "Watanzania wanasema haujitumi" obviously ulitarajia Mbwana awe frustrated

Lakini Mbwana alihitaji research ya Mwandishi, alete imperical data ama vivid evidence na sio maneno! Yes Mbwana alijaribu kuipangua hoja nyepesi kwa akili kubwa

Kuna aina nyingi za kuuliza maswali bila kuleta damage! Njia nzuri ni formulation around the matter, ila wengi wanalilia formulation around the Subject

Bado pia Mwandishi anaweza kureason kwa mazingira husika, hata kama ni kweli je ina umuhimu kwa sasa? Important vs Necessity! Hii ni situational analysis

Bila shaka Mbwana ametupa funzo kubwa kwa Waandishi, wanasoka na vijana maana halisi ya kuwa Professional
Screenshot_20211012-112929_Instagram.jpg
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Oktoba 12, 2021 amezindua wiki ya vijana kitaifa, Chato Mkoani Geita ambapo amesema Vijana ndio kundi kubwa kwenye nguvu kazi ya Taifa huku akitolea mfano wa utafiti uliofanyika mwaka 2014 ambao ulionesha Vijana walikua nguvu kazi ya Taifa kwa 56%, asilimia ambayo kwa sasa inaamika kuwa kubwa zaidi huku akiwafananisha Vijana na injini au magurudumu kwenye gari hivyo bila uwepo wao gari haliwezi kusogea.

"Kwa mujibu wa utafiti wa nguvu kazi ya Taifa (ILFS) wa mwaka 2014 Nchini Tanzania, vijana walibainika kuwa ndiyo kundi kubwa la nguvu kazi ya Taifa kwa asilimia 56%, kundi lenye uwezo wa kufanya kazi kwa muda mrefu, kundi lenye ubunifu, uthubutu, ujuzi na uwezo wa kufanya kazi zaidi ya moja, kwa misingi hiyo, Vijana ni injini kwa maendeleo ya Taifa na kwamba Taifa lisilokuwa na vijana ni sawa na gari lisilokuwa na magurudumu kwa kuwa haliwezi kwenda mbele"

"Serikali kutokana na umuhimu huo imeamua kusisitiza matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwenu Vijana kwani ninyi ndio Watumiaji wakubwa na Wahanga wakubwa wa TEHAMA, ni ukweli usiopingika kuwa matumizi sahihi ya TEHAMA ni nyenzo muhimu kwa maendeleo endelevu ya kiuchumi, kiutamaduni na kijamii yanayoongeza fursa za ajira, Vijana wengi wamefanikiwa kutokana na matumizi sahihi ya TEHAMA hususan kwa kufanya biashara kwa njia ya mtandao, Vijana wameweza kuanzisha na kuendesha vituo vya huduma za intaneti na pia kuanzisha Wakala wa huduma za kifedha kupitia mitandao ya simu"

"Niwakumbushe kujiepusha na matumizi yasiyo sahihi kama vile wizi na utapeli wa fedha unaofanywa kwa njia ya mtandao, kujiunga na makundi yasiyofaa, kujiingiza kwenye majukwaa ya uchochezi kati ya Mtu na Mtu, baina ya Watu na Viongozi wao lakini pia Taifa na Taifa, vitendo hivi vinavuruga amani, utulivu na mshikamano wetu kama Taifa, napenda mtumie TEHAMA kujiletea maendeleo binafsi na Taifa, pia tafuteni fursa za kiuchumi kupitia TEHAMA na siyo kufanya mambo yasiyofaa kupitia Mitandao" ——— Waziri Mkuu Majaliwa, Chato leo
Screenshot_20211012-182836_Instagram.jpg
 
Club ya Yanga SC imepigwa faini ya USD 5000 (Tsh milioni 11.5) na Shirikisho la soka Afrika (CAF) kutokana na kukiuka baadhi ya taratibu ikiweko kuingiza Mashabiki tofauti na maagizo ya kanuni za corona kutoka CAF, kosa jingine ni kushambuliwa kwa mmoja kati ya Viongozi wa Timu ya Rivers United ya Nigeria ambae inadaiwa alishambuliwa na mmoja wa Walinzi wa uwanjani kabla ya mechi vs River United iliyochezwa Dar es salaam.
Screenshot_20211012-183012_Instagram.jpg
 
Mwanafunzi wa chuo cha ufundi stadi Veta Kihonda Manispaa ya Morogoro, Martin Mushi mwenye umri wa miaka 21 amefariki dunia baada ya kuzama wakati akiogelea wenye bwawa lililopo jirani na chuo hicho.

Akizungumzia tukio hilo leo Oktoba12, Kamanda wa kikosi cha zimamoto na uokoaji mkoa wa Morogoro, Goodluck Zelote amesema kuwa tukio hilo lilitokea Oktoba 10 saa moja jioni, ambapo mwanafunzi huyo alizama baada ya maji kumshinda nguvu.

Alisema kuwa kikosi cha waokoaji kilifika katika bwawa hilo akini ilishindikana kumuokoa mwanafunzi huyo kwa wakati kutokana na giza.

Hata hivyo, amesema waokoaji hao waliupata mwili wa marehemu asubuhi ya Oktoba 11 kuupeleka hospitali ya ajili ya uchunguzi wa kidaktari.

Kufuatia tukio hilo, Kamanda Zelote amewataka wanafunzi na wananchi wanaoishi jirani na bwawa hilo kuwa makini wanapochota maji, kuogelea au kufua katika anao hilo.
Screenshot_20211012-183326_Instagram.jpg
 
Katibu wa wizara ya Mifugo na uvuvi, Rashid Tamatama, amesema kuwa ulaji wa nyama na unywaji wa maziwa nchini bado uko chini na imekuwa changamoto kubwa kwa mujibu wa Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP).

Amesema mujibu wa takwimu za shirika hilo, mtu hutakiwa kula nyama kilogramu 50 kwa mwaka na maziwa lita 200, lakini Watanzania hula kilogramu 15 za nyama na lita 50 za maziwa kwa mwaka.

Akizungumza leo Oktoba 12,2021 kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya chakula duniani ambapo Kitaifa yatafanyika Mkoa wa Kilimanjaro, Tamatama amesema kuna haja ya serikali kwa kushirikiana na wadau wa sekta hiyo kuhakikisha kiwango cha ulaji wa nyama na maziwa kinafikia viwango vya kimataifa.

Amesema pia ulaji wa samaki na mayai bado kiwango kiko chini huku uzalishaji ukiwa juu, akisema kauli mbiu ya maadhimisho hayo ya ‘Zingatia uzalishaji na mazingira endelevu kwa lishe na maisha bora’ imelenga kuhamasiaha ulaji huo.

"Ulaji wa vyakula vya protini na wanga bado uko chini, licha ya kuwepo kwa mikoa hapa nchini ambayo inazalisha kwa wingi," amesema Tamatama.
Screenshot_20211012-183938_Instagram.jpg
 
“Tunakwenda kununua mitambo 60 ya huduma ya mionzi, si halmashauri zote zitapata, tumeangalia hospitali za halmashauri ambazo hazina na kila mashine tunatarajia itagharimu Sh420 milioni kwahiyo tutatumia Sh25.2 bilioni kwa ajili ya kuweka mashine hizo,” - Waziri Ummy Mwalimu
Screenshot_20211012-184124_Instagram.jpg
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Ummy Mwalimu amewapiga marufuku wakuu wa mikoa na wakurugenzi kutoka nje ya mkoa bila kibali cha Rais, Makamu wa Rais au Waziri Mkuu.

Ummy amesema hayo leo Jumanne Oktoba 12, 2021 katika mkutano wa waandishi wa habari akifafanua Tamisemi itakavyotumia mkopo wa IMF kutekeleza miradi mbalimbali ambayo utekelezaji wake unawahusu viongozi na watendaji hao wa mikoa nchini.

Amesema kuwa wakuu wa mikoa na wakurugenzi wanatakiwa kuepuka safari zisizo za lazima za kutoka nje ya mkoa isipokuwa kwa kibali cha viongozi hao.

“Lakini kwa sababu tunajambo hili kubwa, ninawaelekeza viongozi wote wa Serikali ndani ya Tamisemi, ngazi ya mikoa, wilaya na halmashauri kuepuka safari zisizo za lazima zinazohusu kutoka nje ya mkoa wako isipokuwa kwa kibali cha viongozi wakuu wa nchi."

“Kwa hiyo mkuu wa mkoa ukitaka kutoka ndani ya Mkoa wako kipindi hiki lazima upate kibali cha rais, kibali cha Makamu wa Rais au Waziri Mkuu.
Screenshot_20211012-184221_Instagram.jpg
 
Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amemwomba Spika wa Bunge, Job Ndugai kubadili uamuzi wake wa kutogombea tena ubunge wa Kongwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Bashe ametoa kauli hiyo jana jioni Oktoba 11, 2021 wakati akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa korosho wa wilaya za Mpwapwa, Kongwa na Manyoni.
Bashe amesema mipango mizuri ambayo imeanzishwa na Ndugai haipaswi kubezwa na kuwa akija mwingine huenda asiendeleze kwani kila mmoja ana mipango yake.

"Nilisoma kwenye mitandao kuwa ukitaka kustaafu na Rais John Magufuli, lakini Mungu ana mipango na makusudi yake, leo tuko na Samia Suluhu Hassan ambaye tunakwenda naye hadi 2030, naomba ufikiri namna ya kubadili uamuzi wako," amesema Bashe.
Screenshot_20211012-185249_Instagram.jpg
 
Neymar Jr anasema kombe la dunia nchini Qatar 2022 litakuwa la mwisho kwake, hajioni tena kuwa na nguvu baada ya hapo

Neymar alianza kucheza World Cup ya 2014 nchini Brazil

Wakati Messi na Ronaldo walianza 2006 ila wanaenda kumaliza nae mwakani

Neymar ameshindwa kuwa Mshindani wao na sasa anaungana nao
Screenshot_20211012-185723_Instagram.jpg
 
Timu ya taifa ya Ufaransa inapigiwa chapuo kuweza kutetea kombe la dunia baada ya kutwaa 2018 nchini Urusi

Kwa talents walizonazo na ubora tunaoshuhudia basi hilo halina shaka, ikichagizwa zaidi na wachezaji wao kuwa kwenye PRIME football age
Screenshot_20211012-185850_Instagram.jpg
 
“Tulituma malalamiko yetu kwa mchezo wa ugenini na mchezo wa hapa nyumbani ambapo waligomea majibu ya vipimo na kulazimisha kutumia wachezaji kwa hivyo Bodi ya nidhamu ya CAF bado tunaikumbusha kutoa maamuzi ya mchezo uliofanyika hapa Nigeria. Sisi kama Rivers tungependa mpira wetu wa Afrika usonge mbele na kuondokana na vitendo vya ovyo.

- Charles Mayuku, Afisa Habari Rivers United.
Screenshot_20211012-190121_Instagram.jpg
 
“Ni mapema sana kulaumiwa ukizingatia tunapata bao moja ni la ushindi hatujaruhusu kufungwa na katika bao hilo moja kunakuwa na nafasi nyingi zinazotengenezwa hivyo hii ni moja ya sifa kwetu kwamba tuna uwezo mkubwa tukitulia.

- Fiston Mayele.
Screenshot_20211012-190308_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom