Makapuku Forum

Makapuku Forum

Bondia Mtanzania Dullah Mbabe leo amepoteza pambano kwa kupigwa kwa point na Bondia Tshimanga Katompa kutokea Congo DRC katika pambano la round 10 lililochezwa PTA jijini Dar es Salaam.
Screenshot_20211010-043001_Instagram.jpg
Screenshot_20211010-043121_Instagram.jpg
Screenshot_20211010-043147_Instagram.jpg
Screenshot_20211010-043209_Instagram.jpg
Screenshot_20211010-043227_Instagram.jpg
 
Madereva 250 wa malori yaliyopaki magogo kutoka Congo na kukwama Zambia kwa zaidi ya miezi minne, wameruhusiwa kuvuka mpaka na kuingia Na Kuingia Tanzania baada ya Serikali kusikia kilio chao na kupata suluhu ya sintofahamu iliyokuwa inawakabili .

Mkuu Wa Wilaya ya Momba Faki Lulandala amefika katika mpaka wa Tanzania na Zambia na kukutana na madereva 52 wa kwanza kuingia Tanzania na kusema awali zoezi la kutatua mgogoro huo lilishindikana katika ngazi ya Wilaya na Mkoa na kumlazimu Raisi Wa Tanzania Samia Suluhu Hasani kuingilia kati Madereva hao sasa wanarejea katika Familia zao .

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Malori (CHAWAMATA) amesema tayari wameanza kuwapokea madereva 52 na wengine wanasubiriwa.

Madereva hao wameshukuru na kuiomba Serikali kuwasaidia waweze kupata stahiki zao kwani wamekaa nje ya Nchi kwa kipindi kirefu huku wakidaiwa fedha ikiwemo za kulipia eneo la kupaki magari hayo na wengine ni wagonjwa.
Screenshot_20211010-043712_Instagram.jpg
 
Baada ya tukio la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Kugoma kuzindua Barabara ya Liwale ambayo kwenye mkataba wa Barabara hio ilipaswa kuwa na taa, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Godfrey Kasekenya kwenye Mkutano wa Ndani na Waziri Mkuu amesema tayari mchakato wa kuweka taa hizo umeanza na amemuomba Waziri Mkuu taa zikifungwa akafungue.

"Baada ya tukio la pale Barabarani tumeanza kufanyia kazi, tumeona taa zinazohitajika ni taa 20 na taa hizo zitatoka nje tumeongea na wenzetu wa TANROADS Kufikia mwisho wa mwezi wa 11 tutakuwa tumeweka taa Barabara ya laki inapoanzia na kuhakikisha katikati ya Mji huu taa zote zinawaka ili kwakweli Waziri Mkuu uje kutufungulia hii Barabara"

Itakumbukwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa October 07,2021 akiwa katika ziara yake Mkoani Lindi aligoma kuzindua barabara ya Liwale Mjini ya KM 1.2 kwa sababu haijawekwa taa za barabarani “Mkataba ni kujenga barabara za lami zenye taa, leo mnaniambia nizindue barabara haina taa?
Screenshot_20211010-043834_Instagram.jpg
 
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Konde, Abdallah Said Hamad amemtangaza Mgombea wa ACT-Wazalendo, Mohamed Said Issa kuwa mshindi wa kiti cha Ubunge kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo uliofanyika leo tarehe 09 Oktoba, 2021, Mgombea huyo amepata kura 2391 kati ya kura halali 3338 zilizopigwa.

Uchaguzi huo ulikuwa na jumla ya wagombea wanne ambapo mgombea Hamad Khamis Mbarouk wa AAFP alipata kura 55, Mbarouk Amour wa CCM amepata kura 794 na Salama Khamis Omar wa CUF amepata kura 98.

Wapiga kura waliojiandikisha ni 6636, waliopiga kura ni 3408, kura halali ni 3338 na kura zilizoharibika ni 70.
Screenshot_20211010-043959_Instagram.jpg
 
Hatimaye Staa wa soka Lionel Messi ameyaongea ya moyoni jinsi alivyolazimika kuondoka Barcelona katika mazingira ya kulazimishwa na ambayo hakuyatarajia ambapo kwenye Interview na CNN, Messi amesema "nilikua nimerudi Hispania baada ya michuano ya Copa America mwezi July, nilichokua nakiwaza ni kwamba mkataba huo uliwekwa pembeni sababu saini yangu tu ndio ilikua inasubiriwa kumbe sivyo"

"Nilipowasili Barcelona niliambiwa hilo la kusaini mkataba mpya haliwezekani tena hivyo nitafute Club nyingine kwasababu Barca haiwezi kuniongezea mkataba, hilo lilinipa wakati mgumu sana nikaanza kufikiria mengi ikiwemo kubadilisha mfumo wa familia yangu kuacha makazi na kwenda kuanza sifuri kwenye sehemu nyingine”

“Kujiunga na PSG sikukosea, kilichonisaidia mimi kutulia baada ya kujiunga na PSG ni sura ninazozifahamu hapo na kuzingatia kwamba kuna Wachezaji wengi wanaoongea lugha ya Kihispania kama 'Ney' 'Lea' (Paredes), 'Fideo' (Di Maria)" ——— Messi ameiambia
Screenshot_20211010-044050_Instagram.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu amesema amepokea malalamiko ya baadhi ya Wananchi kuhusu changamoto zinazojitokeza wakati wa ukusanyaji wa ada za maegesho ya magari kwa kutumia mfumo wa kielektroniki unaosimamiwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA).

Pamoja na dhamira nzuri waliyonayo TARURA katika kuboresha mfumo wa ukusanyaji wa mapato yatokanayo na maegesho ya vyombo vya moto, matumizi ya hifadhi za Barabara na tozo za adhabu zitokanazo na ukiukwaji wa matumizi ya hifadhi za Barabara na ufafanuzi uliotolewa kufuatia malalamiko hayo ya Wananchi, Waziri Ummy Mwalimu amesitisha kwa muda matumizi ya mfumo huo wa ukusanyaji wa ada za maegesho kuanzia leo hii October 09,2021.

Waziri Ummy amemuagiza pia Katibu Mkuu TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe kukutana na Timu ya Wataalamu wa TARURA kujadili namna ya kutatua changamoto zilizojitokeza, wakati hayo yakiendelea ukusanyaji wa ada za maegesho ya magari zitaendelea kukusanywa kwa kutumia mfumo wa awali (manual system) ambao ulikuwa unatumika kukusanyia ada hiyo kabla ya kuanza kutumia mfumo wa Kielekroniki.
Screenshot_20211010-044823_Instagram.jpg
 
Wakulima wa Korosho katika Kata ya Nachunyu Halmashauri ya Mtama Mkoani Lindi leo October 09,2021 wamegoma kuuza korosho zao Tani 1,895 na kilo 579 kwenye mnada uliofanyika ghala la chama cha ushirika Natam Amcos kutokana na kutoridhika na bei ndogo ya Wanunuzi ambapo bei ya juu ni Tsh. 2275 na ya chini Tsh 2010.

Mnada wa kwanza wa korosho kwa msimu wa 2021/2022 ulifanyika Jana katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Newala Mkoani Mtwara chini ya Chama Kikuu cha Ushirika cha TANECU ambapo Wakulima walikubali kuuza korosho zao kwa bei ya juu ya Tsh. 2445 huku bei ya chini ikiwa ni Tsh. 2231 ambapo Kampuni zilizojitokeza kununua ni 15 na jumla ya tani 1486 ziliuzwa.
Screenshot_20211010-045707_Instagram.jpg
 
Mchezaji wa zamani wa Simba SC Raia wa Uganda Emmanuel Okwi (28) amesaini kuichezea Club ya Kiyovu SC ya Rwanda kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Okwi anajiunga na Kiyovu SC ikiwa ni miaka miwili imepita toka aondoke Simba SC 2019 baada ya AFCON na kujiunga na Al Ittihad Alexandria ya Misri.
Screenshot_20211010-050514_Instagram.jpg
 
Juma Hamad Saleh (19) mkazi wa Msuka Konde amekamatwa akidaiwa kuwa na bangi katika kituo cha kupigia kura Jimbo la Konde.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Juma Sadi Khamis amesema tukio hilo limetokea leo Jumamosi Oktoba 9, 2021 katika kituo cha kupigia kura cha Msuka Magharibi.

Kamanda Khamisi amesema kijana huyo alitiliwa mashaka na alipopekuliwa akakutwa na misokoto minne ya bangi.
Screenshot_20211010-052037_Instagram.jpg
 
SIMBA YATANGULIZA WATATU BOTWSANA
.
Katika kuhakikisha inafanya vyema Botswana dhidi ya Jwaneng Galaxy Simba imeamua kutanguliza watu wawili kuweka mambo sawa kabla ya timu yao kufuata wiki ijayo.
.
Taarifa kutoka ndani ya Simba zinasema kuwa, Mratibu Ali Abbas Seleman na mpishi wao Mkuu Samweli Mtundu ‘Sam’ na Mtaalamu wa tathmini Culvin Mavhunga ndio watakaotangulizwa kabla ya timu kuwafuata.
.
Habari za ndani kutoka Simba ni kwamba wawili hao wataondoka kwenda kuweka mambo sawa
Screenshot_20211010-052737_Instagram.jpg
 
[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

ALI KIBA, DARASA LINGINE LA MZIKI LITAISHI MILELE

Kwenye soko la mziki duniani kuna vitu viwili vinaamua aina ipi ya mziki ufanyike! Kuna Trend per Music na Music per trend! Hivi hupelekea muda mwingine kupoteza maana ya muziki

MUSIC PER TREND! Ni kupelekwa na upepo wa aina gani inasumbua sokoni! Mfano Afrika hivi sasa Amapiano imekamata sana, lakini huu ni mziki wa Afrika Kusini, huwezi kufanya zaidi yao na ukiufanya ni kuuza zaidi flavour yao

Wasanii wengi Tanzania wametoa ngoma za Amapiano, lakini hizi ngoma haziishi sana, ngoma hizi pia zinapoteza utambulisho wa mziki wa Tanzania kwenye soko la Afrika, haswa kipindi hiki watu wanapambana mziki wetu utoboe

Wakati Wasanii wengi wakubwa wamekubali kuishi utamaduni wa Wasauzi kwenye nchi huru Tanzania, ni Ali Kiba anakuja kutupa album yake yenye mziki wake bila Amapiano hata moja! Hakuna hata wimbo mmoja ulisukumwa na upepo wa sasa

Huyu ndie Ali Kiba ninaemfahamu, anaishi kwenye ile misingi yake, ndio maana ngoma zake zinaishi sana kwakuwa hazina mlengo wa upepo, unaweza kusikiliza kuanzia Mapenzi Yanarun dunia hadi Oya Oya! Bado ukamuona Kiba ni yule yule

Anaendelea kuulinda mziki wa Tanzania dhidi ya upepo mkali wa Wasauzi, wanaopambana kuupenyeza mziki wao Afrika! Tujiulize SINGELI ni mziki wetu ila umepata mileage kubwa nje? Jibu ni HAPANA, lakini wenzetu wametuteka

Kingine ni TREND PER MUSIC! Ni darasa lingine Kiba anaendelea kuwapa vijana chipukizi wanaotaka kufanikiwa zaidi, tuulizane KIBA ametoa album yake umeona kuna Kiki kazifanya? Umeona kuna skendo kazifanya?

Kiba mziki wake unaishi sana kwakuwa anaandika kutaka uishi na atawale mioyo ya watu, ukifanya kiki utaandika ili utawale vichwa vya watu, kumbuka kichwa kina mengi kinasahau, ila moyo hausahau kamwe

Screenshot_20211010-053235_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom