Makapuku Forum

Makapuku Forum

Dah [emoji2356][emoji2356] kuna kaukweli babe kama ile ya juzi kati ilee najua umeshakumbuka
Screenshot_20211008-184730_Instagram%20Lite.jpg
 
“Bila shaka uamuzi wa kufanya mapokezi haya Zanzibar ni kielelezo cha juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na viongozi wa taifa hili katika kuendeleza na kulinda fikra, mawazo na falsafa za waasisi wa taifa letu katika kuulinda na kuudumisha Muungano wetu"

"Mapokezi ya ndege hizi mbili aina ya Airbus ni hatua muhimu katika juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuliimarisha Shirika la ndege la Tanzania Air Tanzania ambalo lilianzishwa mwaka 1977 "

"Nahimiza taasisi zetu zilizo katika viwanja vya ndege kufanya kazi kwa ushirikiano na ufanisi unaotakiwa. Naamini kwamba tukiwa na ndege zenye kufanya safari za moja kwa moja katika viwanja vyetu, Sekta ya Utalii na Uchumi zitaimarika kwa kasi” asema Rais wa Zanzibar Dr. Hussein Mwinyi leo wakati wa kupokea Ndege mbili mpya za Air Tanzania.
Screenshot_20211008-193313_Instagram.jpg
 
"Ndege zina uwezo wa kubeba Abiria 132 na Abiria 12 ni wa daraja la biashara, Ndege zina uwezo wa kuruka saa 6 bila kutua ikiwa na Abiria pamoja na mizigo"

"Shirika la ndege Tanzania (ATCL) linafanya safari katika vituo 13, pia shirika lipo katika hatua za mwisho za kuanzisha safari za muunganiko (connectivity) za Dodoma-Mwanza na Zanzibar-Pemba"

"Air Tanzania imefanikiwa kufungua vituo nane nje ya nchi, Bujumbura (Burundi), Entebbe (Uganda), Guangzhou (China), Ahaya (Comoro), Harare (Zimbabwe), Lusaka (Zambia), Johannesburg (Afrika Kusini) na Mumbai (India) "

"Air Tanzania inatarajia kuanzisha safari za kimataifa kwa vituo vipya ikiwemo Lubumbashi (Congo), Nairobi (Kenya) na Ndola (Zambia)” asema Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Ladislaus Matindi mbele ya Rais wa Zanzibar Dr. Mwinyi leo Zanzibar wakati wa mapokezi ya Ndege hizo mbili.
Screenshot_20211008-193437_Instagram.jpg
 
Mnada wa kwanza wa korosho kwa msimu wa 2021/2022 umefanyika leo katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Newala Mkoani Mtwara chini ya Chama Kikuu cha Ushirika cha TANECU ambapo Wakulima wamekubali kuuza korosho zao kwa bei ya juu ya Tsh. 2445 huku bei ya chini ikiwa ni Tsh. 2231 ambapo Kampuni zilizojitokeza kununua ni 15 na jumla ya tani 1486 zimeuzwa.
Screenshot_20211008-193536_Instagram.jpg
 
Mchezaji wa Manchester United Cristiano Ronaldo ameshinda Tuzo ya Mchezaji bora wa mwezi wa Ligi Kuu England huku Kocha wa Arsenal Mikel Arteta akishinda tuzo ya Kocha bora wa mwezi September, umeonaje? wanastahili? nani mwingine umemkubali kwenye huo mwezi
Screenshot_20211008-193722_Instagram.jpg
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale aitwae Omary Chingwile ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Liwale ambapo Waziri Mkuu ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kufanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo.

“Hatuwezi kufanya mchezo na fedha ya Serikali, tunahitaji kila mradi uende vizuri, fedha iliyoletwa lazima itumike kama ilivyokusudiwa" - Waziri Mkuu amemsimamisha kazi Afisa huyo October 7, 2021 wakati akizungumza na Madiwani, Watumishi na Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Lindi.
Screenshot_20211008-193852_Instagram.jpg
 
Serikali ya Uingereza imetangaza rasmi kuiondoa Tanzania katika orodha ya Nchi ilizoziwekea vikwazo vya usafiri kutokana na janga la Covid 19 na sasa kuanzia October 10, 2021 Msafiri kutoka Tanzania hatokaa karantini akiingia Uingereza lakini sharti awe amepata moja ya chanjo nne ambazo Uingereza inazitambua ambazo ni Pfizer-BioNTech, Oxford- AstraZeneca, Moderna na Janssen na kwa zinazohitaji kuchomwa mara mbili Mtanzania atatakiwa awe amechoma mara zote mbili.

Tanzania sasa inaingia kwenye orodha ya Nchi nyingine 47 ambazo zimeondolewa kwenye red list ‘list nyekundu’ ya Uingereza ambapo sasa ni Nchi 7 pekee zimebaki kwenye red list ya kutoingia Uingereza ambazo ni Peru, Ecuador, Colombia, Panama, Haiti, Venezuela na Dominican Republic.
Screenshot_20211008-194008_Instagram.jpg
 
Miss Netherlands 2021, Dilay Willemstein ambaye alipaswa kwenda Nchini Puerto Rico December mwaka huu kushiriki shindano la Miss World 2021 amegoma kwenda kwenye Fainali hizo kwasababu moja ya vigezo ni lazima Mshiriki awe amechanjwa chanjo ya corona kitu ambacho hayupo tayari kukifanya kwa sasa.

Dilay mwenye umri wa miaka
21 amesema hakujua kuwa ili uendele kwenye Fainali za Miss World ni lazima uwe umechanja lakini baada ya kuambiwa ameona ni bora asiende hivyo aliyeshika nafasi ya pili kwenye mashindano ndiye atayekwenda Miss Word.

Kupitia Instagram akaunti yake Dilay ambaye licha ya kuwa Mwanamitindo pia nia Dancer na Mwimbaji amesema hayupo tayari kuchanjwa kwa sasa na kusema hata kama hiyo ilikuwa ni sehemu ya kutimiza ndoto zake hajutii uamuzi wake kwa kuwa afya yake ni bora kuliko chochote.
Screenshot_20211008-194138_Instagram.jpg
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Italia, Marina Sereni yaliyofanyika Roma, Italia.

Mazungumzo hayo yamefanyika kando ya Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Afrika na Italia ( Encouters with Africa 2021) ambapo wamezungumzia masuala ya kuendelea kuimarisha biashara, uwekezaji pamoja na Utalii miongoni mwa masuala machache kati ya mengi waliyoyazungumzia.
Screenshot_20211008-194317_Instagram.jpg
 
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro amesema tukio la polisi saba waliovuka mpaka na kuingia nchini Malawi lilikuwa la aibu na kufichua kuwa mali ya magendo waliyokuwa wakiyafukuza thamani yake ni Sh30,000.

Mbali na sakata hilo, Sirro amebainisha kuwa kuna changamoto kubwa ya upelelezi inayosababisha mlundikano wa mahabusu na kuwaagiza wanaosimamia madawati ya upelelezi kuhakikisha suala hilo linamalizika.
Screenshot_20211008-194420_Instagram.jpg
 
Baada ya milenia kadhaa kupita tangu kugundulika kwa ugonjwa wa Malaria, kwa mara ya kwanza Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa idhini kwa chanjo ugonjwa huo kusambazwa Afrika kwa ajili ya kuwalinda

Hatua hiyo inatajwa kuwa ni mojawapo ya mafanikio makubwa katika tasnia ya tiba na sasa watoto barani Afrika watapewa chanjo hiyo baada ya majaribio ya mianga mingi.

Ugonjwa wa malaria unaliathiri zaidi bara la Afrika ambapo watoto 260,000 wamefariki kwa ugonjwa huo mwaka 2019.
Screenshot_20211008-194554_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom