Makapuku Forum

Kiukweli Kijana arudi nyumbani sasa wapumzike, wamehama nae sana

Imagine walikubali kwenda nae mpaka China kipindi flani kulikuwa na tetesi

Wakakubali kuhama nae mpaka City ila Viongozi wakaona busara sasa Mashabiki wake warejee nyumbani

Wanarejea nyumbani ila wamechoka sana Mashabiki wa United
 
Pole Mwanangu, najua umechoka sana! Tusamehe wazazi wako, tulikuacha ukatafute maisha yako

Rudi nyumbani sasa wadogo zako wapo wanakusubiri, wameniripotia sana kuna Mtoto wa mtaa wa pili anaitwa Rudiger, amewasumbua sana
 
Taarifa zinadai kuwa nyota wenzake wa zamani walitumia muda mwingi kupitia WhatsApp kumshawishi Ronaldo arejee Old Trafford

Ndio maana magwiji wengi wamempost na kucomment sana
 
"Kama alikuwa anafikiria kuondoka Juventus, bila shaka anajua tupo hapa" Ole Gunnar, kuhusu Ronaldo

Yani dakika chache tu baada ya kuhusishwa tayari United wamegonga vichwa vya habari

Huwaambii kitu kwa Mtoto wao
 
Farhan Jr

Tayari Lionel Messi ameelekea PSG inayomilikiwa na Waarabu wa Qatar, chini ya Sheikh Tamim Bin Ahmad El Than ambaye pia ni Amir wa nchi ya Qatar

Muda wowote kuanzia sasa Cristiano Ronaldo atatambulishwa kama Mchezaji mpya wa Manchester City, inayomilikiwa na Tajiri wa Kiarabu Sheikh Mansour Bin Zayed El Naian wa Falme za Kiarabu

Maana yangu nini? Kuna siku Sir Alex Ferguson aliwahi kusema " One thing about football is not about football" akimaanisha kitu kimoja kuhusu mpira huwa hakihusu mpira

Kuna kitu kinaitwa ARAB SUPREMACY! Kule Mashariki ya kati kuna vita kubwa sana! Kila taifa la Kiarabu linataka utawala eneo hilo na Football ni sehemu moja wapo, wamehamishia ushindani hapo

Unaweza kuona ni suala la kimpira tu lakini ni zaidi ya mpira, on repeat! One thing about football is not about football
 
OFFICIAL: Klabu ya RS Berkane ya Morocco imetangaza rasmi kukamilisha usajili wa winga raia wa Congo, Tuisila Kisinda mwenye umri miaka (21) kuwa mchezaji wao mpya akisaini kandarasi ya miaka mitatu kutoka Yanga SC.

Ila Tusila kweli una miaka 21
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…