Makapuku Forum

Rais Samia Suluhu Hassan asubuhi hii amefanya ziara ya kushtukiza Katika Soko la Kisutu na kusikiliza kero za Wafanyabiashara.
 
Mbunge wa Momba Condester Michael Sichalwe ametolewa ndani ya ukumbi wa Bunge ili akabadilishe mavazi yake baada ya Mbunge wa Nyangw'ale Hussein Nassor Amar kuomba muongozo wa Spika kuwa kuna baadhi ya Wabunge wamevaa mavazi yasiyo na maadili.

Spika Ndugai alimtaka Mbunge Hussein Nassor Amar kumtaja mmoja ambaye amemuona ndipo alipomtaja Mbunge wa Momba Condester Michael Sichalwe ambapo Spika alimtaka atoke ndani ya ukumbi wa Bunge ili akabadilishe mavazi yake.

Huyu mbunge alieomba muongozo kwa spika sio bwana smart kweli
 
Mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa anayecheza Crystal Palace ya England Mamadou Sakho leo akiwa na Mke wake Majda Sakho wamekaribishwa Bungeni Dodoma.

Jana Mamadou Sakho alitangazwa na Serikali kuwa Balozi wa hiari wa utalii Tanzania na alialikwa IKULU Zanzibar na Rais Dr. Hussein Mwinyi ambako walizungumza mengi kuhusu kukuza vipaji vya soka.
 
Rais Samia Suluhu Hassan asubuhi hii amefanya ziara ya kushtukiza Katika Soko la Kariakoo na kusikiliza kero za Wafanyabiashara.

“Nimeona nije nione eneo ambalo Watanzania wengi wanafanya biashara, nimesikia baadhi ya malalamiko nikaona nije nione mlipo na mnavyofanya biashara zenu, nimefanya mahojiano na wachache sokoni na yamenipa sura ya soko linavyoendeshwa”———Rais Samia Kariakoo
 
Mbona kavaa kiheshima tyuuh jaman lol.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…