Makapuku Forum

Makapuku Forum

“Naagiza hili na lifanyike haraka, Mawaziri wanaohusika mkatatue ile foleni mipakani (Taveta Holili, Namanga) magari yapite, kama ni vyeti vya Corona Mawaziri wa Afya wakae wajue wanavyoweza kufanya, kama Mtu amepewa cheti Tanzania basi aingie Kenya na Mkenya aingie Tanzania”———Rais Kenyatta mbele ya Rais Samia kwenye Kongamano la Wafanyabiashara wa Tanzania na Kenya nchini Kenya leo

“Mawaziri wa Afya mkakae, Kama Mtu amepimwa Corona Tanzania na amepewa cheti basi hiko cheti kiwe sawa aingie Kenya na Kama Mtu amepimwa Corona Kenya na kupewa cheti basi hiko cheti kiwe sawa na aingie Tanzania ndio Watu wafanye biashara zao”———Rais Kenyatta
20210505_194724.jpg
 
“Tuna nafasi na nia ya kuhakikisha kwamba tukifanya pamoja tutainua uchumi wa Kenya na Tanzania, tukishirikiana ushindi utakuwa wa Wananchi wa Nchi zetu mbili, Wananchi wetu wakijiona ni Ndugu ambao wanashirikiana badala ya kushindana,wote tutashinda”———Rais Kenyatta mbele ya Rais Samia kwenye Kongamano la Wafanyabiashara wa Kenya na Tanzania nchini Kenya leo

“Jana Rais Samia ulisema Kenya ni Taifa la tano Duniani kuwekeza Tanzania na tukasema Kampuni za Tanzania ambazo zimewekeza hapa Kenya ni karibu 30, Sisi tungependa Wawekezaji wengi zaidi Watanzania wakuje waje kuwekeza Kenya”——-KENYATTA

“Kenya na Tanzania hatuna lolote la kushindana, tushirikiane, tukijiona kama Nchi ambazo zinashindana hatutaweza kupata Wawekezaji wakubwa wa kuja kuweka viwanda vyao Afrika Mashariki, Vijana wetu watakosa ajira na sisi tutanunua bidhaa nje”———KENYATTA

“Wawekezaji Watanzania fanyeni kazi Kenya kama mnavyofanya Tanzania ilimradi tu mufuate sheria na kanuni ambazo zimekwa na zile ambazo Wafanyabiashara wa Kenya pia lazima wazifuate lakini karibuni sana na tutahakikisha tumerahisisha njia za nyinyi kufanya biashara”———KENYATTA
20210505_194824.jpg
 
“Haya mambo ya Mawaziri kusubiri hadi mkutano uitwe Mtu avae suti yake, sijui kuwe na ajenda mara tuite Wakili, tunataka Mawaziri (Wakenya na Tanzania) tokeni Maofisini mtembeleane ili kuwasaidia Wananchi wetu (Wakenya na Tanzania”———Kenyatta mbele ya Rais Samia nchini Kenya

“Mtu (Waziri) asione amepata Ofisi anakaa anaogopa hataki kuongea na wenzake wa Nchi nyingine, eti anasubiri kuambiwa, kama unasubiri kuambiwa basi hufai kuwa Waziri, Waziri ni Mtu wa kuchukua hatua, umepewa kazi kubwa kwasababu tunaamini una uwezo, itekeleze”———KENYATTA
20210505_194955.jpg
 
“Wafanyabiashara nendeni mkashirikiane na sio kushindana, mna bahati kwamba katika Nchi zetu hizi mbili (Tanzania na Kenya), upande mmoja kuna Uhuru wa kufanya biashara na upande mwingine kuna Suluhu ya kuondosha vikwazo vya biashara, hapo mshindwe nyinyi tu”———Rais Samia mbele ya Rais Kenyatta kwenye Kongamano la Wafanyabiashara wa Kenya na Tanzania nchini Kenya

“Tanzania ipo tayari kuwapokea Wawekezaji wengi zaidi kutoka Kenya na kushirikiana nao, kwa sasa Tanzania tunaendelea kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na kuondoa vikwazo na kodi zinazosumbua Wafanyabiashara”———Rais Samia
20210505_195119.jpg
 
Queen wa Pop ambae pia ni Mshindi wa Tuzo za Grammy mara tano Janet Jackson ameamua kuzipiga mnada nguo zake zaidi ya elfu moja ikiwa ni sehemu ya kusherehekea miaka 55 ya kuzaliwa kwake ambapo mnada huo unafanyika Jijini New York Marekani.

Moja ya nguo zitakazouzwa ni lile sweta alilolivaa kwenye video ya 'scream' na ile kofia ya baseball aliyoivaa kwenye video ya “Rhythm Nation” ambapo pesa inayotarajiwa kukusanywa inafika Dola za kimarekani milioni 2.

Imewekwa wazi kwamba sehemu ya pesa itayopatikana itapelekwa kusaidia Watoto kote duniani kupitia Taasisi ya Compassion International ambayo hufanya kazi na Makanisa mbalimbali kusaidia Watoto kiroho, kiuchumi, kijamii na kuwakwamua kutoka kwenye umasikini.
20210505_195227.jpg
 
Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) imesitisha safari zake za ndege kati ya Dar es salaam na Mumbai (India) kuanzia May 04,2021 hadi itakapotolewa taarifa nyingine ya kurudisha safari hizo hii ni kutokana na kuwepo kwa ongezeko la maambukizi ya Corona nchini India

“Abiria wote wenye tiketi za ATCL katika safari za DSM- Mumbai wanashauriwa kuwasiliana na Ofisi za ATCL au Mawakala wao kwa taratibu za kubadilisha tiketi ili zitumike pindi safari zitakaporejea tena bila gharama yoyote, tunaomba radhi kwa usumbufu”———ATCL
20210505_195345.jpg
 
Mtu mmoja amefariki dunia na wengine wanne kujeruhiwa katika machimbo ya Moivaro yaliyopo wilaya ya Arusha baada ya kifusi kuanguka na kuwafukia wakati wakichimmba mchanga.

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Kenan Kihongosi ameagiza kufungwa kwa machimbo hayo baada ya kufunguliwa kinyemela, mwaka jana machimbo hayo yalifungwa baada yakuua Watu watatu.

Itakumbukwa juzi pia katika machimbo ya moramu katika eneo la Kisongo, Arusha walifariki Watu watatu na wengine watatu kujeruhiwa baada ya kuangukiwa na kifusi.
20210505_195450.jpg
20210505_195508.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu amewataka Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea kuchapa kazi kama awali na sio kukaa kusubiria uteuzi.

Waziri Ummy ameyasema hayo katika ziara yake Wilayani Chemba Mkoani Dodoma kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na Kamati ya Fedha pamoja na Menejimenti ya Halmashauri hiyo.

“Hali inayoendelea kwa Viongozi hawa haileti Afya, wengine hawafanyi kazi eti wanasubiria mkeka, hamuoni kuwa mnaonea wananchi kupata haki yao ya msingi ya kuhudumiwa?”——— Waziri Ummy

“Kipindi hiki mnatakiwa kuendelea kuchapa kazi kama kawaida Wananchi wanahitaji kuendelea kuhudumiwa, suala la mkeka unakuja lini hilo ni kuliachia Mamlaka, ninyi chapeni kazi na mumtangulize Mungu Mbele"———Ummy
20210505_195618.jpg
 
Shabiki wa Yanga Mwanariadha Mang'suli Hussein (45) wa Manispaa ya Kigoma ujiji aliyeamua kukimbia kwa miguu kutoka Kigoma kuanzia April 15 kuelekea Dar es Salaam kutazama Mechi ya Yanga vs Simba mwezi May, amewasili Morogoro usiku wa kuamkia leo lakini amesema anaumwa tumbo na kusema hiyo itamfanya achelewe kufika Dar es salaam.

Tayari ametumia siku 20 tangu aanze safari yake na tarehe ya kufika Dar es Salaam ameibadilisha kutokana na kusumbuliwa na tumbo kwa sasa matarajio yake ni kufika Dar es salaam May 07,2021.

"Niwaombe radhi Watanzania wavute subira kidogo ningekua nimeshaingia Dar es Salaam muda mrefu sasa kutokana na tumbo lilikua linanisumbua siku mbili tatu nikawa nameza dawa tu bila kupima, nimepima leo ikaonekana nina Typhoid kwahiyo kesho nitatumia dawa na Mungu akinijalia Ijumaa nitakua Dar es Salaam kesho nitapumzika, nitaanza safari Alhamisi na Ijumaa May 07,2021 nitakua Dar es Salaam"———Mang'suli
20210505_195810.jpg
 
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Idara ya Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka leo kwenye taarifa yake amevitakia kila la kheri Vyombo vya habari Tanzania kwenye kufanya kazi yake na kusisitiza viendelee kuzingatia weledi na kufichua ufisadi, ubadhirifu wa mali za umma, mapambano dhidi ya rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Shaka amesema Uhuru wa Habari ni sehemu ya maendeleo kwa Taifa ambapo Chama na Serikali inatambua na kuheshimu Waandishi wa Habari na Vyombo vya habari.
20210505_195928.jpg
20210505_195948.jpg
20210505_200003.jpg
 
Mlinda lango wa zamani wa Arsenal Jens Lehmann ameachishwa kazi katika bodi ya klabu ya Bundesliga Hertha Berlin baada ya kumtumia ujumbe wa ubaguzi wa rangi mchambuzi wa kandanda Dennis Aogo, kupitia mtandao wa WhatsApp.
20210505_200410.jpg
 
Baraka mara dufu.

Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 25 raia wa Mali amejifungua watoto tisa katika hali ambayo sio ya kawaida.
-
Halima Cisse, 25, alijifungua watoto wa kike watano na wavulana wanne katika hospitali ya Morocco siku ya Jumanne ambako alikuwa amelazwa, Waziri wa Mali Fanta Siby alisema katika taarifa. Alijifungua kupitia njia ya upasuaji.
-
Kulingana na baba ya watoto hao, Adjudant Kader Arby amethibitisha kuwa watoto wake na mkewe wako salama licha ya kuwa wako nchini Morocco na amekuwa akiwasiliana na mke wake kwa njia ya video mara kwa mara.
-
Familia hii tayari ilikuwa na kifungua mimba msichana.
-
Akizungumza na mwanahabari wa BBC Cheick Bandaogo, Kader Arby amesema hana wasiwasi kuhusiana na watoto hao na anaamini kuwa Mungu ana sababu zake.

-
Amekiri kupokea simu nyingi kutoka kwa watu mbalimbali hata rais wa taifa lake Mali lakini hakueleza kwa kina walichozungumza baina yao.

-
Dkt Siby alisema watoto hao na mama yao “wanaendelea vyema”. Wanatarajiwa kurejea nyumbani wiki chache zijazo.
20210505_200717.jpg
 
"Nilipoanza shule ya msingi nchini Uingereza nilianza urafiki na mtu aliyenifunza kuvuta sigara,siku ya kwanza nilikohoa mno, ya pili vile vile , ila mwisho wa juma hilo nakumbuka nikiwa mraibu,"


Mchungaji Rahab Mwangi anaelezea jaribio lake la kwanza la kuvuta sigara .
Anakumbuka kuwa uraibu huo ulimpatia starehe tofauti lakini hakujua kwamba ungemsababishia madhara ya aina yake.


"Uchunguzi ulionyesha uwepo wa moshi wa sigara kwenye mapafu yangu, wakati ambapo nilikuwa nikivuta sigara 20 kwa siku.


Vilevile kutokana na uvutaji wa bangi madaktari waligundua kwamba nilikuwa na ugonjwa wa kifua kikuu (TB)"


Mwisho wa siku aliolewa na mchungaji
"Mwanzo wa ndoa mambo yalikuwa shwari, mume wangu ambaye pia ni Mchungaji alinipa ushauri na kunipatia nguvu ya kuishi bila utumiaji wowote wa madawa hayo .


Kama mke wa mchungaji pia mimi nilijitosa katika shughuli za kanisa , ila sikutamani kuwa mchungaji au kuwa na majukumu ya kuwa mtumishi kama mume wangu.

20210505_200915.jpg
 
''Wakati nilipozaliwa China, serikali ilikuwa imeweka sheria ya kila familia kuwa na mtoto mmoja.
Hivyo ilikuwa ni bahati mbaya sana kwa mtu kuwa na mtoto mwenye ulemavu wa ngozi -albino.”



Wazazi wa Xueli walimtelekeza katika bustani ya nyumba ya kulelea yatima akiwa ni mtoto.


Nchini China, kuzaliwa na ulemavu wa ngozi au albino ni sawa na kuwa na laana.


Lakini muonekano wake wa tofauti umemuwezesha kufanikiwa kuingia katika tasnia ya ulimbwende .

•“Kuna wengine kama mimi walitelekezwa , wengine walifungiwa na kama wakipelekwa shule, nywele zao zilipakwa rangi.''



Sasa ana miaka 16 na ameweza kuonekana kwenye jarida maarufu duniani la Vogue na katika kampeni nyingi za matangazo ya wabunifu wengi wakubwa.

20210505_201111.jpg
20210505_201126.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom