Makapuku Forum

Makapuku Forum

Madawa ya kulevya, Hususani 'Unga'...Huleta madhara makubwa katika Ubongo..Madawa huaribu Neurotransmitters....hizi ni kemikali zinazotolewa na ubongo ambazo husaidia katika kuhakikisha safari ya neva za seli kutoka moja kwenda nyingine inafanyika ipasavyo.

Kwenye Ubongo kuna Mabilioni ya Seli ambazo zimevunjika vunjika ambapo ili kuwasiliana pamoja ndipo hutumia hizo Kemikali ili kuungana....Baadhi ya kemikali Zinazofahamika sana ni Dopamine, Serotonin, acetylinelcholine, Noradrenaline etc.

Kazi ya 'dopamine' (Kukupa raha), noradrenaline (Kupambana) and 'serotonin' (Mood)....Sasa unapotumia madawa ya kulevya Unaaribu Neurotransmitters, hali inayoweza kupelekea kuongezeka au Kupungua kwa uzalishaji wake...ndio maana Kuna watu wakitumia Madawa tu, Unakuta anakuwa mgomvi tofauti na akiwa kawaida hajatumia

Mwingine akitumia unakuta anafanya mambo ya ajabu lakini kama hajatumia anakuwa na aibu alafu mpole hapo Madawa ya kulevya zinakuwa zimearibu hizo 'neurotransmitters'

Sasa kwa ndugu zetu wanaoutumia Unga hawa ndio balaa zaidi, Sehemu kubwa inayoathirika ni Kemikali hii ya Dopamine...ambayo kazi yake ni kukupa ile raha ambayo huwezi mwelezea mtu mfano kama Mwanaume anapopiga bao (Kufikia kilele) kuna raha fulani inadumu kama sekunde 10 hivii....Sasa unaambiwa Ukitumia 'Unga' ile raha ile, ile raha inaweza kudumu kwa takribani Mpaka dakika 30...hadi Saa nzima.

Sasa kama watu wanahonga hadi magari kwaajili ya kupata kale karaha tu, yani kale karaha ka Sekunde 5 unategemea nini kwa mtu ambae anapata raha hiyo Tripple zaidi... ndio maana unakuta mtu Hadi udenda unatoka..... Kitu kibaya ni wanapoanza, huanza mdogo mdogo, lakini baadae huzidisha zaidi kiasi kwamba Ubongo unakufa kabisa kuzalisha kemikali hizo...hivyo Bila Unga kwako inakuwa tabu...sababu mwili unakuwa unahitaji ili kuuweka Sawa...hapo ndipo tunasema mtu amekuwa adicted.

Na ndio maana mtu kuacha madawa anahitaji sana Counselling, lakini awe ameamua mwenyewe...alafu unaweza kuta mtu akawa Sober kwa miaka hata 10 lakini anaweza kurudia tena...ni vile unakuta kamiss ile raha.
Screenshot_20190228-162502.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom