Makapuku Forum

Makapuku Forum

..
c8a165b843678de9810eac0f2b482548.jpg
Mmmm

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mji wa Bodegraven, nchini Uholanzi waanza kuweka taa za barabarani kwenye njia za wapita kwa miguu maalumu kwa ajili ya watumiaji smartphone.

Hii itawasaidia kuepusha ajali kwa watu waliozoea kuangalia simu zao muda wote na kutokuwa makini wakati wanapotembea barabarani.
920e7209586b6df33eb8bb49882d5a88.jpg
 
Unajua kwamba tumbo lako ni moja kati ya viungo mwilini ambavyo hata vikiondolewa mwilini mwako bado utaweza kuendelea na maisha kama kawaida. Kazi kubwa nne za tumbo mwilini ni kukimeng'enya chakula, kutoa kemikali ambazo zinakilainisha chakula, kukifyonza na kukitoa.

Madaktari wanaweza wakaliondoa tumbo endapo ikatokea kansa au ajali. Mwaka 2012, mwanamke mmoja kutoka Uingereza aliondolewa tumbo lake lote baada ya kunywa pombe iliyokuwa na liquid nitrogen. Unaweza ukaondolewa tumbo lako kisha koromeo (oesophagus) lako likaunganishwa moja kwa moja kwenye utumbo mdogo na maisha yakaendelea bila matatizo.
57865f502c2b5b8c01bb9176ec9e0590.jpg
 
Kutokana na kuwa sayari ya kwanza na ambayo ipo karibu zaidi na Jua watu wengi wanaamini Mercury ndiyo sayari yenye joto kali sana kwenye mfumo wetu wa Jua kitu ambacho sio kweli, Venus - sayari ya pili kutoka kwenye Jua ndiyo yenye joto kali sana.

Joto kwenye sayari ya Mercury huwa linafika hadi nyuzi 400 wakati wa mchana na usiku kunakuwa na baridi kali sana licha ya kuwa karibu zaidi na Jua, nyakati za usiku joto linapungua hadi kufikia nyuzi -175 na hii inatokana na kutokwepo kwa angahewa (atmosphere) kwenye sayari hiyo kama ilivyokuwa kwa sayari nyingine hivyo joto lote huwa linapotea.
9a259a79b10238c9efdd85d51c225713.jpg
 
Utafiti mpya uliofanywa na NASA unaonesha pete maarufu zinazoizunguka sayari ya Saturn zinakaribia kupotea. Pete hizo ambazo ni mchanganyiko wa mapande makubwa ya mawe, barafu, na mavumbi ambayo yametokana na miezi midogo, vimondo, na mawe makubwa yaliyoharibika.

Utafiti huo umeonesha ndani ya miaka milioni 100 pete hizo zitatoweka kutokana na kuvutwa na uga sumaku uliokuwa kwenye sayari hiyo. "Kwa sasa kizazi chetu tunabahati sana ya kuziona pete hizo ambazo zipo katikati ya kipindi cha maisha yake" - alisema mmoja kati ya watafiti kutoka NASA.
1013fcc7796e1e1fa1551021c71db998.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
NASA washutumiwa kwa kuiacha Dunia bila ulinzi dhidi ya mawe makubwa yanayoweza kuja kuangamiza maisha hapa Duniani.

Tangu itengenezwe NEOCam mwaka 2006, kamera ambayo ilitakiwa itumike kuangalia usalama wa Dunia dhidi ya mawe makubwa hatarishi huko angani, kamera hiyo imewekwa tu bila mpango wowote na NASA wakuirusha angani kuanza kazi yake, lakini NASA wamekuwa na utayari wa kufanya safari zingine za ugunduzi wa kisayansi dhidi ya ulimwengu lakini sio kuirusha kamera ya NEOCam huko angani kwa sababu inaonekana haitowasaidia wanasayansi kujifunza kitu kipya kuhusu ulimwengu labda kama kuna jiwe kubwa jipya ambalo halikufahamika hapo awali linakuja kuelekea Dunia ilipo.

Habari njema kama NEOCam ikirushwa itawasaidia wanasayansi kuweza kugundua mapema mawe makubwa yanayokuja huku Duniani, ila haitosadia kuweza kuyakwepa na ndiyo maana NASA hawana mpango na hiyo kamera, pia habari nyingine njema kwa raia tuliokuwa huku Duniani endapo kama kamera hiyo ikiwekwa angani itatusaidia sisi kuweza kujiandaa dhitanzanifo kisichoepukika kwa sababu kwa teknolojia ya sasa hakuna shirika lolote la anga ambalo litaweza kuzuia jiwe kubwa kugongana na Dunia na kuna baadhi ya mawe huko angani ni makubwa sana kiasi cha kwamba kama likidondoka kwenye jiji kama Dar es Salaam linaturudisha moja kwa moja kwenye zama za mawe.
3ded72af0dfa9a9cbac7c71ea08bac4c.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Timu ya wanasayansi kutoka NASA, Caltech, na Honda washirikiana kutengeneza aina mpya ya betri za Fluoride ambazo zinaweza kuhifadhi chaji mara kumi ya betri za Lithium-Ion.

Wakati wakielezea betri hizo zinavyofanya kazi wanasayansi hao walisema betri za Fluoride si ni mara yake ya kwanza zipo kwa muda mrefu lakini zinahitaji joto la nyuzi 150 ndipo ziweze kufanya kazi.

Kwa sasa betri hizo za Fluoride sio tu zinaweza kuhifadhi chaji kwa muda mrefu bali usalama wake ni mkubwa sana tofauti na betri za Lithium-Ion ambazo huwa zina overheat na kulipuka hovyo.

Pia betri za FIB ni salama kwa mazingira kwa sababu athari zake katika upatikanaji wa nyezo za kutengenezea ni chache ukilinganisha na athari za uchimbaji wa lithium na cobalt. Hebu fikiria unaichaji simu yako mara moja tu kwa mwezi?
3b7dc1eb1eaf4b8ec4d64d2741b3596f.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Unajua kwamba tumbo lako ni moja kati ya viungo mwilini ambavyo hata vikiondolewa mwilini mwako bado utaweza kuendelea na maisha kama kawaida. Kazi kubwa nne za tumbo mwilini ni kukimeng'enya chakula, kutoa kemikali ambazo zinakilainisha chakula, kukifyonza na kukitoa.

Madaktari wanaweza wakaliondoa tumbo endapo ikatokea kansa au ajali. Mwaka 2012, mwanamke mmoja kutoka Uingereza aliondolewa tumbo lake lote baada ya kunywa pombe iliyokuwa na liquid nitrogen. Unaweza ukaondolewa tumbo lako kisha koromeo (oesophagus) lako likaunganishwa moja kwa moja kwenye utumbo mdogo na maisha yakaendelea bila matatizo.
57865f502c2b5b8c01bb9176ec9e0590.jpg
Aisee kwahiyo aliishi kwa muda gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom