Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kama ni mrefu wastan upo vizuri ila kuna wanaume wengine hawajiamin hasa wafupi wanavaa vyenye soli ndefu
...mimi nina kitambi, sio flat shoe tu ndo navaa , sipendi viatu vya kufunga gidamu, navaa vya kuchomeka tu sio nianze kuinama kusumbua kitambi changu nilichokisumbukia kwa muda mrefu

42186c23734edfe2b1594d680c1eeb5f.gif
 
Kuna aina nyingi ya viatu vya aina hii ambavyo vimekuwa vikiuzwa madukani lakini ni muhimu wakati unataka kununua kiatu cha aina hii unatakiwa kuzingatia malighafi ambayo imetengeneza kiatu.
Viatu vya ngozi huwa ni vizuri zaidi kwani huvaliwa muda mrefu bila kuharibika tofauti na viatu vya plastiki ambavyo hudumu kwa muda mfupi na kuchanika chanika.

...mzee wangu Mungu amrehemu, alininunulia kiatu kimoja cha ngozi yaani nimeanza nacho fomuwani hadi fomfoo ndo nikaamua kukitupa, kiatu cha ngozi hadi kikafanana na mimi
 
Jaribu kutumia manukato kiasi fulani kwani aina nyingine hudumu muda mrefu na unapojipulizia manukato ona unafanya hivyo kwa faida yako na sio kuhakikisha kuwa kila mtu anajua umetumia manukato ya aina fulani hapo ndiyo huleta shida kidogo kutokana na kutumia kiasi kikubwa cha manukato na hivyo kuleta shida kwa wengine.
Pia unashauriwa kutotumia manukato ili kuondoa harufu ya mwili kutokana na kutooga au kutokana na sababu nyingine hapo maana ya manukato hupotea. Manukato hupendeza iwapo yatapuliziwa wakati mwili na nguo zikiwa safi. Tumia aina ya manukato uipendayo ili kuweza kukuweka mrembo zaidi.
 
Vya ngozi vinadumu sana na vizuri mno
...mzee wangu Mungu amrehemu, alininunulia kiatu kimoja cha ngozi yaani nimeanza nacho fomuwani hadi fomfoo ndo nikaamua kukitupa, kiatu cha ngozi hadi kikafanana na mimi
 
Mambo yanayoharibu katika urembo ni pamoja na kutokuangalia fiziki yaani kutofanya mazoezi. Hata kama hakuna mtu ambaye atakuona kuacha kufanya mazoezi, kutojali usafi kunatibua muonekano wako na kuondoa kujiamini.
Kitu kingine ambacho watu huwa hawakijali ni kusafisha na kurekebisha meno yao. Unapotabasamu kitu cha kwanza kuonekana kwa watu ni meno yako. basi jaribu kuyajali kidogo. yasafishe na hakikisha yanapendeza.

...mtu meno yana layer ya njano akitabasamu utadhani mdomoni kuna mgodi wa dhahabu.
 
Unachotakiwa na kufutafuta limao au ndimu unaikata kisha unakamua. Chukua kitambaa weka maji maji ya limao na kisha anza kusugua taratibu kwapa lako.
Hakikisha unafanya hivyo wakati ukiwa umetoka kuoga. Pia unaweza kukata limao au ndimu bila ya kukamua na kuanza kusugua katika kwapa lako. Vitu hivyo vina nguvu za kuondoa uchafu katika kwapa.
Baada ya hapo unaosha au,,?
 
Ni muhimu kusafisha kwapa kwani kwapa linapokuwa si safi hata unapovaa nguo ya wazi unakuwa huna uhuru wa kunyanyua mkono juu pindi inapokulazimu kufanya hivyo.
Kwapa ni sehemu muhimu sana ni lazima iangaliwe kwa namna ya pekee na uhakikishe unakuwa safi muda wote ili kuondoa harufu na muonekano mbaya katika kwapa.
asante
 
Kama wewe ulivoyafanyaa kwa kuagaa kwamba unaendaa ile sehemu kumbe umekachaaa ila anko wangu unajijuaa wewe


...ile sehemu nilienda ila ndo hivyo nikakuta umeacha chata tayari, ikabidi niwe mpole, ila sasa safari hii anko usimtelekeze kama ulivyomfanya yule teller wa bank kule tanga, unatujazia watoto wasio na mama tu
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Moja ya vitu ambavyo humfanya mtu kuwa na furaha na maisha mazuri ni ubashashi unaombatana na kuondoka kwa mikonjo ya moyo kwa kupata huduma ya ngono.
Nyingi ya dawa zinazoleta hamu ya ngono puia husaidia kurekebisha mfumo wa afya ya mwanamke, ndio maana nimetaka kwa hapa kidogo kuzungumzia vyakula vya kuleta ashki
Watafiti wamesema kwamba kuna aina fulani ya vyakula huleta ashki kubwa kiasi cha kuwafanya watu wawe na hamu ya kufanya ngono.


...ngoja nikae kiti cha mbele kabisa, hili somo zuri na tunakoelekea utatufundisha na mastyle maana mama yenu anataka style za kikiristo tu. Asante
 
...ile sehemu nilienda ila ndo hivyo nikakuta umeacha chata tayari, ikabidi niwe mpole, ila sasa safari hii anko usimtelekeze kama ulivyomfanya yule teller wa bank kule tanga, unatujazia watoto wasio na mama tu
Alafuu kama ulikuwepooo wa tanga kanidiiiipuuuu
 
Vyakula hivyo vimedaiwa kuwa na aina fulani za kemikali ambazo hufumua mifumo ya tamaa na kufanya dai la kufanya ngono kuwa na nguvu zaidi.
Kutumia chakula kitamu kwa upungufu na kupata lishe kamili yenye uhakikakunaweza kukufanya wewe kufurahia ngono na kutamani kama masuala hayo yameanza kukimbia.
Yaani ukipata dozi inayotakiwa ya protein, carbs, na fats ni dhahiri utakuwa na nguvu zaidi kuliko hapo awali.
Lakini kabla sijakuchanganya zaidi natakakusema kwamba kuwa na nguvu ni kitu kingine na kuwa na hamu ya kufanya ngono na kuimudu ni kitu kingine.

...ukishapata dozi hii halafu uwe na hela sasa na uwe umelipa madeni yote, ukiachana na lile la bodi ya mikopo basi hamu inafika kileleni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom