Dunia ya leo ni ulimwengu wa wanawake wanaojipamba na kuonekana warembo zaidi.
Wanawake ambao wana uzuri wa asili hasa wale ambao wametunza ngozi zao nyeusi za asili hupendeza sana kama watajipamba kwa vitu vya asili kama kuvaa hereni, mikufu au bangili zilizotengenezwa kwa vitu vya asili kama vifuu vya nazi, magome ya miti au kutengenezwa kwa kutumia shanga.
Wakati huu wanawake wenye uwezo kifedha wamekuwa wakitumia fedha zao kujipamba kwa mapambo ya gharama kubwa kama kuvaa mikufu na saa zenye za dhahabu na hata madini mengine yenye thamani kubwa kama almasi.
Uvaaji wa mikufu, hereni, bangili ni mambo ambayo mwanamke anatakiwa kuyazingatia ili kuweza kuongeza urembo wake.