Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kwa afya njema ya kinywa chako, unashauriwa kupiga mswaki mara mbili kwa siku. Wakati unafanya hivyo, usiwe na haraka. Chukua muda wa kutosha kusugua meno yako yote kwa ukamilifu huku ukihakikisha kila kinachopaswa kuondolewa kimefikiwa.

Kulingana na umri, mazingira au hali ya afya, unashauriwa kutumia mswaki sahihi utakaokufaa pamoja na dawa ya meno iliyo na madini ya floridi. Mswaki mzuri ni ule ambao visafishio vyake havikuumizi na unaokaa vizuri kinywan

Watoto wapewe mswaki unaofanana na umri wao ili kufanikisha hili. Wale wadogo wasimamiwe ili kuzingatia namna ya upigaji na kuepuka kutomeza dawa ya meno ambayo haipaswi kumezwa.

Kanuni ya tatu ni kujizoeza njia nzuri za kupiga mswaki. Unapaswa kuushika mswaki wako kwa namna ambayo visafishio (brashi) vyake vitalenga kwenye makutano ya meno na ufizi.
 
Unachotakiwa kufanya ni kusafisha meno yako kwa mwendo mfupi wa kwenda mbele na nyuma, juu na chini. Kumbuka kusafisha nje, ndani na sehemu za kutafunia. Halikadhalika usisahau kusafisha ulimi kwa kutumia mswaki wakati ukipiga mswaki.

Ni muhimu kuutunza mswaki katika hali ya usafi kila baada ya kuutumia. Mara zote safisha mswaki wako kwa maji safi umalizapo kuutumia. Unapouhifadhi, usimamishe ili ukauke mpaka utakapoutumia tena.


Kama una miswaki kadhaa na yote unaitunza mahali pamoja, tenganisha huu uliotumia sasa na hiyo mingine ili kuzuia maambukizi ya bakteria. Weka mswaki wako mahali penye hewa ya kutosha vinginevyo huweza kuchochea ukuaji wa bakteria na fangasi kwenye mswaki wako ambao wanaweza kukusababishia maambukizi ya mgonjwa ya kinywa au mwili kwa ujumla.
 
Kanuni ya tano na mwisho kwa leo ni kutambua wakati sahihi wa kubadilisha mswaki wako. Mswaki hupoteza ubora wake kadri uutumiavyo hivyo kustahili kubadilishwa. Kila mtengenezaji anapaswa kuandika mswaki unaoununua unastahili kutumika kwa muda gani…ingawa hufanya hivyo ila wengi hatuzingatii kusoma maelekezo yaliyomo. Lakini ipo kanuni ya jumla. Unatakiwa kuhakikisha unatumia mswaki mpya kila baada ya miezi matatu mpaka minne. Ni vyema kama utafanya hivyo chini ya muda huo au pale utakapoona umeanza kuharibika.
 
Flosi

Flosi ni uzi maalumu uliotengenezwa ili kusafisha katikati ya meno ambamo brashi za mswaki haziwezi kufika na kutekeleza lengo hilo. Hivyo, kuflosi ni kusafisha maeneo yaliyo kati ya jino na jino ambayo hayawezi kufikiwa na mswaki.
 
Kutokana na ugumu wa kupiga mswaki maeneno ya kati jino na jino, inashauriwa kusafisha mara moja kwa siku ili kuimarisha usafi kamili wa kinywa na kujihakikishia siha njema.


Zipo kanuni au taratibu za kuzingatia. Kwanza unashauriwa kukata uzi wa kufanyia flosi wa kutosha. Kwa mtu mzima, inapendekezwa uwe na urefu walau sentimita 45.
 
Kisha zungusha sehemu kubwa ya uzi huo kwenye kidole cha kati cha mkono mmoja na fanya vivyo hivyo kwenye kidole cha kati cha mkono mwingine.


Flosi hufanywa taratibu. Unashauriwa kuelekeza na kuupitisha uzi kati ya meno ukitumia na kusugua. Sugua meno na sio ufizi. Fanya hivyo kutoka jino moja kwenda jingine kwa zamu.
 
Flosi jino moja kwa wakati mmoja. Jiridhishe kwa ukamilifu ulioufanya kwenye jino la kwanza kabla hujahamia la pili. Flosi taratibu kwa kusugua kwenye jino kwa kwenda juu na kushuka chini.


Habari njema ni kwamba hujachelewa kwani ukifanya kazi yako vizuri, haijalishi umeanza lini kupiga mswaki au kuflosi matokeo ni sawasawa. Utakuwa na afya njema na utajiamini popote utakapokuwa.
 
Auntie zako wananisumbua huku,,,kila siku wananiuliza aunt anakuja ln
ntakuja jumapili niwasalimie
watafurahi sana
waulize wanataka zawadi gani niwaletee
Unadhan hata wana mambo mengi,,mmoja hapa anataka popcon mwingine chocolate
Sawa kumbe ntajtahid niwaletee
ABJ twende tukawasalimu akina anti
Tena kama ABJ toka amewaona ni muda mrefu,,,wanamuuliza yule aunt anapenda kuja na ice cream yupo wapi
ngoja nimshawishi nije nae kwa kweli
Ninge kumbe na wewe una watoto wa insta kama tumosa yaani watoto wa kuchorwa
 
TUOMBE:Baba Mtakatifu Mungu wetu mwenye upendo mkuu Asante sana kutuamsha salama leo Jumamosi tarehe 27 Oktoba 2018 tukiwa wenye Afya njema .Wapo wengi walitamani kuiona leo Hawajaweza.. Tunawaombea wote waliopoteza ndugu,jamaa ,marafiki wenza wapate faraja kuu tunawaombea wajane,wagane yatima wapate tumaini na kukutegemea wewe tu Baba wa ya yatima.Tunaomba Amani itawale.Tunajikabidhi leo hii mikononi mwako kaa nasi Baba ongoza ratiba zetu zote uwe nasi katika Majonzi ,katika furaha,katika kazi hesabu hatua zetu tukutangulize katika kila jambo Mfalme wa Amani.Uwe Tumaini letu katika yote .Tujalie safari njema majini ,nchi kavu,angani tuende na kurudi salama..Tunaomba bariki kazi za mikono yetu tusaidie tupate yote ambayo umetujalia.Mungu wetu tunawaombea watoto na wajukuu zetu wawe salama popote walipo...Wasaidie watoto wetu wakujue na wakufuate wewe katika maisha wakutegemee katika kila jambo.Tunaomba Amani Mshikamano, kuvumiliana na Upendo wako utawale.Ponya wagonjwa na wote wanaopitia changamoto mbalimbali na watu wote wapate haja za mioyo sawasawa na mapenzi yako.Roho Mtakatifu kaa nasi .
Tunaomba yote katika jina la Yesu Kristo Amen.
JUMAMOSI NJEMA YA BARAKA DAMU TAKATIFU YA YESU KRISTO ITUFUNIKE
Ameeeeeeen
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom