Makapuku Forum

Makapuku Forum

Hili ndilo swali ambalo Elon Musk anauliza watu kwenye usahili wa kazi na wengi wanashindwa kulijibu. Vipi wewe unaweza ukalijibu hilo swali?
Screenshot_20181025-190202.jpeg
 
Wanafalaki wagundua mkusanyiko mkubwa zaidi wa galaksi wenye umri wa miaka bilioni 2.3 tangu kutokea Big Bang, mkusanyiko huo uliopewa jina la Hyperion ndiyo eneo kubwa kugunduliwa mpaka sasa tangu kuanza kwa ulimwengu.

Ukubwa wa eneo hilo ni mara 5,000,000,000,000 ya Jua letu au sawa na mara 10,000 ya eneo zima la galaksi yetu ya Milky Way.
Screenshot_20181025-190258.jpeg
 
Kuchunguzwa na serikali katika kila kitu unachokifanya ni jambo la kawaida sana nchini China, ila kwa hili la kuanza kuchunguza idadi ya waislamu nchini humo limevuka mipaka.

Hivi karibuni serikali ya China imepitisha sheria mpya ambayo inazitaka kampuni zote za teknolojia zinazotoa huduma nchini humo kuanza kuchunguza mienendo na tabia za waumini wa kiislamu nchi nzima.

Serikali ya China wamekuja na mpango huo kama sehemu ya kuwazuia waislamu wenye misimamo mikali wanaotaka kuingilia mipango ya serikali.
Screenshot_20181025-190409.jpeg
 
Mate Pro ndiyo simu yenye teknolojia ya hali ya juu kutoka Huawei kwa sasa. Simu hiyo inategemewa kushindana sokoni na simu kutoka Apple na Samsung - ambapo kupitia simu hiyo utaweza kufyonza chaji kutoka kwenye simu ya rafiki yako bila waya (wirelessly) endapo utakuwa hauna chaja au power bank.

Huawei Mate Pro itaanzia dola 1,215 (2,700,000) ikiwa na skrini ya inchi 6.39, finger print, kamera ya mbele yenye megapikseli 20 na nyuma 40. Tangu kuachiwa kwa simu hiyo imesaidia kuirudisha kampuni ya Huawei kwenye soko la simu haraka, huku wakiipita kampuni ya Apple katika simu zilizouzika sana mwaka huu.
Screenshot_20181025-190527.jpeg
 
Huyu jamaa alikuwa ni mwanafunzi anayechukua ujuzi NASA, alishakaa jela miaka 6 kwa kosa la kuiba mawe yenye uzito wa kilo 7 ambayo wanaanga walitoka nayo mwezini.

Jamaa alifanya hivyo vyote ili tu kumfurahisha mchumba wake ambaye alijuana naye kwa wiki tatu, basi aliiba hayo mawe kisha akayatandaza kwenye shuka la kwenye nyumba ya wageni halafu wakafanya mapenzi juu ya hayo mawe.

Kosa kubwa alilolifanya ni kujaribu kuyauza hayo mawe mtandaoni pasipo kufahamu mtu anayemuuzia ni askari upelelezi wa FBI.
Screenshot_20181025-190635.jpeg
 
Kondomu hizo ambazo zilifadhiliwa na shirika la "Bill and Melinda Gates Foundation" zinauwezo wa kuhimili zaidi ya misukumo 1,000 au sawa na kwenda dakika 16 mfululizo bila kusimama.

Katika utafiti uliofanywa pia unaonesha kwa kawaida tendo la kujamiiana linahusisha misukumo 100 mpaka 500.
Screenshot_20181025-190746.jpeg
 
Serikali ya China wapo mbioni kutengeneza mwezi bandia na kuurusha angani ifikapo mwaka 2020. Mwezi huo bandia utatumika kuangaza jiji la Chengdu lenye wakazi wanaofikia milioni 14.
Screenshot_20181025-190935.jpeg
 
Back
Top Bottom