Makapuku Forum

Makapuku Forum

.
Screenshot_20181024-194119.jpeg
 
Watoto wawili walio tumboni wamefanyiwa upasuaji wa uti wa mgongo, ili kuziba shimo walioumbwa nalo wakiwa ndani ya tumbo la mama yao.

Operesheni hiyo ya kihistoria iliyowajumuisha madaktari 30 katika hospitali moja huko Uingereza. Watoto hao walikuwa wanaugua ugonjwa unaofahamika kama Spina Bifida.
Screenshot_20181025-185403.jpeg
 
Endapo itatokea binadamu tukakutana na Aliens, basi kuna uwezekano mkubwa wa sisi kuwaua kulingana na mwanafizikia za nadharia Alexander Berezin kutoka nchini Urusi alivyoandika kwenye utafiti wake. Hii ikiwa na maana kama binadamu tukiweza kukutana na Aliens, basi sisi tutakuwa ndiyo viumbe wenye akili sana kuliko wao na kwa kipindi hicho tutakuwa na uwezo wa kusafiri mbali zaidi ulimwenguni

(Intersteller Travel) kuliko wao na kama wakijaribu kutuzuia sisi kuwatawala tutawaua kulingana na teknolojia ya juu ambayo tutakayo kuwa nayo kwa wakati huo - yaani kati ya wao na sisi atakaye kuwa wa kwanza kusafiri mbali zaidi ulimwenguni (Intersteller Travel) ndiye atakaye kuwa yupo juu zaidi kwa teknolojia na kama wao wakifanikiwa kufika Duniani basi tumekwisha na sisi tukifanikiwa kuwatembelea wao basi wamekwisha.

Kwenye galaksi yetu ya Milky Way peke yake kuna zaidi
ya nyota bilioni 100 ambazo wanasayansi wanaamini baadhi ya nyota hizo zinazungukwa na sayari ambazo zinaviumbe hai walioendelea kuliko sisi na huenda tayari wameshaanza kutembelea nyota wakati sisi bado hata kwenye sayari ya Mars hautajifika - tuombe wasije wakatufikia kabla ya sisi kuwa na uwezo wa kusafiri mbali zaidi.
Screenshot_20181025-185658.jpeg
 
Mwanasayansi nguli wa masuala ya anga - marehemu Stephen Hawking alishaonya kwamba hapa Duniani tumebakiza miaka michache sana ya kuishi muda wowote linaweza likaja janga kubwa ambalo litapelekea Dunia kuangamia pamoja na binadamu kutoweka kabisa ulimwenguni kama ilivyokuwa kwa dinosa.
Screenshot_20181025-185920.jpeg
 
Jopo la wachunguzi kutoka chuo cha Georgetown, kwa kutumia mifano hai wameweza kugundua madhara makubwa yanayoweza kutokea kwa binadamu endapo atasafiri kwenye anga la ndani zaidi.

Katika utafiti huo inaonesha sehemu kubwa ya tumbo itaharibika kutokana na miale iliyokuwa nje ya Dunia (Galactic Cosmic Radiation), ambayo yenyewe haiwezi kutudhuru huku Duniani kwa sababu Dunia yetu ina uga wa sumaku unaozuia miale hiyo kuja moja kwa moja
Screenshot_20181025-190050.jpeg
 
Back
Top Bottom