Makapuku Forum

Makapuku Forum

1.diet coke.



Hata kama nimekuwa nikiisikia muda mrefu sana , lakini bado natamani kuionja. Kinywaji hiki kimekuwa kikidanganya watu kuwa hakina madhara , lakini kumbe kinasababisha mtu kupata magonjwa ya kisukari, maumivu ya miguu, kupata kitambi, inapoteza hamu ya kawaida ya kula. Watu wanaotumia kinywaji hiki waache mara moja.
 
2.Vyakula Vya Kwenye Makopo Na Vile Vilivyotunzwa Muda Mrefu Kwenye Friji.





Watu wametegwa kwenye vyakula vilivyo tayari, ambavyo vimetengenezwa tayari na wewe kazi yako ni kupasha na kula. Hivyo vyakula ni sumu kali hatujui tu., vinakuwa vimewekwa chumvi nyingi sana kwa ajili ya utunzaji , na ndio maana utakuta watu wanaongezeka uzito sana,

Ukweli ni kwamba, sodium inaweza kuwa na kazi kubwa ya kuthibiti insulini kuliko ilivyokuwa mwanzo.
 
3.Nafaka.



Watoto wa kileo siku hizi wanataka chai yao iwe ya maziwa na nafaka, tumefunikwa macho yetu kuona kuwa nafaka zilizofungwa kwenye mabox ni halisi. Lakini kumbuka kuwa wamejaza vyakula vya wanga tena vilivyokobolewa vikatolewa viini vyake. , na vina sukari nyingi ili kuleta ladha ya hicho chakula. Ondoa hicho chakula kwa watoto na kwenye diet.
 
4.Vyakula Vinavyotengenezwa Hotelini Kutumia Viungo Mbalimbali.



Tumekuwa tukila chemicals nyingi hasa hotelini , maana kila kiungo chao ni ready made, kwa maana kimetengenezwa tayari muda mrefu. Na huko mahitaji yao huwa sio fresh, wanatumia vitu vilivyokaa muda mrefu wengi wao. Nakushauri tu kutumia chakula cha nyumbani amacho ni fresh kwa ajili ya afya yako , kama unajali.

Lakini unaweza kuagiza aina ya chakula ambacho hakina viungo kabisa, na lazima uwe unafahamu kuwa kitakuwa fresh.
 
5.Doughnut.



Donati zinanukia vizuri na zinavutia kwa macho lakini ni chakula ambacho kitakuletea uzito mkubwa, kwa sababu kila unaposikia njaa zenyewe zipo tayari pamoja na soda . acha kutumia donat , tumia matunda kama apple, pears, parachichi unapokuwa una njaa.
 
6.Keki za mitaani na mikate iliotengenezewa Siagi.



Nimekuwa nikifikiri kuwa keki na mikate ni nzuri kwa sababu imetengenezwa na unga na mayai. Lakini kumbe ni hatari sana kula keki , mikate myeupe , kidogo ule mkate wa unga usiokobolewa . kila ukinunua keki za kiwandani soma kiti yake imetengenezwa na nini utaona jinsi zilivyo na sukari nyingi . vitakusababishia kupata kisukari na uzito wako kuwa mkubwa. punguza au acha kabisa kula hivyo vitu.
 
VYAKULA VYENYE NGUVU YA KUPIGANA NA SARATANI:

Kwa watu ambao wanahitaji afya njema , saratani yaweza kuwa ni woga mkubwa sana kwao, kwa sababu zaidi ya hapo ni kifo .Ulimwenguni mwote watu wanahaha kutafuta jinsi ya kuepukana na ugonjwa huu ambao matibabu yake ni makubwa, kimwili kiuchumi na kihisia.

Matibabu yake ni ya upasuaji mkubwa, mionzi, kidini na yote hio ni hatari tu. hata hivyo kuna habari nzuri kwamba, kuna kubadili mtindo wa kula chakula chako, kuna mtindo rahisi sana ambao kila mtu anatakiwa kuchagua huo ili kupunguza hatari ya kupata saratani. moja ya chaguzi hizi ni diet ambayo imekusanya vifuatavyo.
 
Mboga Ya Cruciferous.



Mboga ya cruferous ni lishe yenye nguvu na imekusanya vifuatavyo , broccolli,qauliflower na kale, hizi zote ni mboga bora katika kundi lote la mboga ambazo zinapigana na saratani, kula hizi mboga kila siku ukiweza. kama una mazoea ya kufuatilia jinsi ya kuzuia saratani tumia diet hii.

kwa nini? zina sulfur ambayo ina sulforaphones, haya ni maneno ya kichemia. vina uwezo wa kusukuma mwili kupigana na saratani. inasaidia kuzuia aina tofauti za saratani , kama ya ini, tumbo, ngozi na bladder.
 
Berries.



Hii ni aina nyingine pia imehakikishwa kuwa ina uwezo mkubwa wa kuepukana na athari ya saratani ukiwa unatumia mara kwa mara. na ni tamu sana utazifurahia , katika kundi hili kuna, straberries, cherries, blueberries na akai berries.
 
Alliums.



Alliums imekusanya vifuatavyo, vitunguu maji , vitunguu thoum, chives, leeks. hivi sio tu kuwa dunia nzima inavipenda kwa kuwa vinaongeza ladha kwenye vyakula, hapana. ni moja ya vyakula vinavyopigana sana kuzuia saratani na vitu vyote vinavyoharibu mwili. vinasaidia kuepukana sana na saratani ya esophagus stomach na saratani ya utumbo mkubwa.
 
Nyanya.



Nyanya ni kiungo kizuri kwenye vyakula mbalimbali, lakini pia ni chakula kinachosaidia kupigana na saratani. tumia kama mboga zingine, hasa kachumbari ni nzuri iliyotengenezwa na nyanya. tumia kama diet.
 
mboga ya kijani ya leefy.



Zipende mboga za kijani, penda mboga ya kale, spinachi na mboga zingine zote zenye kijani iliokolea. leefy green zinatengenezewa salad, supu, pasta na casse roles, zina faida kubwa mwilini , kwa kuwa zinazuia saratani hasa ya mdomo na koo.

Pamoja na kwamba hakuna risasi ya kuipiga saratani inapoingia mwilini, lakini kuna njia nzuri za kuzuia isiingie mwilini mwako.
 
Back
Top Bottom