Makapuku Forum

Makapuku Forum

NJIA KUMI ZA HARAKA KUONDOA “STRESS” NA UCHOVU

1.Pitia picha zako zako za zamani kidogo, Picha za tukio moja wapo lililokufurahisha au za mtu mwingine yeyote wa karibu yako!

2.Fungua madirisha na kuruhusu mwanga na hewa kupita kwa kiasi kikubwa. Epuka kukaa sehemu yenye mwanga mdogo kwani hufanya hali yako ya uchovu au stress kuwa juu zaidi.

3. Imba huku unaoga! Sio lazima uwe muimbaji mahiri bali chagua tu wimbo wako unaoupenda, imba kwa namna yeyote huku ukiendelea kuoga

4. Epuka kubaki mpweke. Tafuta mtu yeyote uongee nae (hata mtoto mdogo) itakusaidia kupunguza mawazo au uchovu
 
5. Sikiliza muziki au mpigie simu rafiki yako mliyepotezana muda mrefu.

6. Fanya Mazoezi (japo kwa dakika moja)

7.Badilisha Mazingira, Mfano kama unapita njia hiyohiyo moja kutoka kazini/shule, badilisha na upite nyingine.

8. Fanya utafiti wa kijinga kwa kuwaangalia wapita njia na kutoa kasoro zao kimavazi, muonekano wao bila ya wao kujua.

9. Nenda Saluni kunyoa/kuosha/kusuka nywele zako.

10. Chukua kalamu na karatasi, anza kujifunza kuchora!
 
KWA MWENYE AKILI TIMAMU LAZIMA UJIULIZE MASWALI HAYA KUMI KABLA SIKU HAIJAISHA

1.Je, leo nina nafuu yoyote kuliko jana? Kama ipo ni ipi?

2. Ni Kitu gani kipya nimejifunza leo?kama hakuna basi soma hata kitabu ukurasa mmoja.

3. Kuna maamuzi yapi mapya au chaguzi zipi nimefanya kuboresha maisha yangu?

4.Kuna chochote nimefanya kwa ajili ya mtu mwingine au dunia kwa ujumla. Kumbuka sio kila zuri unalofanya lazima likufaidishe wewe au ndugu yako moja kwa moja, bali mazuri yaw engine ndiyo yatakayokunufaisha wewe na jamii yako.



5. Je, nimemuudhi nani leo? Au pengine
nimekwaruzana na nani? Na je nini hatma yake?
 
6. Je, nini umekifanya kwa ajili ya kesho?

7.Umetimiza kiasi gani mipango uliyojiwekea hapo kabla?

8. Nitafanya nini Kesho ili Kurekebisha nilipokosea leo?

9. Je , nimeonesha upendo kiasi gani kwa familia yangu kwa ujumla? mzazi, mke, mume, watoto au hata mpenzi wako.

10. Ni lipi limekuudhi zaidi na ni lipi limekufurahisha pia?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom