Makapuku Forum

Makapuku Forum

Ani Liu, ni mbunifu ambaye anatumia sayansi na teknolojia katika kazi zake ili kutengeneza marashi tofauti tofauti, hivi karibuni amekuja na njia mpya ambayo itawawezesha watu kuhifadhi kwenye chupa harufu za watu wanaowapenda kwa muda mrefu/ikiwezekana milele.

Liu anaondoa harufu za muhusika kwenye nguo kisha anahifadhi kwenye chupa kama kumbukumbu kwa muda mrefu na kwa sasa tayari amesha fanya kwa watu sita:

Mume wake, yeye mwenyewe, wazazi wake, msaidizi wake, na mkemia ambaye anamsaidia.

Liu anasema alifanya hivyo kwa wazazi wake kwa sababu anajua kunasiku wataondoka Duniani, hivyo anataka kubaki na kumbukumbu ya jinsi wanavyonukia.
Screenshot_20180907-185240.jpeg
 
Watafiti kutoka chuo cha MIT wafanikiwa kutengeneza kifaa ambacho ukikivaa kinaweza kutambua maneno yote unayofikiria kichwani mwako ila hauyasemi, kwa kutumia ishara ambazo ubongo unazituma kwenye sura na taya la chini pale mtu anapotaka kuongea.

Kifaa hicho kinachoitwa AlterEgo Headset kinadaka mienendo ya misuli ya neva ambayo huwa inafanyika pale mtu anapotaka kuongea kisha inabadilisha mienendo hiyo kuwa maneno ambayo mtu alikuwa anataka kuyasema.

Utafiti uliofanywa kwa watu mbali mbali unaonesha uwezo wa kifaa hicho kuweza kufanyakazi kwa asilimia 92pia mtu anaweza akatumia kompyuta au simu kwa mawazo yake akiwa amevaa kifaa hicho.

Screenshot_20180907-185630.jpeg
 
Kwa mara ya kwanza wanasayansi wafanikiwa kugundua kilichomo ndani ya mapiramidi yaliyoko Misri.

Kupitia cosmic particles wanasayansi waliweza kuona ndani ya mapiramidi hayo ambayo yalitengenezwa miaka 4,500
Screenshot_20180907-185823.jpeg
 
Ikifika mwaka 2050 wanasayansi wamewahakikishia matajiri uwezo wa kuishi milele kwa kuweza kupakia kwenye kompyuta taarifa zote zilizokuwemo kwenye ubongo, hivyo kuwafanya waendelee kuishi ndani ya kompyuta hata baada ya kufa.

Ila watu masikini itabidi wasubiri mpaka mwaka 2075 au 2080, wakati teknolojia hiyo itakapokuwa nafuu na kawaida kwa kila mtu.
Screenshot_20180907-190007.jpeg
 
Mshambuliaji wa klabu ya Tottenham, Lucas Moura ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa Mwezi wa Nane (Agosti) ndani ya Premier ya England, Katika Mwezi huo Mbrazil huyo wa kwanza tokea 2011 kutwaa tuzo hiyo amefanikiwa kufunga magoli Matatu (3) na kutoa Assist Moja (1) klabu yake ikishinda Mechi tatu ndani ya Mwezi huo......

Moura amewashinda Wachezaji Marcos Alonso wa Chelsea, Neil Etheridge wa Cardiff City, Benjamin Mendy wa Manchester City, Roberto Pereyra wa Watford, Sadio Mane na Virgil Van Dijk wote wakikipiga na Liverpool.
.
•Wakati huo huo Kocha mkui wa Watford, Javi Gracia ameshinda tuzo ya kocha bora mwezi wa nane (Augosti) ndani ya Premier ya England...Katika mwezi huo, Gracia aliiongoza Watford kushinda mechi zote tatu (3) ndani ya mwezi huo Pia Amewabwaga makocha Jurgen Klopp wa Liverpool, Mauricio Pochettino wa Tottenham na Maurizio Sarri wa Chelsea.
.
•Pia Tuzo ya Goli Bora la Mwezi wa nane (Agosti) imebebwa na Kiungo wa Klabu ya Fulham, Jean-Michael Seri, ni goli ambalo alifunga katika mchezo wa Premier League dhidi ya Burnley..
Screenshot_20180907-191510.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom