Blackburn haitomruhusu Bradley Dack, mwenye umri wa miaka 24, kuondoka kwenye klabu hiyo baada ya kuktaa ombi lenye thamani ya ziada ya £ milioni 5 kwa mchezaji huyo wa West Brom. (Sky Sports)
Beki wa kulia wa England Danny Simpson, mwenye umri wa miaka 31, na mchezaji wa kiungo cha kati wa Wales Andy King, 29, wanatarajiwa kuondoka Leicester kabla ya muda wa mwisho leo Ijumaa wa uhamisho wa kimataifa.(Leicester Mercury)
Aliyekuwa mchezaji wa kiungo cha kati wa England Gareth Barry, aliye na miaka 37, atakuwa na jukumu kuu kwa West Brom msimu huu kwa mujibu wa meneja Darren Moore. (Express and Star)
Pazia la michuano ya klabu bingwa Ulaya msimu wa 2018/19 limefunguliwa kwa kupangwa makundi ambapo klabu ya Manchester United inapambana na nyota wake wa zamani Cristiano Ronaldo aliyehamia klabu ya Juventus.
Ronaldo alikipiga na United kwa miaka sita (2003-2009) kisha akachezea Real Madrid kwa miaka tisa na mwezi Julai mwaka huu akahamia klabu ya Juventus, maarufu kama Bibi Kizee wa Turin. Ronaldo ameifunga United mara mbili walipocheza na Real Madrid katika michuano kama hii mwezi Februari na Machi 2013.
United na Juve zimepangwa katika kundi H pamoja na Valencia na Young Boys ya Uswizi.
Timu ya Real Madrid ambayo ilinyakua ubingwa kwa kuwafunga 3-1 katika fainali ya msimu uliopita wameondoka na ushindi mwengine baada ya wachezaji wake kunyakua tuzo zote zilizoshindaniwa.
Luka Modric amenyakua tuzo ya kiungo bora wa mwaka pamoja na ya mchezaji bora wa bara Ulaya.
Keylor Navas amenyakua tuzo ya kipa bora, Sergio Ramos beki bora na Cristiano Ronaldo mshambuliaji bora.
Mchezaji wa zamani wa Manchester United na Real Madrid David Beckham alipewa tuzo ya heshima ya Rais wa Shirikisho la Soka la Bara la Ulaya UEFA.
"Kuanzia kunyakua ubingwa wa Ulaya na Real Madrid na kufikia hatua ya fainali ya Kombe la Dudia na timu ya taifa langu ya Croatia mpaka kupata tuzo hii, nasikia fahari sana kwa kila nilichofanikisha mwaka huu. Huu ni mwaka bora kabisa katika maisha yangu ya mpira," alisema Modric.
Dirisha la uhamisho la klabu za Uingereza tayari limefungwa lakini BBC michezo inaangazia makubaiano ambayo huenda yakakamilishwa barani Ulaya
Timu zilizopo nje ya Uingereza zinaweza kufanya makubaliano ya uhamisho hadi saa moja usiku saa za Afrika mashariki , huku madirisha ya uhamisho ya Uhispania, Ujerumani na Ufaransa pia yakifungwa siku ya leo.
BBC Michezo inaangazia baadhi ya wachezaji wa Ulaya ambao huenda wakamia klabu mpya.
Position:Kiungo wa katiUmri:30Anahusishwa na: Paris St-Germain
Kuwasili kwa Arturo Vidal na Arthur kunatoa ushindani mkubwa kwa Ivan rakitric katika safu ya kati ya klabu ya Barcelona.
Huku hatma ya mchezaji wa Ufaransa Adrien Rabiot ikiwa haijulikani katika klabu ya Paris St-Germain, klabu hiyo ya Ligue 1 inamnyatia kiungo huyo wa kati wa Croatia na wanataka kuimarisha kitita cha uhamisho wake cha £112m
Uwezekano wa beki huyo wa Ujerumani Boateng kusalia na mabingwa hao wa Bundesliga uko nusu nusu
Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester City alihusishwa na uhamisho wa Manchester United msimu huu , lakini klabi hiyo ya ligi ya dara la kwanza huenda ndiko anakoelekea.
Position:Kiungo wa katiUmri:29Anahusishwa na:Sevilla, Marseille
Kiungo wa kati wa zamani katika klabu ya Manchester United Kagawa hakushiriki katika mechi ya ufunguzi wa klabu ya Dortmund dhidi ya RB Leipzig na ameripotiwa kutokuwa miongoni mwa mipango ya meneja mpyaLucien Favre
Huku mchezaji mpya aliyesajiliwa Axel Witsel na Thomas Delaney wakitarajiwa , mchezaji huyo wa Japan huenda akaondoka katiika uwanja wa Westfalenstadion katika siku ya mwisho ya uhamisho.
Kandarasi ya kiungo wa kati wa Itali Marchisio katika klabu ya Juventus ilikatizwa kutokana na makubaliano kati ya pande zote mbili na sasa anatafuta klabu mpya.
Porto na Benfica wamehusishwa ijapokuwa klabu nchini Ureno zina hadi tarehe 21 Septemba kufanikisha makubaliano yao.
Position:Kiungo wa katiUmri:24Anahusishwa na😛AOK, Anderlecht
Ni kweli kwamba bado ni mchezaji wa Liverpool. Raia huyo wa Serbia alijiunga na Liverpool kwa dau la £20m kutoka benfica 2014, lakini hajaichezea klabu hiyo tangu 2015.
Position:Kiungo wa katiUmri:22Anahusishwa na: Monaco, Schalke
Loftus-Cheek alihudumu msimu uliopita kwa mkopo katika klabu ya Crystal Palace, ambapo mchezo wake ulimfanya kuitwa katika kikosicha cha timu ya taifa ya Uingereza cha kombe la dunia.
Huku Jorginho, N'Golo Kante, Ross Barkley na Mateo Kovacic wakiwa mbele yake katika wachezaji wanaotarajiwa kucheza katika kikosi vcha kwanza cha timu katika klabu ya Stamford Bridge, Loftus-Cheek huenda akaanza kutafuta klabu mpya.
Mwanariadha wa Kenyan Conseslus Kipruto alikaidi pigo la kupoiteza kiatu mapema ili kuibuka mshindi wa mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji katika ligi ya almasi ya IAAF Diamond League mjini Zurich, nchini Switzerland.
Baada ya kupiga kona moja ya uwanja kiatu chake cha kushoto kilitoka lakini hilo halikumzuia .
'' Ilikuwa kisirani .Lakini nilipata motisha ya kupigana zaidi ili niendelee vyema'', alisema baadaye.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.