Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Onana Sio Onea

...mara zote ni jambo zuri kukuona hapa anko wangu Lyon Lee pamoja na Makapuku wote ambao sio siri na wala siwezi kuchoka kusema kuwa mnalifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo. Unajua kuwepo kuna maana kubwa sana na kama ilivyo kwa Norway ambao hawana hata simba mmoja nchini kwao lakini kwenye bendera yao wameweka simba. Picha maana yake wanajiamini na pica huongea kuliko maneno.

Muziki sasa, siongei mengi maana humu ukimywa umetawala na si kosa kuwa kimya inawezekana ni hili zoezi la mkuu wa mkoa wa Tanzania, waliohitajika wamehudhuria na watuhumiwa wamejificha kusubiri wito wao utakuja lini.

 
Tafasiri Unavyoweza: Kipaumbele Kione Mbali Sio Mbele

Hivi unajua idadi ya watanzania wanaopata maji safi ya uhakika tangu tupate uhuru iko chini ya asilimia 60 (usiniulize chanzo cha takwimu hizi maana wakati mwingine kama wewe ni mtembezi huhitaji watu wa mjini wakuambia changamoto ya maji inatatuliwa kwa kasi). Na katika asilimia hii, 73 asilimia ya wanaopata maji ya uhakika iko mjini na iliyobaki iko vijijini ambako. Kwa taarifa yako tu ni kuwa asilimia 68 ya watanzania wanaishi vijijini kwa mujibu wa takwimu za WB. Kutokana na changamoto ya maji ya uhakika, suala la maji limekuwa ni sehemu muhimu ya ahadi za kampeni zisizotekelezwa na bado wananchi wanaendelea kuchagua chama kile kile na wabunge wale wale. tafasiri unavyoweza.

Kurahisisha tu ni kuwa serikali imeboresha zaidi huduma za simu na mitandao ya simu kuliko huduma za maji. Na kwa kuwa upatikanaji wa simu na huduma za mawasiliano ya mtandao ni rahisi suala la vipaumbele vya msingi haliangaliwi tena kwa sababu minara ya mawasiliano ni mingi kuliko visima vya maji ya uhakika kwa wananchi.

Tuna safari ndefu sana kama jamii na taifa kwa ujumla. Tutakaa kuambiana maendeleo hayana chama, dini na mamneno mengine ya kipuuzi lakini suala la kuwa na vipaumbele vinavyoangalia mbele na kusahau kuangalia mbali litatugharimu siku moja. Tafasiri unavyoweza.
 
Muziki: Ukimya Unaoaminika

...ukimya wa humu haujabadilisha imani yangu kwa wote mnaolipitia jukwaa hili na kulifanya kuwa sehemu nzuri kuwepo. Asante sana wewe unayenisoma muda huu, sitochoka kukwambia kuwa wewe u sehemu muhimu inayolifanya Jukwaa hili kusimama na kutokuwa jukwaa la msimu.

Muziki sasa, nisikuchoshe na maneno mengi hasa baada ya wiki kuwa tayari tumeigawanya kati na usiku ndo uunaishia.

 
-Obe
-shunie
-jimena
-afande shululu
-mama mchungaji blessedhope
-lionlee
-bitoz
-makaveli

Hamjambo nimewamis sana
 
Tafasiri Unavyoweza: Usinilaumu, Onesha Umefikaje Ulipo

Hakuna ubishi kuwa wapo baadhi wamejifanya na kujizoesha kuwa wavivu wa kila kitu, hawapendi kujishughulisha na chochote. Wanategemea mbeleko za kila namna (free riders) na hata mambo ambayo yako ndani ya uwezo wao kabisa kufanya hawafanyi. Hawa ni wachache sana katika wengi ambao kila kukicha wanajitahdi kupambana kuondokana na umaskini kwa kufanya kazi, kutia bidii katika yale halali wanayofanya. Hawa ndo msingi wa kipengele hiki cha leo, wanahitaji maelekezo na mbinu za kufanikiwa ulipo na wala huna haja ya kukaa unawalaumu kwa kushindwa kwao kufanikiwa.

Mafanikio yako leo usiyafanye kama mafanikio ya wazee wetu wa zamani ambao walipofariki basi na mafanikio yalipotea. Mafanikio endelevu hurithishwa na si uishie kutoa msaada tu wakati unatakiwa kutoa ndoano na kumfundisha mmoja namna ya kuvua samaki.

tumekuwa na tatizo la kuficha siri za mafanikio yetu tuliyonayo, nia na uthubutu wa mmoja hauwezi kufanikiwa kama hakuna waliotangulia kufika watamshika mkono na kumwelekeza namna sahihi ya kufikia walipo na kwenda mbele zaidi. Tafasiri unavyoweza inamaliza kwa kusema usiishie tu kulaumu mwingine wakati hujaweza kuonesha namna unavyoweza kuondoa lawama kwa unayemlaumu.
 
Muziki: Karibu Ijumaa

...yamebaki masaa machache tu iwe Ijumaa, siku nzuri ya mwanzo wa weekend na kwangu ni wiki ya kifamilia zaidi maana ninapata wasaa wa kukaa na waio karibu yangu ukiwemo wewe kapuku ambaye nachukua muda huu kukusalimia na kukutakia usiku mzuri. Asante kwa omarion5 kwa kuja sehemu yako ya kujidai.

Muziki sasa, burudika na bakulutu kinamna

 
Watu wako busy


.....kuna kitu kinaitwa sabbatical leave, haya ni mapumziko ambayo mtu hasa mfanyakazi au mwalimu wa chuo anachukua break fupi na baadaye atarudi.
mapuziko haya yanamruhusu kufanya mambo mengine nje ya kazi na ndo ukimya unaotamba humu kwa sasa

untitled-design-24.jpg
 
Tafasiri Unavyoweza: Ujinga Ni Kutosema

Najua kabisa naandika ikiwa ni mwanzo wa mapumziko ya mwisho wa wiki. Kawaida sana huwa sipendi kuandika mambo magumu na ya kufikirisha sana maana hata nami ninahitaji, kama ulivyo wewe, mapumziko ya kurudisha kilichopotea na nilichokosa kwa siku tano za kazi. Ninaandika magumu leo kwa sababu tu ya kuwepo kwa nia ya kufumba jamii mdomo, isiongee, isihoji na wala isiwe na maoni tofauti na wenye kukasimiwa madaraka. Taifa sio viongozi na kwa kuwa taifa letu tumeamua kuwaamini wachache kuongoza basi haimaanishi kuwa wao wanao uwezo wa kufikiria na kutuamulia wanachotaka wao binafsi au taasisi wanazoziongoza. Hii ni kwa sababu si wote wenye maslahi timamu kwa taifa, wengine ni kutaka kujineemesha wenyewe na tunaliona sana hili kwa sasa.

Bunge halifanyi kazi yake, linakutana kutegemea huruma za dola ambayo nayo inatoa masharti mengi tu ili bunge na mahakama ziendelee kuilamba miguu dola. Upo ushahidi wa maneno na vitendo vya wakuu wa taasisi hizi mbili wakijipendekeza vilivyo kwa taasisi dola ambayo kiongozi wake anatamani kuwa kila kitu, awe IGP, awe rais wa Znz awe kamishna wa kodi awe mkuu wa bandari, awe mpiga ngoma, awe 'stedishoo' na lolote unaloweza kutaja.

Bunge butu, bunge kibogoyo, bunge linalowafanya wabunge waingie na 'power bank' kwa sababu hakuna kinachojadiliwa cha maana na hivyo bora mbunge aendelee kucheza game au kutizama mitandao wakati wa mijadala ya bunge. Bunge linaloamua kupeleka taarifa yake ya uchunguzi kwa serikali bila kwanza kuijadili. Ukiwa unadhani ninaandika hisia basi jipe muda wa kufuatilia majukumu ya bunge na uangalie kinachofanyika sasa, tafasiri unavyoweza.

Bunge linaloongozwa na baadhi ya viongozi wanaowakilisha wapiga kura wajinga, ndiyo wapiga kura wajinga ambao hawajui thamani ya kura waliyoipiga, wanapiga kwa mazoea na hivyo kuendelea kuaminin wanachoambiwa na nambunge hata kama ni cha uongo ilmradi tu walikula wali nyama na kilo ya chumvi wakati wa kampeni za uchaguzi.

Ukikaa kimya bila kuongelea udhalimu na unyang'anyi unaofanywa na bunge hili la sasa usijedhani uko salama na ukaendelea kukenua meno kwa viongozi wasiotaka kusikia maoni mengine na hasa wasiyoyapenda. Hakuna mnafiki anayekufa mara mbili. Uwe na mapumziko mema.

Tukutane wiki lijalo.
 
Muziki: Tufurahi Pamoja Sikitika Peke Yako

Kuna mengi yanaendelea na mengine yanavutia machoni na masikioni ila mengine kama ilivyo kwa kila chenye sura basi hakikosi kisogo, mengine yanaumiza na kukarahisha lakini maisha ni lazima yaendelee. Haijalishi umekuwa na wiki ya namna gani, leo ni mwanzo wa mapumziko, weekend nami kama kwaida, nakusalimi na kukutakia mapumziko mazuri maana bila wewe kuwepo hapa, Jukwaa hili linabaki kuwa si sehemu nzuri kuwepo.

Muziki sasa, nimekuona mdau shululu kwa mbali, najua ukikamilisha unachofanya utakuja kulisongesha gurudumu letu hapa.

 
Back
Top Bottom