Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Karanga Zenye Michanga

Wiki inakwenda kasi sana, huwezi kuamini majuzi kuna wadau walikuwa wamefunga na sasa wamerudia maisha yao ya kawaida, yale maisha waliyoyazoea na kuwafanya wawe wao kama wao na si kuiga majina ya kwenye vitabu. Ninakusalimia Kapuku mwenzangu na kukuambia tu kuwa japo hujauliza siku yangu ilikuwa nzuri sana, asante kwa kutouliza. Ninajiaminisha ulikuwa na siku nzuri pia, karibu hata kama hujaniambia asante. Siwezi kuacha kukushukuru wewe kwa kuwepo hapa, unalifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri sana kuwepo.

Nilikuwa naongea na anko wangu Lyon Lee ambaye kwa sasa yupo mapumzikoni, hivi kuna wau wa ajabau kweli, yaani mtu anachukua likizo kipindi cha Aprili, kweli!!! Lakini nisiseme sana lakini ndo anko wangu kachukua likizo, ila kasema hataki kusafiri maana akisafiri tu mipango yake inachelewa. Hapa somo ni kuwa likizo japo inapendeza kusafiri hakuna ubaya usiposafiri, simu si zipo bhana.

Muziki sasa, nakusalimia Tumosa mama JJ na kukuambia unalifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo. Furahia muziki maana wote wanaosema kitumbua kikiingia mchanga hakiliki, hawajajaribu karanga


Kazi yako ni njema mtaasisi
 
Muziki: It is Almost Furahiday


U khali gani Kapuku tunayeheshimiana, mimi sijambo na ninakusalimia kukukumbusha tu kuwa kesho ni Ijumaa, yaani Furahiday na wakati huu unapokuwa umeshajirejesha nyumbani baada ya kazi nimeona ni vizuri kukukumbusha.

Ninawasalimia wadau wote ambao huwa mnakuwa na muda wa kutembela hapa.

Muziki sasa, nikutakie wakati mzuri na maandalizi mema ya Ijumaa

 
Muziki: It is Almost Furahiday


U khali gani Kapuku tunayeheshimiana, mimi sijambo na ninakusalimia kukukumbusha tu kuwa kesho ni Ijumaa, yaani Furahiday na wakati huu unapokuwa umeshajirejesha nyumbani baada ya kazi nimeona ni vizuri kukukumbusha.

Ninawasalimia wadau wote ambao huwa mnakuwa na muda wa kutembela hapa.

Muziki sasa, nikutakie wakati mzuri na maandalizi mema ya Ijumaa


Tuko pamoja mtaasisi
 
Muziki: Potea Njia

....ni wakati wa kwenda tu ndo unaweza kupotea njia lakini sio wakati wa kurudi. Ninakusalimia Kapuku mwenzangu na kukutakia wiki yenye mafanikio

Muziki sasa, burudika kufidia ukimya uliopo na unaotawala humu

 
Muziki: Potea Njia

....ni wakati wa kwenda tu ndo unaweza kupotea njia lakini sio wakati wa kurudi. Ninakusalimia Kapuku mwenzangu na kukutakia wiki yenye mafanikio

Muziki sasa, burudika kufidia ukimya uliopo na unaotawala humu

Binamu
 
Tafasiri Unavyoweza: Mkumbatie Simba Kwenye Picha

Zimepita siku kadhaa sijaandika kipengele hiki, kimahususikabisa ni siku mbili sijaandika kutokana na sababu zilizo ndani ya uwezo wangu. Tafasiri unavyoweza. kuna mengi yamepita katika siku hizi ambazo sikuandika, mengi unayajua na mengine huyajui maana ni ngumu kujua kila kitu hata kama utakuwa unakaa jirani na radio au luninga. Mimi nayajua machache na ndiyo maana kuja kwangu hapa ni njia mojawapo ya kuongeza ufahamu maana wewe unayenisoma una mchango mkubwa katika kuifanya akili yangu kuwa 'sharp', asante sana kwa busara unazoleta hapa Makapuku forum.

Ukweli usemwe, kumekuwa kimya humu, sana tu tangu wiki ya Pasaka na unaweza kujiuliza mengi, ni muda au majukumu yamezidi. Kuzidi kwa majukumu si jambo baya, kadri unavyokuwa kiumri na changamoto zinakuja kipekee. Huo ndo ukubwa, na ukiwa mkubwa ni lazima uwe na ngozi ngumu. Maana yake ngozi ngumu inavumilia na kuhimili changamoto za kila siku unazokumbana nazo katika maisha yako iwe ya kikazi, mapenzi, elimu na mahusiano au taja chochote maana unaruhusiwa kutafasiri unavyoweza.

Usije ukaona simba kanyeshewa ukadhani paka na ukataka kumkumbatia kumfuta maji, simba ni simba atakurarua hapendi kukumbatiwa, muache afanye yake kama haingilii njia zako za maisha na ikitokea akaingilia niia zako basi usisiste kumtoa njiani na kumpeleka panapomfaa. Tafasiri unavyoweza
 
Back
Top Bottom