Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tafasiri Unavyoweza: Nje Sawa, Ndani ya Box Unapajua?

Kama kumetokea msemo unaosikika sana katika miaka ya hivi karibuni ni huu unaosema fikiria nje ya box (Thinking outside the box). Huu ni msemo ambao ni maarufu sana katika nyanja za ujasiriamali. Ukihudhuria mafunzo ya wajasiriamli utausikia sana huu msemo. Ni msemo unaovutia kusikiliza na utashangaa unaambiwa kufikiria nje ya box wakati hakuna anayekuuliza ndani ya box ulilomo kuna nini. Tafasiri unavyoweza.

Labda nipunguze kuandika mengi, kufikiria nje ya box ni hali ya kuwa mbunifu, kutambua nguvu ulizonazo na madhaifu yako katika kutekeleza jambo mahsusi. Maana yake hapa ni kuwa huwezi kufikiri nje ya box kama hauko ndani ya box na kujua kilichomo ndani ya box ni kitu gani na ufanye nini kutatua changamoto za ndani ya box.

Ukishajua kilichomo ndani ya box, na si lazima mtu mwingine akwambie nini kilichomo ndani ya box unalilomo, unayajua yaliyomo yamo ndani ya box, ni jukumu lako kuyajua haya na si mtu mwingine ajitokeze na kukwambia ufikirie nje ya box. Ukishajua kilichomo ndani ya box sasa una haki ya kfikiri nje ya box na unawezaje kufikiri nje ya box, hili ndo suala sasa.
Unaweza kufanya mambo kadhaa ya msingi kama unataka kufikiri nje ya box, mfano, siku zote unanyoa toka juu kwenda chini, haya ni mazoea, hebu leo badili unaponyoa anzia chini kwenda juu, huku ndo kufikiria nje ya box. Tafuta maarifa na taarifa sahihi, fanya uthubutu na usidharau, tafuta ushauri kwa mtoto mdogo, wanajua ya kujua na anaweza kukwambia kitu ambacho hukutegemea. Jipe nafasi ya kuwa msafi, oga na vaa vizuri kila wakati.

Hivi unajua kuota ni moja ya njia nzuri ya kupanga mpango timamu! (Dreaming is a form of planning!!). Tafasiri unavyoweza.
[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji7]
 
Tafasiri Unavyoweza: Taswira Darajani

Kila mmoja wetu ana historia ambayo inapendeza wengine wakaijuana hasa watoto. Kwanini nasema hivi, najiaminisha kuwa wengi wetu humu tuna umri wa kitaifa na wengine tumeanza kukaribia kutoka kwenye umri wa kijana. Katika hatua zote hizi tumepitia mengi na tuna mengi ya kushirikisha wengine na hasa watoto wayafahamu, itawasaidia sana katika makuzi yao. Itawafanya wawe na maisha yanayofaa kwenye jamii. Kumbuka akili ya mtoto hukuzwa na wanaomzunguka na uwepo wako humu Jukwaani inaonesha kuwa wewe ni mtu makini, vinginevyo hata usingikuwa na ruhusa ya kuandika na kusoma unayopenda hapa. Tafasiri unavyoweza.

Taswira darajani inaega kukuonesha kuwa ni namna gani wewe unaweza kuwa chanzo cha mabadiliko kwa mtoto, ndiyo, pale utakapochukua kalamu na karatasi na kuamua kuandika kitu, iwe shairi, ngonjera, nyimbo au hadithi. Naandika haya nikijua kabisa kuandika si jambo rahisi na hasa kuandika tunzi zisomwe na watoto (crafting a children book is not easy, need creative skills into creating a successful story). Lakini, kwa maisha ambayo umeyapitia huwezi kushindwa kuandika kitu ambacho kitamsaidia mtoto wa Taifa hili.

Sisi ni walezi wa watoto kwa nafasi za majina yetu tofauti iwe baba, mama, mjomba, shangazi na jina lolote lile linalokufanya uwajibike kwa mtoto wa Tanzania, andika kitu, mfanye mtoto asome na itamjengea uwezo wa kufikiri na kuwa mdadisi (inquisitive) na hili ni afya kwa jamii na taifa letu. Tafasiri unavyoweza
 
Muziki: Ukikunja Ngumi Hufikiri Sawasawa


...kufikiri ni mchakato/ process na si jambo linalohitaji nguvu ya mwili zaidi (physique-tamka fiz-eek) bali utambuzi, nguvu ya kuchambua mambo na zaidi nguvu ya akili timamu. Ninakusalimia Kapuku mwenzangu na kukwambia tu it is almost Furahiday.

Siku nyingi sijaandika mengi hapa, naweka muziki tu na kuacha muziki uongee, si unamkumbuka Hamza Kalala na kile kibwagizo chake cha eee mamama tunakula miziki' ndo nilikuwa nafanya. Na huu ulikuwa ni ushauri wa anko wangu Lyon Lee ambaye kwa kweli amekuwa kwenye wakati mgumu sana kipindi hiki maana ukiacha safari zake za kanda ya kaskazini bado hata huku JF alikuwa akipambana na waandamanaji waliojipanga kimkakati kukaa wanamsifia aunt yangu.

Muziki, niseme tu Makapuku forum ni sehemu nzuri kuwepo na ukisoma kipenegele hiki utajijua wewe ni mtu muhimu namna gani humu Jukwaani.

 
Muziki: Ukikunja Ngumi Hufikiri Sawasawa


...kufikiri ni mchakato/ process na si jambo linalohitaji nguvu ya mwili zaidi (physique-tamka fiz-eek) bali utambuzi, nguvu ya kuchambua mambo na zaidi nguvu ya akili timamu. Ninakusalimia Kapuku mwenzangu na kukwambia tu it is almost Furahiday.

Siku nyingi sijaandika mengi hapa, naweka muziki tu na kuacha muziki uongee, si unamkumbuka Hamza Kalala na kile kibwagizo chake cha eee mamama tunakula miziki' ndo nilikuwa nafanya. Na huu ulikuwa ni ushauri wa anko wangu Lyon Lee ambaye kwa kweli amekuwa kwenye wakati mgumu sana kipindi hiki maana ukiacha safari zake za kanda ya kaskazini bado hata huku JF alikuwa akipambana na waandamanaji waliojipanga kimkakati kukaa wanamsifia aunt yangu.

Muziki, niseme tu Makapuku forum ni sehemu nzuri kuwepo na ukisoma kipenegele hiki utajijua wewe ni mtu muhimu namna gani humu Jukwaani.


Ahsante sana mtaasisi kwa kibao cha Loi toka kwa mkali wa zamani Olomide
 
Back
Top Bottom