Makapuku Forum

Shikamoo
 
Muziki: Kuna Tofauti


Asante sana Transcend kwa kunikumbusha kuweka muziki, ujue nini, tangu nimeanza kuandika Tafasiri Unavyoweza nimekuwa na wakati mgumu wa kuwa ndani ya wakati kutupia kipengele cha muziki. Anyway, hakijaharibika kitu na kwa kutoharibika huku ninakusalimia sana kapuku wewe unayetumia muda wako kuwa hapa na kulifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo. Asante Tumosa kwa kunisalimia.

Yeah, nilikuwa naongea na anko wangu huyu huyu Lyon Lee ambaye kwa kweli amekuwa na safari nyingi kuzidi safari lager yenyewe. Ila kila tukiongea kama kawaida yake haachi kunipa elimu ambayo nami kwa kupenda kushare knowledge siwezi kuacha kutowaambia. Kuna tofauti, ndivyo alivyoanza kusema, tofauti ya kuoga na kuogelea, tofauti ya huyu na yule, bure na bila malipo, kupendwa na kuachwa, bangi na bangili moja uikalie mbali kwani inakaa nawe miaka saba.

Muziki sasa, nakupenda sana wewe kapuku na sioni uchovu kukwambia hili kila wakati. Na kwa kutambua hili nakuacha na muziki huku ukitafakari tofauti zetu zinaztufanya kuwa wamoja


 
AsanteObe ubarikiwe usiku mwema
 
Ubarikiwe sana
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…