Makapuku Forum

KWA UNAYESIKIA UMEVUNJIKA MOYO,KWA USIKIAE KUWA NA MZIGO MZITO KWA MAPITO YAKO YALIYOSABABISHWA LABDA NA UNYANYASAJI FULANI,YAKABIDHI KWA MUNGU MKUU UPATE SULUHU LA KUDUMU;

YAKABIDHI HAYO KWA KRISTO YESU AKUSAIDIE;
Mathayo 11:28.
28 Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

MTAFUTE MUNGU,
Zaburi 34:4-5.
4 Nalimtafuta Bwana akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote.
5 Wakamwelekea macho wakatiwa nuru, Wala nyuso zao hazitaona haya.

MTWIKE YEYE FADHAA ZAKO ZOTE(YAKUSUMBUAYO);
1 Petro 5:7
7 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

MTEGEMEE MUNGU PEKEE(MUNGU WA AMANI);

Isaya 26:3-4.
3 Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemea Katika amani kamilifu, kwa kuwa anakutumaini.
4 Mtumainini Bwana siku zote Maana Bwana YEHOVA ni mwamba wa milele.

USIZITEGEMEE AKILI ZAKO;

Mithali 3:5-6.
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6 Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.

MTUMAINI MUNGU;
Zaburi 42:11.
11 Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.


UBARIKIWE,
Shalom.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…