Muziki: Wapi Noah Zetu
Kwanza hapa nina furaha sana maana ninaanza kwa kukusalimia Kapuku wewe mheshimika na kisha nakujulisha tu siku yangu ilikuwa nzuri, sijui wewe siku yako ilikuwaje lakini ile kukuona tu hapa basi najua kabisa uko poa.
Hivi mnakumbuka, sijui kama niliwaambia, baada ya anko kuninunulia simu aliitwa kimyakimya kwenye ile kamati ya makinikia na mnavyomjua anko tena badala ya kumanikia yeye akachikichia na CM. Nisikuchoshe, alichosema ni kuwa kila mmoja atapata Noah nami nikajichagulia kabisa rangi ya hudhurungi na nikaenda veta kusomea udereva na cheti nikapata nina C tatu. Sasa ninamtafuta anielekeze je Noah yangu nitaipataje?
Muziki sasa, juma la kicongo linaendelea. Mniwie radhi Niko busy natengeneza uwanja wa kupaki Noah yangu.