Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu Bwana Mungu wa Majeshi Asante kwa Upendo wako na kutuamsha tukiwa wazima na Afya njema,wapo watu wengi walitamani kuiona siku ya leo Baba hawajaweza ,tunatoa Sifa ,Shukurani,Heshima na Utukufu kwa Neema hii.

Tunakuja Mbele zako tukikukabidhi siku ya leo ya Jumatano 11 Oktoba 2017 ikawe njema na ya kukupendeza.
Tunaomba toba kwa yote tuliyokosea.
Tuimarishe ili tukupende,tukuheshimu na kuishi maisha ya kukupendeza wewe tu.
Tunaikabidhi Nchi yetu iwe na Amani.
Tunazikabidhi Familia zetu zidumishe Upendo na Mshikamano.
Tunawakabidhi wagonjwa na wenye shida mbalimbali majumbani na mahospitalini Baba ukawaponye miili na roho pia.
Baba wasafiri wote majini,nchi kavu,angani ukawe nao waende na kirudi salama.Na wanaoacha familia Baba mwema zikawe salama.
Watoto wetu popote walipo makazini na mashuleni ukawasimamie wakawe vichwa si mikia wafanye mambo yote kwa ufanisi.
Baba Mungu tunazikataa kazi zote za shetani zisipate nafasi katika maisha yetu tunazivunja katika jina la Yesu tunamwaga damu ya Yesu ikatakase kila pando na kuling'oa Mfalme wa Amani.
Tunakabidhi kazi zote za mikono yetu zikapate kibali mbele yako tuingiapo na kutoka utubariki.
Baba Asante kwa Matendo yako Makuu yasiyo na mwisho,tunauona ukuu wako siku zote za maisha yetu tunasema Asante Baba na tunaomba uzidi kutuimarisha imani zetu zipande kuwa viwango vya juu ili tuweze kushudia matendo yako siku hadi siku.Roho Mtakatifu tutie nguvu.
Nakushukuru maana utatenda yote sawa na mapenzi yako
Katika jina la Yesu naomba naamini na nashukuru Amen

SIKU NJEMA WAPENDWA
Amen
 
YESU ANAFAHAMU SHIDA YAKO LAKINI HAIONDOI MPAKA UMWAMBIE AKUSAIDIE*

Math 20:32 Yesu akasimama, akawaita, akasema, Mnataka niwafanyie nini?

33 Wakamwambia, Bwana, twataka macho yetu yafumbuliwe.

34 Yesu akawahurumia, akawagusa macho yao; mara wakapata kuona, wakamfuata.

Yesu hajawahi kumponya mtu asiyehitaji kuponywa
Unaweza ukabaki na shida ndani yako huku ukisema Mungu ananiona ni kweli anakuona lakini umemwambia kuwa akusaidie?
Nakwambia utabaki na shida yako maana Mungu hatakusaidia maana yeye anasikiliza Maombi mathayo 7:7-8
Mungu anataka uombe
Ukisoma mathayo 6:8 inasema kabla hujaomba tayari Mungu anajua shida yako

Kujua shida yako hakumfanyi Mungu akusaidie bali yeye anasikiliza Maombi yako

Ndiyo maana ukisoma unaona wale watu walikuwa vipofu tena walikuwa wanalia kwa sauti lakini Yesu bado aliwauliza mwataka niwafanyie nini?

Hebu jiulize inamaana Yesu alikuwa hawaoni kuwa ni vipofu?

Jibu aliwaona lakini alikuwa anasikiliza Maombi yao na haja ya mioyo yao


YESU ANAKUONA LAKINI HAKUGUSI MPAKA UOMBE

UBARIKIWE
 
13 Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?
1 Petro 3 :13

MBARIKIWE
5228930560209932e7a45ea27afcbac5.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom