Makapuku Forum

Makapuku Forum

JE' WAJUA..Kuwa lita 25 za [HASHTAG]#MAJI[/HASHTAG] hutumika kutengeneza lita moja tu ya [HASHTAG]#BIA[/HASHTAG]!?
cf0a8b9d856cebea8e8e365970691e2a.jpg
 
Majina ya watoto (vikembe) wa wanyama mbalimbali...

gombe......Ndama
Nzige...kimatu/maige/tunutu/matumatu/funutu
Ndege....Kinda
Kipepeo/nondo....kiwavi
Nzi......Buu
Farasi....Kitekli
Mamba...... Kigwena
Nyangumi..... Kinyangunya
Fisi.... Kikuto/bakaya
Ngamia..... Nirigi/nirihi
Paka.......kinyaunyau/kipusi
Ndovu.... Kidanga
Mbweha.... Nyamawa
Nyani...... Kigunge
Kondoo..... Kibebe/katama
Mbuzi.....Kibui/kibuli/kimeme
Farasi na punda.... Nyumbu
Punda.... Kiongwe/kihongwe
Mbu....kiluwiluwi
Chura.... kiluwiluwi
Kuku..... Kifaranga
Papa.... Kinengwe
Nyuki.... Jana
Simba..... Shibli
Sungura.....Kitungule
Kwanga/wibari.... " "
Samaki.... Chengo/kichengo
Chui.... Chongole/kisui
Mbwa..... Kilebu/kidue/kibwa
Nyoka...... Kinyemere
Njiwa..... Kipura
Wazazi wenye rangi tofauti.... Chotara/suriama
 
Saudi Arabia ni nchi kubwa sana duniani lakini haina mto hata mmoja wala maji yatiririkayo...
Maji ya kunywa huchujwa na kuondolewa chumvi toka baharini au chini ya ardhi.
 
Misri ndio nchi ambayo imekuwa na mamlaka (sovereignity) yake kwa muda mrefu zaidi kuliko nchi nyingine yoyote duniani.
Misri ilianza kuwa na utawala mwaka 3100 Kabla ya Kristo.
 
Msanii David Michangello alipoulizwa anawzaje kuchonga sanamu nzuri toka kwenye jiwe baya alijibu kuwa ...."Huwa ninaondoa tu sehemu ya jiwe isiyovutia"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom