Makapuku Forum

10/Chris Jericho
Alizaliwa Novemba 9 mwaka 1870
Huyu ni mcheza mieleka mweupe mfuga nywele filani hivi mwenye vituko ila nyumbani ni baba wa familia
Ameshastaafu mieleka sasa hivi kajikita kwenye kazi kibao za kisanii
Amewahi kushinda ubingwa wa dunia wa mchezo huo kwa kiwadunda wahenga kibao
Siku hizi ni mtunzi mcheza filamu na mwanamuziki
Kawahi kuvunjika mguu wakati akidensi wimbo wa Dancing With The Stars
Tayari ana albamu zaidi ya sita
Ana utajiri wa USD 19 Milioni
........
 
9/Big Show
Alizaliwa Februari 8 mwaka 1972
Huyu ni mzee wa show za kibabe kuanzia ulingoni hadi kitandani hivyo usije ukafikiri mwili wake mkubwa ni mzigo utaumia !!
Jina lake halisi ni Paul Randall Wight Jr jamaani jitu la miraba minne akiwa na urefu wa futi 7 na uzito wambao akikukalia utalalamika utafikiri umebebeshwa gunia la kokoto
Ni mcheza mieleka maarufu nchini Marekani na anautumia umaarufu wake vizuri kwa kuingiza mpunga kupitia mchezo huo na filamu
Kachukua mataji kibao WWE Ana utajiri wa USD 22 Milioni
.......
 
Kuna michezo mingine bana

Yani watu waliovaa vichupi wanagombea mkanda wakauvalie wapi?
(Natania ila wrestling me sio shabiki kabisa)

Madame S
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…