Katika kisiwa cha De Queimada Grande kilichopo nchini Brazil, ndipo anakopatikana nyoka pekee mwenye sumu kali zaidi duniani, Golden Lancehead Viper. Wataalamu wanasema sumu ya nyoka huyo ina nguvu karibu mara tano ya wengine wanaoishi ardhini. Nyoka hawa hupata chakula chao kwa kuwala ndege wanaokwenda kisiwani hapo kufanya mapumziko. Serikali ya Brazili imepiga marufuku watu kutembelea kisiwa hicho, isipokuwa kwa kibali maalum.
USHIRIKIANO: Rais Magufuli akutana na kufanya mazungumzo na tajiri namba moja duniani, Bill Gates alipomtembelea Ikulu, jijini Dar Es Salaam.
Bill Gates yuko nchini katika ziara ya kukagua miradi ambayo taasisi yake ya Bill and Melinda inasaidia ukiwemo wa kupambana na magonjwa yasiyopewa kipaumbele....