Makapuku Forum

TOP TEN
Leo nilibanwa pia sikupanga kuandika kitu
Hivyo napost marudio kwa faida ya ambao hawakuwepo siku husika zen nacheki game la Man Utd

Juzijuzi kuna mwanamke alizua gumzo barani Afrika kutokana na kuwa na watoto 38 wakati ana umri wa miaka 37 tu yaani anafyatua fastafasta kuwazidi hata panya!
Sasa leo tuwaone wengine wenye watoto wengi hapa tunazungumzia zaidi wanawake au ndoa za mume na mke mmoja ila kuna usemi

Mama pekee ndiye ajuaye baba halisi wa mtoto
Km kawa wazungu maana waafrika hatuna utamaduni wa kutunza kumbukumbu wala kujitangaza kwenye mitandao hivyo inawezekana huko Musoma wapo wengi tu

Karibuni
...........
 
Eeeka mbee mangyi
 
10/Mary & John Jonas Nimeitafuta picha ya familia yao sijaipata zaidi ya vielelezo tu
Hawa wakiishi miaka ya 1800 huko
Walibahatika kupata Watoto 33 ikiwemo pea 15 za mapacha wa kike na kiume
Baadhi walifariki utotoni huku wengine wakifikia uzeeni
Watoto 10 walikuwa hai wakati dingi wao akifariki mwaka 1892
Mary alifariki mwaka 1899
......
 
8/Elizabeth & Thomas Greenhill Huyu ni mtoto wao wa mwisho aitwaye Thomas Hii mayo ni familia ya karne ya 17 huko
Ilikuwa na watoto 39
Wakiume 7 na wakike 32
Huku mapacha wakipatikana mara 1 pekee

...........
 
7/Alice Hookes Siyo picha yake halisi
Mtoto wake wa mwisho (41) alifariki mnamo mwaka 1637
Huyu mama alikiwa ni binti wa Kiwales aliyezalishwa na wanaume tofauti

Alifyatua watoto 41

..........
 
6/Elizabeth &John Mott Mzee John Mott Binti yake
Elizabeth na John walioana mwaka 1676 na kujaaliwa kupata watoto 42
Elizabeth alifariki mwaka 1720

...........
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…