Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Ukiitwa Itika Hata Kama Huji

Kesho ni Ijumaaa, TG! Nimeamua nikujulishe tu kapuku mheshimika maana wengine kalenda hamna na mnategemea kalenda za simu, siku ikiisha chaji huioni siku wala kujua uko kwenye siku ya hatari au vipi. Kuna zile kalenda za kuweka ukutana, ndiyo, wall calendar zile za klabu ya Simba, zinapendeza sana ndani. Ninakusalimia sasa baada ya kuwa nimekukumbusha kununua kalenda na kwa kuwa mwaka tushaugawa kati, zimepungua bei.

Unataka niseme ni juu yako kapuku mheshimika shedede , shululu ,lee empire , Shunie ,husna muba , Tumosa Nyagei , Mondray , demi , Mkushi wa kusi , mzeewakungoa , Mndali ndanyelakakomu ,Madame S ,Bitoz , Bailly5 ,dumejeuri ,dingimtoto ,Clkey ,Sakayo , Transcend , BlessedHope ,QUIGLEY , Jimena , koncho77 ,werrason na wengine wengi ambao uwepo wenu humu hulifanya jukwaa hili kuwa special. Not only that you guys are awesome, you are exceptional and you know it. Asanteni sana, nimewaita tu na hakuna nilichowaitia maana usawa huu ishieni kusema asante maana mnanifanya nipapende hapa.

Muziki sasa, ukiachana na sisi wazee wa bakulutu, mwanamuziki solo ambaye anajulikana maeneno mengi Tanzania basi Komandoo Jide anaweza kuwa anajulikana zaidi. Lady JayDee ana sauti nzuri jamani, ile inayosemwaga inamtoa nyoka pangoni haifikii maana nyoka wengine wanakaa mtini ukipita tu anakugonga. Utafurahi kumuona akiperform na bendi yake live.

Asante husna muba kwa chaguo hili.

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom