Makapuku Forum

Makapuku Forum

Sehemu ya 29



Alivuta taswira na kukumbuka kamishna Shebby kuwa mtu pekee wa kwanza kumuonesha thamani kubwa ndani ya jela. Aliamini hakuna na hatotokea mpaka mtu kama yeye mapaka siku atayoingia kaburini. Sheby alikuwa kijana wa ajabu sana kwake. Alijiuliza vipi leo hii afe kabla yake!? Aliumia sana Hussein na kumlilia Kamishna Shaaban kama mtoto wake wa kumzaa.
Hadi kunakucha Hussein alibaki kasimama palepale mlangoni. Alishindwa kabisa kulala na kusogea popote zaidi ya kububujikwa machozi yaliyobeba kumbukumbu nyingi za huzuni na hasira kuhusu MR.X Usiku huo aliomba mambo mengi sana huku jambo kubwa alitamani sana Mungu amfanyie muujiza ili amuue Mr. X kwa mkono wake mwenyewe. Aliamini kama atafanikiwa hilo basi hata kifo chake atakifurahia kuliko kufa akamuacha mr. X duniani akizidi kuwamaliza watu wasio na hatia wataotaka kuufichua ukweli ambao aliamini chanzo cha yote ni mkewe yule aliyekuwa binti mrembo kutoka Arusha.
*****
|MCHEZO wa MR X|
================
"Mr. X ni kivuli cha jina la mtu mmoja hatari sana mwenye mbinu ngumu za haraka na mitego yenye sumu isiyoonekana hata kwa darubini kali. Hakutumia sana nguvu katika kuuficha ukweli juu ya siri kuwa yeye ni nani? Na laiti angetumia nguvu sana basi serikali ni kubwa na ina nguvu sana hivyo muda mrefu angeshajulikana na kukamatwa. Lakini tofauti yeye anatanguliza akili nyingi na nguvu kidogo zinafuata nyuma. Akili anayoitumia imebeba maarifa mengi na ya ajabu. Jinsi ya kupigana na mr X ili umshinde inabidi ujiingize kwenye akili zake na umzunguke. Tega mabomu ya akili zako kwenye akili zake ili siku utapoyalipua atakosa akili mpya. Na hapo ndipo utamkamata kiurahisi zaidi.
Pia Mr X ana mtandao mkubwa sana wa watu wanaomfanyia kazi waliogawanyika katika makundi mawili.
Kundi la kwanza ni wale wanaojijua kuwa wanafanya kazi katika mtandao wa mr X. Na kundi la pili ni la wale wasiojijua kama wanafanya kazi katika mtandao wa mr. X.
Kwa weledi na utaalam wa akili za mr X ameweza kuyatengeneza makundi hayo na kuyaweka sehemu moja bila upande wowote kubaini chochote. Na pia ameweza kuwafanya wote wanaomfanyia kazi wasijue mr. X mwenyewe ni nani hasa. Pia hakuna ofisi yoyote aliyojenga mr X ambayo ingeweza kuwakutanisha watu wake. Mtu pekee aliyejua ukweli wote kuhusu yeye alikuwa mmoja tu. Mtu ambaye anajua siri zote pia ni rahisi sana kwako kufika alipo. Lakini ni vigumu tena vigumu sano kumjua mtu mwenyewe. Na hii yote ni kwa sababu mr X anawachezesha mchezo. Mchezo wenye akili nyingi kuliko michezo yote unayoijua au uliyowahi kuisikia.
Mchezo ambao hauna mashabiki na inabidi uucheze bila pupa na kwa akili nyingi. Mr X ndiye mwenye mchezo huu. Mchezo ambao humuingiza yeyote atakaye kumtafuta na kumjua yeye ni nani. Sasa nawe umejiingiza kwenye mchezo pasipo na mr. X kutaraji wala kuhitaji. Lakini kwa kuwa umetaka mwenyewe basi inabidi ujiandae kuucheza huu mchezo kwani ushakuwa mchezaji mpya na umepewa namba....! Jibu lako liko wazi sana Shebby. Amka sasa usilale unakaribishwa kwenye MCHEZO wa MR X.
Amka Shebby amkaaa sasa ujiandae kwa lile zoezi uliloambiwa ili umshinde Mr X kwenye mchezo huu. Amka muda ndio huu anza sasa kujifunza zoezi hili..
Amkaaaa Shebiiiiiii... Amkaaaa Ukikamate kivuli Chakooo!"
...............................
Alistuka kwenye usingizi mzito Shebby mara baada ya kuisikia sauti ya ajabu kichwani mwake. Aliachama kinywa ili apige kelele lakini alijikuta anashindwa baada ya taya kukaza kinywa. Alitamani kugeuza mwili lakini alishindwa pia. Alipotaka kujinyanyua ndio kabisa mawasiliano yote yalikosekana. Nguvu zilimtupa mkono ganzi ilimshika mwili. Alipotulia ndipo aligundua kumbe alikuwa amefungwa kwenye kitanda maalum ambacho bado hajajua kilikuwa wapi.
"Pumzika tu Mkuu, upo salama sasa tunarudi nyumbani." Sauti ilisikika ya kijana mmoja mweupe aliyevaa gwanda maalum nyeusi huku begani mwake kukiwa na alama ya bendera ya Tanzania. Kamishna Shebby japo alishindwa kuzungumza lakini alipomtupia jicho aligundua kijana yule ni wa kikosi maalum cha jeshi la polisi wanaotumwa kwa shughuli maalum. Hapo akili yake ilizidi kutuama akabaini zaidi kuwa walikuwa ndani ya helkopta na muda huo wapo angani. Maumivu makali alianza kuyasikia hususani upande wa mguu wake wa kushoto. Kumbukumbu zake zikamrudishia taswira ya kilichotokea kabla na kukumbuka kuwa alipigwa risasi ya mguu.
Nyuso za wenzake walivyokuwa wanauawa kinyama zilimuumiza hasa alipomkumbuka Sajent Kimaro machozi yalizidi kumtoka na uchungu kumuingia moyoni. Alijiapiza moyoni mwake endapo akipona lazima amtafute Mr. X kwa udi na uvumba pia yule mwanamke aliyewaua wenzake lazima nae aje kumuua kinyama tena kwa mkono wake. Alijiweka tayari nafsini kuucheza huo mchezo na kuupata ushindi kwa njia yoyote ile.
* * *
Helkopta ilifika jijini Dar na kutua kwenye hospitali maalum ya kulipia aliyoamrisha mzee Mwinchande. Hadi muda huo tayari mzee Mwinchande na mkuu msaidizi wa gereza wakiwa na baadhi ya askari wakubwa walikuwa wanasubiri kwa majonzi kumuona Kamishna Shebby na kuushuhudia mwili wa sajent Kimaro ambao nao ulikuwamo kwenye ile helkopta. Kila kiongozi wa jeshi la polisi na askari wote walipopata habari ile walishangazwa na kujiuliza sana nini kiliwakuta huko porini Mkuyuni na kwanini kamishna kaenda kufanya kazi ambayo hakupaswa kabisa wala haikumuhusu. Kwanza cheo chake kilikuwa kikubwa hakupaswa kuhangaika kwa kuwa alikuwa na uwezo wa kuwatuma askari wengi waliokuwa chini yake. Lakini tofauti na makamishna wngine, Shebby siku zote hakupenda ukubwa wala kutumia cheo chake kama fimbo kwa wengine. Baada ya vitanda viwili kushushwa kwenye helkopta haraka vilikokotwa na askari kuwahishwa ndani ya hospitali sambamba na madaktari. Kitanda kimoja ambacho kilifunikwa kabisa kuashilia aliyelala mule hakuwa mwenye uhai, kiliwaliza askari waliokuwa pale ambao walimjua Kimaro. Kile kitanda cha pili kilichoachwa wazi sehemu za juu ulionekana uso wa Kamishna Shebby ukiwa una alama na michilizi mingi ya damu. Moja kwa moja aliingizwa kwa daktari mkuu.
"Eeeh Mungu baba, mponye mwanangu naomba kikombe hiki kimuepuka aaah!" Aliomba kwa simanzi na uchungu mzee Mwinchande huku machozi yakimtoka baada ya kuona hali ya mwanae na kutoamini kama kweli bado mzima.
Shebby aliishia kulia pasi na kusema kitu huku akijilaumu tena kichwani kwanini hajawahi kumshirikisha baba yake japo kwa ushauri tu juu ya mpango aliokuwa nao hadi akaenda kujiongoza bila kufata ushauri wa watu wazoefu kama babaye ambaye alidumu kazini kwa zaidi ya miaka 30.
Alifumba macho baada ya kitanda kutolewa kwa daktari alipomchunguza haraka na kuingizwa kwenye chumba cha upasuaji haraka. Huko kulikuwa na daktari maalum wa kujitegemea ambaye alikuwa bingwa wa mifupa na alikuwa pale kwa ajili ya kumtibu Shebby tu. Daktari huyu bingwa aliaminika sana baada ya kusomea taaluma ile ya utabibu tokea angali na miaka kumi huko nchini India alipochukuliwa na wafadhili waliomlea miaka yote hiyo. Kwenye moja ya mahojiano miaka ya nyuma aliwahi kusema aliipenda kazi ya utabibu toka angali mtoto. Dakatari huyu wa kike alikuwa bingwa wa mifupa na mishipa na alidhihirisha kipawa chake angali bado yuko India na hata aliporudi Tanzania nchi ilijivunia ingawa serikali ilishindwa kumuajiri kutokana na kiasi kikubwa alichopaswa kulipwa. Ikabaki kuwa anakodiwa kwa kazi maalum tu na kulipwa pesa nyingi sana kwa kazi moja ambayo aliifanya kwa uhakika wa hali ya juu. Japo alionekana bado binti mdogo tofauti na madaktari wengi kuonekana na umri mkubwa lakini anapokuwa katika kazi zake hugeuka kuwa mkubwa sana kutokana na ufanisi wake. Ilikuwa vigumu mno akiwa nje ya ofisi kum'baini kama binti yule alikuwa daktari. Uzuri wa kipekee wa sura na umbo unemfanya ashinde hata mashindano ya ulimwende bila kupingwa kama angehitaji. Binti aliye chini ya miaka 28 alitabaruku mbele ya kitanda alicholazwa kamishna Shebby tayari kumfanyia upasuaji.
Jina lake liliandikwa kwenye kitambulisho kilichokuwa kinaning'inia shingoni mwake. DK ASHA ndivyo jina lilivyosomeka kitambulishoni. Kazi ile kwake ilikuwa ndogo sana ingawa mguu wa Shebby ulifumka vibaya eneo la goti.
"Pole sana kaka ila usiogope utakuwa sawa tu na utatembea kama zamani." Alimfariji kwa sauti ya haiba ya kike wakati akiandaa vitu vyake sawa tayari kuanza kumshughulikia Shebby. Moja kwa moja aliupachika mguu wa shebby kwenye mashine maalum mara baada ya kumchoma sindano nne za paja zilizoua mawasiliano yote ambayo yangeweza kumletea maumivu Shebby. Aliifanya kazi yake kwa uhuru na umakini bila Shebby kuhisi chochote. Mwanadada alianza kucheza na nyama za Shebby huku akipekechua mifupa kwa umakini upasuaji ukachukua nafasi.
-..............
 
Uf....
c72646e0ec0f85cc09438b75e2c6c494.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom