Muziki: Jumamosi Fleva
Ni jumamosi usiku sasa, lakini kama ilivyokuwa koloni la Malkia Liz, unaweza kuta ni saa sababu mchana sehemu fulani na wote tunaungana hapa KF kuburudika.
Usidanganywe na utando wa juu wa uji ukauparamia, juu umepoa ila ndani ni wa moto pasi mfano. Hii ndo hali ya leo humu KF, asanteni sana kwa mlioamua kupumzika. Mapumziko yenu tunayapenda na kipengele cha muziki kipo kuwaburudisha
Leo ni siku ya miziki ya kisasa zaidi na ni jambo zuri kwamba Makapuku Forum ni sehemu bora kabisa kuwa na hasa kwa kuwa wewe unayesoma segement hii u sehemu yake. Najua unajijua kuwa u mtu maalum kabisa pasi mfano si wale moja haikai mbili haiingii.
Kuna kolabo zinavutia kutazama wakiimba maana wote wanajua na utawafurahia. Sikiza kolabo hii ya komandoo pekee wa Tanzania ambaye huwa hakaribishwi sherehe za muungano kupasua matofari, yeah, Lady JayDee mkali mwenye sauti ya iliyopangika Kisababto na itakuvutia. Hapa anaungana Kidumu, unataka niongee nini kuhusu Kidumu. Tizama