Manchester United wamekubaliana ada ya uhamisho ya takriban pauni milioni 75 na Everton ya kumsajili mshambuliaji Romelu Lukaku, 24.
Taarifa zinasema United sasa hawatoendelea kumfuatilia Alvaro Morata wa Real Madrid.
Hatua hii pia haihusiani na mazungumzo ya Wayne Rooney kuhamia Everton.
Manchester United wametoa dau la pauni milioni 66 kutaka kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, 24, na huenda makubaliano kati ya timu hizo mbili yakafikiwa katika saa chache zijazo (Marca).
Bahati mbaya Madrid wakaweka ngumu kwa kutangaza dau....
Manchester United wangependa kumsajili kiungo wa Borussia Dortmund Julian Weigl baada ya kushindwa kuwapata Eric Dier kutoka Tottenham na Nemanja Matic kutoka Chelsea (Daily Mail)
Atletico Madrid wanajiandaa kutoa dau rasmi la pauni milioni 22 kutaka kumsajili Diego Costa, 28, kutoka Chelsea limeandika (Guardian).
Ila mirror limeripoti kuwa
Hatua ya Atletico Madrid kutaka kumsajili tena Diego Costa itategemea kama wataruhusiwa kumpeleka China kwa mkopo hadi adhabu yao ya usajili itakapomalizika mwezi Januari (Mirror).
Chelsea wamefikia makubaliano na Roma ya kumsajili beki Antonio Rudiger, 24 kwa pauni milioni 34, ingawa mchezaji huyo bado hajafikia makubaliano rasmi kuhusu maslahi binafsi (Sky Sports).
Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28, anataka mshahara wa pauni 400,000 kwa wiki, ambao ni ongezeko la pauni 125,000 kwa wiki katika mshahara wake wa sasa (Daily Mirror).
Kiungo wa Chelsea Nathaniel Chalobah, 22, anazungumza na Watford kutaka kuhamia katika timu hiyo aliyoichezea kwa mkopo msimu wa 2012-13 (Daily Mirror).