Makapuku Forum

10/Vietnam War
Ilikuwa vita kati ya Vietnam Kusini na Kaskazini
Vita ilianza Nov 01 1955 baada ya Marekani kuanza kutosa sapoti ya kijeshi kwa Vietnam Kusini ambao walikuwa wakipambana dhidi ya Ukomunisti na Kaskazini
Urusi na China nao wakasapoti Vietnam Kaskazini na vita ikawa kali na kupiganwa hadi 1975
Rais wa USA alikuwa ni John F Kennedy ambaye baadaye aliuawa na kurithiwa na Lyndon B Johnson ambaye aliendeleza gurudumu la vita
Mwisho wa siku April 30 1975 Vietnam Kusini na USA wakashindwa vita na hivyo Vietnam Kaskazini kuimegaKusini na kuunda The Socialist Republic of Vietnam
Vita iligharimu maisha ya watu Milioni 2.4
Ilidumu kwa miaka 19
.........
 
9/The Great Northern War Hii ilikuwa ni vita baina ya Urusi chini ya Peter The Creat dhidi ya Swedish Empire chini ya Charles XII hapohapo pembeni walikuwepo Denmark,Poland,Uingereza,Norway na Ottoman Empire
Watu 300,000 walipoteza maisha
Ilipigwa kati ya mwaka 1700 hadi 1721
Urusi enzi hizo Russian Empire alishinda vita na hatimaye kuwa Taifa/dola lenye nguvu duniani
Vita ilichukua miaka 21
........
 
8/First Punic War
Hii ilikuwa ni moja kati ya mfululizo Wa vita tatu za kibabe huko Kaskazini mwa Afrika kati ya Carthage(Tunisia) na Roman Republic kugombea njia(route) za kibiashara katika bahari ya Mediterrania....mwanzoni mwa vita ya Punic ilikuwa ni kugombea kisiwa cha Sicily
Waroma walishinda vita na pia kupora tembo zaidi ya 100 wa Wacarthage(Tunisia)
Watu zaidi ya 20,000 walipoteza maisha
Ilipiganwa kwa miaka 23 (264--241BC)
.....
 
7/The Achinese War
Hii ilitokana na Wadachi kusimika utawala wao huko Dutch East Indies ambayo ilikuwa ni koloni lao(Indonesia)
Vita ilianza mwaka 1873 baada ya Wadachi kumshambulia Sultan wa Aceh ambayo ilikuwa ni himaya yake huru huko Indonesia kaatika kisiwa cha Sumatra
Wadachi walishinda vita.....Leo hii Aceh ni jimbo la Indonesia
Watu 90,000 walipoteza maisha
Vita ilidumu miaka 31 /(1873--1904)
........
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…