Makapi ya CCM yanapokuwa ngano kwa CHADEMA

Duh! mkuu wangu umeogopa kuwa mmoja wa wendawazimu au?

Psychiatrists wanatuambia characteristic moja common ya wendawazimu ni kujiona wao wako sawa na ulimwengu mzima pembeni yao ulio tofauti nao umejaa wendawazimu, kwa hiyo ogopa sana mtu anayerusharusha hili neno "wendawazimu" kirahisi rahisi.
 
Psychiatrists wanatuambia characteristic moja common ya wendawazimu ni kujiona wao wako sawa na ulimwengu mzima pembeni yao ulio tofauti nao umejaa wendawazimu, kwa hiyo ogopa sana mtu anayerusharusha hili neno "wendawazimu" kirahisi rahisi.
Ndio sawa na kusema hao Ma Psychiatrists, wengi wao ni wendawazimu wenyewe..
 
Tukubali tu kwamba ni kawaida Siasa kujaa makapi. siyo CCM wala CHADEMA. Tatizo la CCM ni kutaka tuone kwamba wao brain imejaa. Ni majigambo ya siasa lakini kama ni kupima utendaji, CHADEMA na CUF Brain imejaa.

Binafsi nakubali kwamba hata wana-CUF toka Z'bar wako juu ya wenzao wa CCM toka huko Z'bar kwa jinsi nilivyowaona miaka yote Bungeni.


Hao wachache wa CHADEMA bado wametuonyesha mengi kuliko hao walioachwa CCM waendelee.

Lakini huyu tunayemwita Rais naye naona hana hakika na. Leo nimemsikia akionyesha wasi wasi wake wakati anarudisha fomu ya maombi ya kazi. Naona kama jeuri inaanza kupungua.

Kasema kwa yale waliyoyafanya ana imani watashinda, watachaguliwa kwa wingi wa kura. Wakati huo huo akasema inabidi tukazane kueleza yale tuliyoyafanya, kazi siyo rahisi. Hapo nikaamini hata yeye hana hakika kama wananchi wanayaona hayo asemayo wameyafanya na pia ana wasiwasi wa ushindi.
 
Hayo hayo makapi yenu safari hii yanawamaliza... hakuna kulala mpaka kieleweke....kwanza kuitoa CCM halafu kuchuja makapi. Swali la kizushi: Kama ni makapi mbona mnayaogopa?

Huwezi kusema mtu ni kapi wakati umemfukuza kwa roho mbaya yako tu yaani hayuko kwenye system fulani ya ndani ya CCM, ilhali kura ya maoni inaonyesha anatakiwa. Ndio maana hayo makapi yanahama na wafuasi lukuki.

Safari hii mmekwisha kila mbinu imedhibitiwa sasa mnahaha! Welcome ''makapi''..Hameni wote waacheni wenye CCM yao.
 
Tatizo lenu mnataka a simplistic approach, CCM mafisadi, kwa hiyo yeyote anayetaka kuitoa CCM rafiki yetu, yeyote anayekuwa critical kwa yeyote anayetaka kuitoa CCM ni adui yetu na rafiki wa CCM.

Hamuwezi kujiuliza kwamba hata katika vita hii ya kupigana na ufisadi kuna mafisadi wanachukua nafasi na kujifanya ni wapinzani, na kama mtakubali kila kitu bila kuuuliza mtajikuta mnamtoa fisadi mmoja na kumuweka fisadi mwingine.

Kuwa critical ni lazima, kama tunakuwa critical kwa CCM, kwa nini tusiwe critical kwa CHADEMA ?

Kiranga;

Mwanasiasa yeyote yule duniani ni opportunist na chama anachokimbilia kinampokea kwa kuamini kuwa kufika kwae kutawaongezea nafasi ndani ya Bunge na baadae ufanisi wa chama chao;sio tu CHADEMA ambao ni wa kwanza kuchukua watu ambao ama walikosa nafasi kwenye vyama vyao vya awali!

Yaliyotokea UK mwaka 2005 wakati mwanasiasa nguli na Mbunge wa Labour Party Charles Kenedy alipokihama ghafla chama hicho na kujiunga na Liberal Democracy au Frolida kwa Gavana Chris au Colorado kwa Mzee Tancredo au hata Penslavyania kwa mkongwe Arlen Specter ni ushahidi wa wazi kabisa kuwa hata kwenye nchi zilizopiga sana hatua kwenye mageuzi ya siasa kuhama vyama bila kuchunguzwa na hatimaye kupokelewa huko unakoenda ni jambo la kawaida kabisa!

Slaa alitoka wapi kama ni lzm tumchunguze aliyehamia CHADEMA?Tunaangalia opportunities kama ataweza kushinda ili kupunguza nguvu za CCM ndani ya Bunge na wala sio sababu zingine zaidi ya hii!
 
Hayo hayo makapi yenu safari hii yanawamaliza... hakuna kulala mpaka kieleweke....kwanza kuitoa CCM halafu kuchuja makapi. Swali la kizushi: Kama ni makapi mbona mnayaogopa?

Huwezi kusema mtu ni kapi wakati umemfukuza kwa roho mbaya yako tu yaani hayuko kwenye system fulani ya ndani ya CCM, ilhali kura ya maoni inaonyesha anatakiwa. Ndio maana hayo makapi yanahama na wafuasi lukuki.

Safari hii mmekwisha kila mbinu imedhibitiwa sasa mnahaha! Welcome ''makapi''..Hameni wote waacheni wenye CCM yao.

Mkuu mwenzangu Wa Mjengoni;

Mgombea kama Thomas Nyimbo wa jimbo mojawapo la Njombe,au Hussein Bashe wa Nzega au hata Mzee Ramole wa Moshi-Mjini hawa wote waliongoza kwenye kura za maoni ndani ya CCM lkn kamati kuu ya CCM ikawaona hawana sifa kwa vigezo wanavyovijua wenyewe na kupuuza kabisa kura za wana CCM wa majimbo yao waliyowapa ridhaa ya kuwa wagombea wao;kam wagombea kama hao niliowataja juu wakija CHADEMA basi tuwape miaka 5 ya kuwachunguza?!

Kiranga na wenzako hamjaeleweka na sidhani kama mtaeleweka;tufafanulieni iweje aliyeongoza kura za maoni CCM akija CHADEMA tumchunguze wakati kuja kwake ni nafasi ya wazi ya CHADEMA kuongoza kiti bungeni?
 
Kuhama vyama ni hali ya kawaida, uchaguzi wa Marekani uliopita mgombea wa Democtrat Leberman aliama na kujiunga na Repablica na kugombea huko, hivyo si kitu cha kushangaza.

Kwa taarifa zako zaidi ya asilimia 90 ya viongozi wa vyama vya upinzani walitoka ccm. Kwa hiyo CHADEMA kuwapokea ni kuhimarisha democrasia nchini. Pia maeneo walipopewa nafasi ni yale maeneo ambako CHADEMA na vyama vingine hawakuwa na wagombea makini, hivyo watapeperusha bendera yao na kukuza chama kujulikana zaidi kwa wananchi, kama walivyofanya akina Dr. Slaa.
 
Kuhama si dhambi; hapa tunaangalia umakini wa mtu.

Dr.Slaa mwenyewe alitemwa na CCM akaenda CHADEMA akashinda ubunge; na umahili wake tumeuona.Marehemu rais wa Marekani Ronald Regan alitemwa kugombea urais na chama chake cha Democrat akaenda chama pinzani Republican akashinda akawa rais wa Marekani.

Hivyo kuchaguliwa kwa haki kunatoka kwa wapiga kura na si viongozi wa juu wa CCM! Mbona hata CCM inakumbatia watu wanaotoka vyama vingine? Nsanzugwako, Mtemvu, Dr.Limbu kutaja wachache wote hawa walikuwa vyama vya upinzani wakiitukana CCM kwelikweli lakini walipohamia CCM walipokelewa na kupata uongozi je? wao hawakuwa makapi ya upnzani! Hapa tuangalie ukombozi wa nchi yetu; ni nani wakututoa katika lindi hili la umasikini na kutuletea maendeleo ya kweli, bila kujali kama walikuwa CCM au la.

"MUNGU IBARIKI TANZANIA"
 
Mkuu mwenzangu Wa Mjengoni;

Mgombea kama Thomas Nyimbo wa jimbo mojawapo la Njombe,au Hussein Bashe wa Nzega au hata Mzee Ramole wa Moshi-Mjini hawa wote waliongoza kwenye kura za maoni ndani ya CCM lkn kamati kuu ya CCM ikawaona hawana sifa kwa vigezo wanavyovijua wenyewe na kupuuza kabisa kura za wana CCM wa majimbo yao waliyowapa ridhaa ya kuwa wagombea wao;kam wagombea kama hao niliowataja juu wakija CHADEMA basi tuwape miaka 5 ya kuwachunguza?!

Kiranga na wenzako hamjaeleweka na sidhani kama mtaeleweka;tufafanulieni iweje aliyeongoza kura za maoni CCM akija CHADEMA tumchunguze wakati kuja kwake ni nafasi ya wazi ya CHADEMA kuongoza kiti bungeni?

Huyu inabidi achunguzwe kama anakuja CHADEMA kwa moyo kwamba kakubali sera za CHADEMA au anakuja CHADEMA kwa sababu anataka ubunge tu na hana jinsi ila kukubali chama chochote promising ili mradi apate ubunge tu.

Ukiangalia sana hapa utagundua kuna tofauti kati ya watu wanaoamini katika sera za vyama na wanaoamini katika personalities, watu wanaoamini katika sera za vyama kama mimi watataka kuhakikisha kwamba hawa wagombea kweli wanajikita katika sera za vyama, hili litaweza kuhakikishwa na muda tu.

Kwa wale wanaoangalia personalities bila kujali sera za vyama hivi, of course unaweza kutangaza kuhama CCM asubuhi na jioni ukatangazwa mgombea ubune wa CHADEMA.

Tatizo linakuja kama mtu anakuja katika chama bila kuwa na mapenzi ya sera, kesho akishaingia mjengoni anaweza kurudi kwao CCM kisiasa akawa ana vote nao CCM, na kuwapa ramani ya vita, kwa hiyo CHADEMA wanaweza kujiona wanajua kumbe wakawa wanaungua na jua.
 
Mara nyingine nafikiri hatujielewi kama watu na mazingira yetu. Malafyale kaleta mifano ya kina Tekero wa Kolorado na Kristi na hata Spekta, hawa wako Marekani ambapo vyama hivi vikubwa viwili, vimejijenga kwa zaidi ya miaka 150 na vyote vinafahamika misimamo na itikadi zao kitu ambacho ni tofauti na Tanzania ambako CCM ina miaka 60+ huku kina CHADEMA na CUF ni bado wachanga.

Siasa za Afrika paoja na kuwa tunataka kuleta mfumo wa kidemokrasia kama ule wa Marekani, Uongereza hata Japan, ni bado zina mfomo kandamizi wa kikomunisti unaojiita ujamaa na tamaduni za asili za Kiafrika ambazo mara nyingine ni sawa na roho kutu (kumbukeni vagi kati ya Shaka na kaka zake).

Nilipoandika suala la Mizoga au mkipenda Pumba, Makapi, Ghalasa, Mabua au Makombo, ni kutokana na kuuelewa mfumo wetu wa Siasa na ni jinsi gani vyama vya Upinzani vimekuwa vikionewa na CCM kwa ujumla miaka nenda rudi a hakuna hata mwanachama mmoja wa CCM aliyediriki kusimama na kukikana Chama chake au kuzikana mbinu na tabia chafu za chama chake katika si kudhalilisha tuu, bali ni hata kuhujumu na kuonea si vyama vya upinzani pekee bali hata Wananchi wa Tanzania kwa kisa cha kulinda na kutumikia maslahi ya CCM na kutimiza wajibu wa mwanachama wa CCM kwa mujibu wa ibara ya 15.1

Swali nililoliuliza wiki iliyopita nitaliuliza tena leo, je hawa mamluki na wakimbizi, leo hi ndio wamekula iman na yamini na kuona CHADEMA ni chama mbadala? Au CUF au TLP?

Iweje leo hii wakurupuke kama kundi la kongoni au mbogo wakakimbilia wote na kuhamia CHADEMA, CUF, TLP, NCCR, DP na kwingineko baada ya wao kukataliwa ulua wao ndai ya chama chao CCM?

Je walikuwa hawajiamini tangu awali na wakahamia huku walikokukimbiia sasa?

Kama tutadai kuwa wanakubalika sana majimboni na wananchi, kwa nini basi huku wakijua kuwa CCM kumeoza na uchafu wake umeota mizizi, hawakufanya ridhaa kwa wamamchi na kuhamia vyama vingine kama wanajiamini wanapendwa na wananchi?

Ni kukurupuka huku kwa shangwe za ulevi wa ulanzi kuwa tumepata mateka ambako kunaweza vyama vya upinzani kupumbaa na kujiamini kupita kiasi ilhali kumbe hawa nia yao si Tanzania bali ni matumbo yao na ni mamluki waliotumwa rasmi kuja kudhoofisha vyama hivi ili 2015, CCM iangushe Tsunami nyingine!

Wanasemaga wazungu "better safe than sorry" Slaa is one in million, but Kabouru, Lamwai, Tambwe and others are many in tens!
 
Kuhama vyama ni hali ya kawaida, uchaguzi wa Marekani uliopita mgombea wa Democtrat Leberman aliama na kujiunga na Repablica na kugombea huko, hivyo si kitu cha kushangaza.
Kwa taarifa zako zaidi ya asilimia 90 ya viongozi wa vyama vya upinzani walitoka ccm. Kwa hiyo CHADEMA kuwapokea ni kuhimarisha democrasia nchini. Pia maeneo walipopewa nafasi ni yale maeneo ambako CHADEMA na vyama vingine hawakuwa na wagombea makini, hivyo watapeperusha bendera yao na kukuza chama kujulikana zaidi kwa wananchi, kama walivyofanya akina Dr. Slaa.

And 20 years later they are not anywhere near to be united or redeem Tanzania from CCM, they are disorganized and uninspiring. Mostly they have been chaos and no wonder no one makes progress and they are all running back to shower CCM with praises.
 
Nilimsikia Mnyika DW akisema kuna 'wana scrutiny system' naamini inafanya kazi vizuri.

Pili makapi yanafaida sana tu - mfano kapi la ngano unaweza kulishia mifugo ambayo kama ni ng'ombe utapata nyama nzuri au maziwa safi!

Cha msingi ni kujua namna ya kulitumia hilo kapi! Au kapi hilo ni kulitumia kama mashine tu! Wayatumie makapi hayo kama "loud speaker (wasiseme ya kwao ila ya Chadema!)", "farasi", "failure ya CCM".
 
Ninashangaa sana jinsi ambavyo CHADEMA inapoteza umakini wake. Swala la members wa CCM kuhamia CHADEMA linachukuliwa kirahisi sana lakini halipaswi kuchukuliwa hivyo. Taarifa zisizo rasmi ni kuwa kuna mamluki lukuki wametumwa kuibomoa CHADEMA, wengine wameshawapokea na kuwakubali kuwa wagombea wa ubunge na udiwani. Time will tell. Washinde wasishinde lengo lao ni moja tu "kuhakikisha CHADEMA sio tishio tena kwa CCM kwa gharama yeyote".

Ni lazima CHADEMA wakubali kuwa ili kuleta mabadiliko ya kweli ni lazima kuwaandaa wanachama wao muda mrefu ili kuongoza sio chama tu bali dola pia. Sio mtu anakurupushwa huko akiwa na ngeu, anahema na amekunjwa suruali, kisha anawatupia kadi ya CCM wakati hamkumpa nyie, na kumkabidhi kadi ya chama bila ya yeye kujua hata sera ya CHADEMA inasema je. Kisha kesho yake mnampa barua inayoonesha kuwa ndie mgombea wa CHADEMA. This is nonsense kwa chama makini na chenye nia ya kuleta mabadiliko ya kweli.

Sikatai kuhusu uzalendo wa baadhi ya waliohamia CHADEMA, na wala sitathubutu kuuhoji, ila ninahoji ukosefu wa subira. Mambo mazuri huivishwa kwa moto wa muda. Naogopa pale CHADEMA itakapogeuka ccmb, kama ambavyo TLP ya Mrema imegeuka.

Kwa ushauri wangu CHADEMA wawekeze zaidi kwenye wanachama vijana, wawape mafunzo ya Uzalendo, Uadilifu, Ubunifu na hali ya kuthubutu. Itachukua muda mrefu lakini itakuwa na matokeo ya kudumu na ya muda mrefu yenye kukijenga chama na Taifa kwa ujumla.

I love my country & i respect patriotism & intergrity.

Ngugu yangu,
Shurti(sio sharti) uelwew kuwa siasa in tactics zake...kuwapokea hawa Watanzania ni jambo la muhimu katika kujijenga...hivi unajua 1994 millions of makaburu walijiunga na ANC na Mandela aliwaambia wenziwe waacheni wajiunge?unjua kuwa uhasama wao ulikuwa mbaya kiasi gani?....nadhani unajua.

Inawezekana kweli mtu anakurupushwa huko akiwa na ngeu, anahema na amekunjwa suruali halafu awe ametumwa kweli? Labda sijakuelewa....

Kama utaangalia vizuri wanaopewa haki nya kugombea ni wale wa maeneo ambayo CHADEMA yenyewe imejihakiki na kuona kuwa haina candidate mahiri kwa hivyo wanampa nafasi huyo mhamiaji siadahi kama mgombea CCM aliyeshindwa na akahamia CHADEMA Karatu angepewa nafasi ya kugombea.....
 
Shoo gap,
Nimeupenda sana mtazamo wako - Makapi ya sisiemu yanapokuwa ngano kwa chadema.

Ni kweli kabisa kwa mswahili, mswahili ngano ni ile ilikwisha kuwa processed na unga wake mweupe ndio bora na chakula, pasipo kufahamu kwamba ni Makapi ya ngano ndio yenye high in fible na nutrition zaidi ya huo unga mweupe.

Pili, ikiwa hawa wanaopokelewa ni makapi ya ngano, ni ubora gani wa hiyo ngano ilobakia CCM umeutazama kama sii kwa ubora wa kutengeneza chakula ulokizoea?...yaani Chapati na Mandazi!. ina maana unazungumzia kitu kilichokuwa bora kulingana na ufinyu wa ubunifu wa chakula bora kiasi kwamba unayaona makapi hayawezi kupika Chapati wala mandazi.

Well Chadema wanakuiletea mapishi ya kitu kinaitwa - Cereals.. Ni ngano yote inatumika hakitupwi kitu.
Wadhungu wanasema A brand natural of whole grain wheat with high fiber.... Ushindi ni Lazima

Umenikumbusha bro, kumbe makapi ndiyo hayo hutengeneza hivi vitavyoitwa virutubisho, ambavyo wajanja wa GNLD na wengineo ndo wanaviuza kwa bei ghali sana kwa wale waliopungukiwa navyo, pamoja na wale wanaohitaji kuboresha mifupa na misuli yao!

[hii haina maana kuwa nashabikia CHADEMA kukumbatia CHADEMA kukumbatia hao jamaa though, matumizi ya maneno hapa yanahitaji kuangaliwa upya I think]
 
...........Ukiangalia sana hapa utagundua kuna tofauti kati ya watu wanaoamini katika sera za vyama na wanaoamini katika personalities, watu wanaoamini katika sera za vyama kama mimi watataka kuhakikisha kwamba hawa wagombea kweli wanajikita katika sera za vyama, hili litaweza kuhakikishwa na muda tu.

Kwa wale wanaoangalia personalities bila kujali sera za vyama hivi, of course unaweza kutangaza kuhama CCM asubuhi na jioni ukatangazwa mgombea ubune wa CHADEMA.

Tatizo linakuja kama mtu anakuja katika chama bila kuwa na mapenzi ya sera, kesho akishaingia mjengoni anaweza kurudi kwao CCM kisiasa akawa ana vote nao CCM, na kuwapa ramani ya vita, kwa hiyo CHADEMA wanaweza kujiona wanajua kumbe wakawa wanaungua na jua.

Hili jambo la uaminifu wa sera nimekuwa siliamini kabisa! Hivi kweli nchi hizi zetu tuna sera tunazozifuata? Tunaziandika lakini hatuzifuati.

Hawa CCM kweli wana sera? Tunapomwangalia huyo aitwaye JK matendo yake kweli ni mfuasi wa sera za CCM? Na hao akina Lowasa na Rostam wanafuata sera ipi?

Huku kuhama na hasa kutoka CCM kuja vyama vya upinzani kunanipa tumaini kubwa sana maana kitendo hicho tu ni moja ya matukio ya kisiasa kuwapa wananchi confidence kwamba kumbe siyo kosa kutoka CCM.

Kumbuka tulikotoka ambako hata mwananchi wa kawaida anafungiwa kibanda chake cha biashara kwa sababu tu ya kujiunga na upinzani. Hii ndo imewafanya CCM kulitawala Bunge. Wengi bado tunaogopa kuingia upinzani kwa kuogopa hata kuondolewa ktk utumishi wa serikali. Na kweli wanafanya hivyo.

Kwa CHADEMA hii ni bahati kwao maana wanapokea majina yaliyokwisha sikika. Tuache propaganda za CCM, eti sera, sera, sera, nambari wani,.....nk.
 
tafsiri ya makapi ni pana sana. Ukipembua mchele yale mapumba yanayotupwa ambayo huwa ni kiasi kidogo na kubaki mchele mwingi hii ni tafsiri moja. Pia ukichukua udongo na kupembua dhahabu ambayo ni kidogo na kutupa udongo ambao ni mwingi hapa makapi ni huu udongo.

Hawa watu wanaohama ccm ni dhahabu, hawakutumia rushwa ndio maana hawakupata kuteuliwa ccm. Ukitaka ubunge kupitia ccm ni lazima uwe tajiri (yaani uwe na hela nyingi za takrima). Kama huna hutapata haijarishi wewe ni malechela au ntagazwa.

jafar - indeed you are a great thinker!!!!! Fully support you what you have quoted above!!!!
 
Wote wana haki na pia CCM na mfumo wao ndio wanafanya watu kuwa hivyo ila CHADEMA ni chama makini
 
Back
Top Bottom