Makapi ya CCM yanapokuwa ngano kwa CHADEMA

Nimekuwa nikisema more or less the same thing hapa, wanaotoka CCM sasa hivi waangaliwe mpaka at least 2015, kama wameonekana kwamba wamefuata kazi ya chama -na sio kutafuta ubunge kwa sababu wameshindwa kura za maoni CCM - ndipo wapewe nafasi hizi.

Vinginevyo CHADEMA itakuwa inaalika chaos.

Hii ni kweli. Kwa sasa muamko wa vijana na watu wengi kutafuta ubunge au udiwani si kwa nia ya kulikomboa taifa bali ni kwa nia ya kutafuta ajira yenye umaarufu na hela za haraka. Hivyo wanapokosa CCM hukimbilia chadema kwa kuwa wanasema ccm imewaonea kumbe sivyo hawa wanatafuta ajira kwa sababu wengi ni wataalam wa kupiga domo na siyo kufanya kazi. Katika hali ya sasa ya kushindana soko la ajira vijana wengi wavivu na wasiokuwa na CV nzuri hukuimbilia siasa kwani huko hata la saba anaweza kupata uwaziri.
Na ieleweke kuwa vijana wadogo ambao hawajafanya hata kazi au miradi fulani kukimbilia siasa ni janga la taifa. Si kwamba wana akili sana bali ni wazuri kuongea hadharani tu kama kina zito na wenzake ambao hupewa taarifa na watu au makampuni kuja kuongea bungeni kwa nguvu ambazo at the end hatuoni matunda yake.
 
Nimekuwa nikisema more or less the same thing hapa, wanaotoka CCM sasa hivi waangaliwe mpaka at least 2015, kama wameonekana kwamba wamefuata kazi ya chama -na sio kutafuta ubunge kwa
sababu wameshindwa kura za maoni CCM - ndipo wapewe nafasi hizi.

Mimi nitakuwa na mawazo tofauti kidogo,tukiliangalia suala hili kwa sura moja tayari hapa tumejenga double standard.Historia kubwa ya viongozi wa Chadema inaundwa na wale waliokimbia kutoka vyama vingine kama CCM (Dr.Slaa, Mpendazoe na Ntagazwa),CUF(Prof. Safari),NCCR (Prof. Baregu na Marando),TLP (Lema) na katika mazingira hayo hayo ya kushindwa uchaguzi hasa Slaa na Safari.

Tunawatambuaje hawa kwamba huyu ni Slaa oooooh Mzuri huyu na huyu ni Sumaye aaaah,ataleta shida!Hii ni double standard, na tambueni katika siasa ni ''unafiki'' tu ndio umetamalaki kwa maana ya watu kujivisha ngozi ya kondoo.

Chadema kama Chama kinakuwa na changamoto sasa ni nyingi kupita za awali.Hoja ya waliokifia chama kuwa hawana vyeo na hawa wanaokuja wanapata vyeo haina political sound.Mind product ya nje mara nyingi inakuja na mtaji kwa maana ya wafuasi tofauti na alie ndani, wafuasi hawa upenda kumuona yule alieondoka nao ananafasi pia ndani ya chama hii ndiyo changamoto.

CCM huwa hawana tabia ya kugawa vyeo haraka.Tazama kamati kuu yao haina Mamluki wa vyama vingine kama yupo i stand to be corrected.Tazama kamati kuu ya Chadema,sehemu kubwa imejaa Mamluki toka vyama vingine ambao nimetaja hapo juu.Sasa jeuri ya kuwazuia wengine eti ni makapi aaaah inatoka wapi?nani wa kuthubutu na kwa hoja gani?Labda Zitto na Mbowe!Lakini sio Slaa,Safari, Lema, Marando wala Baregu kwani wote hawa walikuwa makapi kwenye vyama vyao na leo ni ngano CDM.
 
Kwenye hizi game za kisiasa, to the best of my knowledge, zinafanana na ule msemo kuwa kwenye msafara wa mamba kenge nao wamo! Nil kama kokolo, linalokusanya kila kitu; samaki, dagaa, vyura n.k! It follows that wanaohama CCM wanahama kwa mengi, kuna wanaotumwa kama mamluki, na kuna wanaotoka kwa kwa kuona mfumo wa rushwa uliokithiri ndani ya chama hicho hautawawezesha kuwa viongozi hata kama wana sifa kwa kuwa hawana fedha! Lakini all in all, huku wanakokuja, wamluki na waukweli watajulikana; si mnajua kuwa watatambulika kwa matendo yao. CDM ni chama makini kinachoweza kumjua bila shaka na yule wa ukweli...!
 
Ninashangaa sana jinsi ambavyo CHADEMA inapoteza umakini wake. Swala la members wa CCM kuhamia CHADEMA linachukuliwa kirahisi sana lakini halipaswi kuchukuliwa hivyo. Taarifa zisizo rasmi ni kuwa kuna mamluki lukuki wametumwa kuibomoa CHADEMA, wengine wameshawapokea na kuwakubali kuwa wagombea wa ubunge na udiwani. Time will tell. Washinde wasishinde lengo lao ni moja tu "kuhakikisha CHADEMA sio tishio tena kwa CCM kwa gharama yeyote".

Ni lazima CHADEMA wakubali kuwa ili kuleta mabadiliko ya kweli ni lazima kuwaandaa wanachama wao muda mrefu ili kuongoza sio chama tu bali dola pia. Sio mtu anakurupushwa huko akiwa na ngeu, anahema na amekunjwa suruali, kisha anawatupia kadi ya CCM wakati hamkumpa nyie, na kumkabidhi kadi ya chama bila ya yeye kujua hata sera ya CHADEMA inasema je. Kisha kesho yake mnampa barua inayoonesha kuwa ndie mgombea wa CHADEMA. This is nonsense kwa chama makini na chenye nia ya kuleta mabadiliko ya kweli.

Sikatai kuhusu uzalendo wa baadhi ya waliohamia CHADEMA, na wala sitathubutu kuuhoji, ila ninahoji ukosefu wa subira. Mambo mazuri huivishwa kwa moto wa muda. Naogopa pale CHADEMA itakapogeuka ccmb, kama ambavyo TLP ya Mrema imegeuka.

Kwa ushauri wangu CHADEMA wawekeze zaidi kwenye wanachama vijana, wawape mafunzo ya Uzalendo, Uadilifu, Ubunifu na hali ya kuthubutu. Itachukua muda mrefu lakini itakuwa na matokeo ya kudumu na ya muda mrefu yenye kukijenga chama na Taifa kwa ujumla.

I love my country & i respect patriotism & intergrity.

ni watanzania wachache wasiozijua sera za chadema!
 
Hadi sasa cdm imechelewa. Makapi waliingia kwa wingi 2010. CDM iyajue makapi yafuatayo yakiongozwa na Zitto Kabwe; halima mdee, kasulumbai, ester, sugu, wenje, vicent. Hawa wako mtandao mmoja unaomsupport Zitto kugombea urais. Hawa pia hawakubaliani na ukandamizaji unaofanywa na Mbowe na Slaa. Wanaamini utawala wa vijana ndani ya chama. Amini usiamini hawa ndiyo wasaliti ndani ya CDM na kwamba wameamua kuimaliza CDM kwa kutoa siri zake kwa CCM. Slaa alishahojiwa na wakuu wa usalama kuhusu tuhuma za kuandaa mafia huko Italy ili kuendesha mauaji kwa malengo ya kisiasa. Slaa alikana mwanzoni lakini alivyooneshwa nyaraka za kiuhamiaji na picha za video zilizonaswa Italy, zikimwonesha Slaa akifanya mazungumzo na Master of Italy Mafioso, alikiri. Anayedaiwa kuvujisha siri hizo kwa wanausalama kupitia Halima Mdee ni Askofu mmoja(jina kapuni) jijini Mwanza ambaye haelewani na Slaa. Askofu huyo alihamishiwa Mwanza kuisaidia ccm kurejesha jiji mikononi mwake. Alipofika mwanza alimtumia wenje kutoa kauli za kuchukiza kwa machinga na baadae kuligawa baraza la madiwani na kisha kumshauri vibaya Dr Slaa kuwafukuza madiwani. Slaa aziangalie sana movement za watajwa ni hatari kupita maelezo.
 
Nimekuwa nikisema more or less the same thing hapa, wanaotoka CCM sasa hivi waangaliwe mpaka at least 2015, kama wameonekana kwamba wamefuata kazi ya chama -na sio kutafuta ubunge kwa sababu wameshindwa kura za maoni CCM - ndipo wapewe nafasi hizi.

Vinginevyo CHADEMA itakuwa inaalika chaos.

Mimi nina mawazo tofauti juu ya hoja hii. Wanaojiunga na vyama vya siasa vyote hapa nchini ni watanzania. Wote wana kiu ya kuona mabadiliko katika mfumo wa maisha yao ya kila siku. N a majibu ya mabadiliko yako katika vyama vya siasa. Leo mtu akipoteza matumaini kupata mabadiliko kupitia CCM aende popota anapoona kuna mwelekeo huo na mchango wake usibezwe. Cha kujihadhari pengine ni kuwathamini zaidi wahamiaji kuliko waliokuwepo hasa katika uchaguzi. Pia si busara kumpa mtu uongozi kwa kigezo cha huyu ni mwenzetu! Uwezo wa mtu uangaliwe! Hivyo kwa kutumia vigezo vilivyowekwa na chama wawachuje kuona uwezzo wao katika kukitumikia chama
 
Anyway sijui mtazamo wa mleta hoja..lakini nachoamini ni kuwa makapi hupitia mchakato au chujio na ni mchakato huo ndio huwa unaleta makapi hayo, ubora wa mchakato hufanya hata ubora wa makapi uwe katika hali bora, na mchakato mzuri utafanya makapi yakose sifa kabisa ya kuwa na kitu muhimu ambacho kimebaki, lakini mchakato mbaya hufanya ubora wa makapi nao kuwa wa hatihati, makapi yatakayobaki na vitu ambavyo vilitakiwa kukamulia au kuondolewa, hayo sio makapi ila yakiingizwa kwenye mchakato kwenye mashine ambayo inafanya kazi kwa ubora bado yanaweza kutoa kitu ambacho kinaweza kuwa na tija.....kwa hiyo uamuzi wa kuyatumia au kutoyatumia unabaki kwa ridhaa ya muongoza mchakato. kama amejiridhisha kuwa hali ya makapi haina hasara kwake, basi hiyo haimaanisha kuwa makapi hayo yakitumiwa na mtu mwingine na kuwa na tija hiyo italeta hasara kwa alieongoza mchakato wa kwanza....
lakini cha msingi zaidi je yaliyoitwa makapi ni makapi kweli, ana alichoamini kuwa ni material je ni kweli ni material?..manake inaweza kuwa umesema umetoa makapi na kubaki material kumbe umetoa material na kubakiza makapi....logic yangu nature ya mchakato inaweza kubainisha ubora wa makapi..ili makapi yawe na sifa ya umakapi usio na thamani inategemeana na chujio au mchakato.....kwa hiyo kitendo cha watu au kikundi flani kugombea makapi kama yanavyoitwa inaweza kuwa ni sahihi kama tu chujio lilipitisha malighafi na huku mwenye chujio akijua kuwa kilichotoka ni makapi.....kwa hiyo hakili kumkichwa, je haya ni makapi kweli au malighafi?..na je hata kama ni malighafi je yanapaswa kutumika kutengenezea bidhaa hii mpya yenye jina tofauti ingawa mwilini ina kazi sawa?....pia hapa aliekota makapi nae anapaswa kuwa makini kuangalia ubora wa makapi......
 
Mimi nina mawazo tofauti juu ya hoja hii. Wanaojiunga na vyama vya siasa vyote hapa nchini ni watanzania. Wote wana kiu ya kuona mabadiliko katika mfumo wa maisha yao ya kila siku. N a majibu ya mabadiliko yako katika vyama vya siasa. Leo mtu akipoteza matumaini kupata mabadiliko kupitia CCM aende popota anapoona kuna mwelekeo huo na mchango wake usibezwe. Cha kujihadhari pengine ni kuwathamini zaidi wahamiaji kuliko waliokuwepo hasa katika uchaguzi. Pia si busara kumpa mtu uongozi kwa kigezo cha huyu ni mwenzetu! Uwezo wa mtu uangaliwe! Hivyo kwa kutumia vigezo vilivyowekwa na chama wawachuje kuona uwezzo wao katika kukitumikia chama

Unachanganya mambo mawili tofauti.

Moja ni haki ya kila Mtanzania kupata nafasi ya kugombea uongozi (ambalo jibu lake ni kuruhusu wagombea binafsi) na la pili ni haki ya vyama kuhakikisha wagombea wake wanaelewa itikadi za vyama hivyo na hawajaingia vyamani kwa tamaa ya uongozi tu.

Kama unataka haki ya Mtanzania kugombea uongozi isiminywe, tetea ugombea binafsi.

Mtu yeyote anayeheshimu itikadi ya chama atajua kwamba huwezi kupewa uongozi kihalali katika chama cha watu wenye akili kwa kujiunga tu.

Hata kwa hao Wakatoliki au Waislamu wenye wingi wa rehema za kidini huwezi kupewa u kardinali au u mufti mara baada ya kujiunga tu na dini. Utapewa katekisimu kwanza ujue dini, utapewa madrasa etc, ukikomaa unapandishwa ngazi kwa ngazi.

The only reason tunaona haya mambo ya mtu kujiunga chamani wiki hii na wiki ya kesho anagombea uongozi ni kwa sababu siasa zetu, kama ninavyo lament kila siku hapa, zinaangalia majina ya watu binafsi na sio itikadi za vyama.

Ndiyo maana unaona mtu kama Shibuda analeta fujo sana CHADEMA. Kwa sababu anaamini kashinda uchaguzi kama Shibuda na sio kama mwanachama wa CHADEMA, na hata kesho CHADEMA wakimmwaga akienda CUF ana jeuri ya kushinda ubunge. Na CHADEMA kwa kuendekeza uchu wa viti vya ubunge wakamkubali chapchap bila kuangalia matatizo atakayowaletea mbele ya safari.
 
Ninashangaa sana jinsi ambavyo CHADEMA inapoteza umakini wake. Swala la members wa CCM kuhamia CHADEMA linachukuliwa kirahisi sana lakini halipaswi kuchukuliwa hivyo. Taarifa zisizo rasmi ni kuwa kuna mamluki lukuki wametumwa kuibomoa CHADEMA, wengine wameshawapokea na kuwakubali kuwa wagombea wa ubunge na udiwani. Time will tell. Washinde wasishinde lengo lao ni moja tu "kuhakikisha CHADEMA sio tishio tena kwa CCM kwa gharama yeyote".

Ni lazima CHADEMA wakubali kuwa ili kuleta mabadiliko ya kweli ni lazima kuwaandaa wanachama wao muda mrefu ili kuongoza sio chama tu bali dola pia. Sio mtu anakurupushwa huko akiwa na ngeu, anahema na amekunjwa suruali, kisha anawatupia kadi ya CCM wakati hamkumpa nyie, na kumkabidhi kadi ya chama bila ya yeye kujua hata sera ya CHADEMA inasema je. Kisha kesho yake mnampa barua inayoonesha kuwa ndie mgombea wa CHADEMA. This is nonsense kwa chama makini na chenye nia ya kuleta mabadiliko ya kweli.

Sikatai kuhusu uzalendo wa baadhi ya waliohamia CHADEMA, na wala sitathubutu kuuhoji, ila ninahoji ukosefu wa subira. Mambo mazuri huivishwa kwa moto wa muda. Naogopa pale CHADEMA itakapogeuka ccmb, kama ambavyo TLP ya Mrema imegeuka.

Kwa ushauri wangu CHADEMA wawekeze zaidi kwenye wanachama vijana, wawape mafunzo ya Uzalendo, Uadilifu, Ubunifu na hali ya kuthubutu. Itachukua muda mrefu lakini itakuwa na matokeo ya kudumu na ya muda mrefu yenye kukijenga chama na Taifa kwa ujumla.

I love my country & i respect patriotism & intergrity.

Ninavyoelewa ni kwamba CDM ndio wanaoset agenda CCM .NI wewe ututhibitishie kuwa wanachukua makapi na si wanaacha makapi.
 
Nimekuwa nikisema more or less the same thing hapa, wanaotoka CCM sasa hivi waangaliwe mpaka at least 2015, kama wameonekana kwamba wamefuata kazi ya chama -na sio kutafuta ubunge kwa
sababu wameshindwa kura za maoni CCM - ndipo wapewe nafasi hizi.

Mimi nitakuwa na mawazo tofauti kidogo,tukiliangalia suala hili kwa sura moja tayari hapa tumejenga double standard.Historia kubwa ya viongozi wa Chadema inaundwa na wale waliokimbia kutoka vyama vingine kama CCM (Dr.Slaa, Mpendazoe na Ntagazwa),CUF(Prof. Safari),NCCR (Prof. Baregu na Marando),TLP (Lema) na katika mazingira hayo hayo ya kushindwa uchaguzi hasa Slaa na Safari.

Tunawatambuaje hawa kwamba huyu ni Slaa oooooh Mzuri huyu na huyu ni Sumaye aaaah,ataleta shida!Hii ni double standard, na tambueni katika siasa ni ''unafiki'' tu ndio umetamalaki kwa maana ya watu kujivisha ngozi ya kondoo.

Chadema kama Chama kinakuwa na changamoto sasa ni nyingi kupita za awali.Hoja ya waliokifia chama kuwa hawana vyeo na hawa wanaokuja wanapata vyeo haina political sound.Mind product ya nje mara nyingi inakuja na mtaji kwa maana ya wafuasi tofauti na alie ndani, wafuasi hawa upenda kumuona yule alieondoka nao ananafasi pia ndani ya chama hii ndiyo changamoto.

CCM huwa hawana tabia ya kugawa vyeo haraka.Tazama kamati kuu yao haina Mamluki wa vyama vingine kama yupo i stand to be corrected.Tazama kamati kuu ya Chadema,sehemu kubwa imejaa Mamluki toka vyama vingine ambao nimetaja hapo juu.Sasa jeuri ya kuwazuia wengine eti ni makapi aaaah inatoka wapi?nani wa kuthubutu na kwa hoja gani?Labda Zitto na Mbowe!Lakini sio Slaa,Safari, Lema, Marando wala Baregu kwani wote hawa walikuwa makapi kwenye vyama vyao na leo ni ngano CDM.

Ni kweli Slaa alitoka CCM. Katika nchi iliyokuwa ya chama kimoja, karibu kila mtu aliyekuwa katika siasa alitoka CCM.

Kuna tofauti kati ya mtu kama Slaa ambae alitoka CCM zamani, akaenda CHADEMA wakati CHADEMA haina hata chart, akahusika sana katika kuijenga CHADEMA, na mtu kama Shibuda au Sumaye (anavyosemwa) anayekuja kuingia CHADEMA wakati imeshajijenga kisiasa tayari.

Dr. Slaa anaweza kusema mimi nikipewa uongozi CHADEMA sasa hivi nina deserve hilo, kwa sababu nimeanzia mbali wakati chama kina struggle sana, enzi hizo NCCR na CUF vilikuwa vinasikika kuliko CHADEMA. Nikakijenga chama kwa kushirikiana na waasisi kimefika hapa kilipo.

Mtu kama Shibuda alipokuja CHADEMA na kupewa nafasi ya kugombea ubunge, achilia mbali kuweza kusema kakijenga chama, hakuweza hata kusema kwamba anazielewa itikadi za CHADEMA kiundani kama mwanachama vizuri.

Tofauti hii ni kubwa. Zaidi ya yote, CHADEMA wakiwa ni watu wa kukubali makapi ya CCM na kuyapa uongozi harakaharaka tu, wananchi tutaona CHADEMA ama haijali muonekano wa ugwiji wa kiitikadi ya chama kama kifungu muhimu cha sifa za uongozi, ama inajali siasa za majina zaidi ya siasa za itikadi. Vyote viwili ni vibaya.

Na CHADEMA bila kuwapa hawa wageni muda ndani ya chama kuwajua vizuri, itajuaje kama haipewi mapandikizi ya CCM yaliyo na lengo la kukivunja chama?
 
Acheni magugu yakue pamoja na ngano!!! Wakati wa mavuno ukifika magugu yatatiwa motoni na ngano itawekwa ghalani!!!
 
haya maswala yalituponza kule TARIME jamaa amehama ccm akapitishwa kugombea ubunge akaja na sera yake mpya kuwa wale madiwani wote waliokuwa ndani ya halmashauri kupitia chadema wapumzike anaweka wapya akaanza na
1 netto sasi kemambo
2mama nyagabona mjini(viti maalum)
3mama tecla(viti maalum)
4mzee maswi(nyarero)
5machage b machage(matongo)
6john heche (tarime mjini)
akasema hawa wote wapumzike na kweli alipata nguvu akawashinda hawa jamaa wote alipambana na huyu no5 tu kimabavu no 5 akagombea na mgombea aliyekuwa anapigiwa chapuo na huyu jamaa aliyetoka ccm akahamia NCCR akapata kura 127 kata nzima huku no 5 akipata kura zaidi ya 3400 na kumshinda wa ccm aliyepata 2300
hawa akina heche na familia yao na wao akawapiga wanted kuwaona kwenye kampeni zake wa kakaa pembeni jamaa akasema yeye atawakata mawakala vichwa kila kituo atakachokuta kashindwa mawakala wakamsusa jamaa alikuwa hana hata nia njema mpaka majukwaani alitoa matusi mpaka unapoenda kwenye mkutno wake chukua tahadhari kama mama na baba wapo au kama familia yako ni chadema wote maana anaweza kuporomosha neno la aibu kila mmoja akatafuta pa kuondokea tena kwa kilugha watu wakamchoka akawa analewa chakali akaachia na jimbo live
kule singida kuna mtu alitoka ccm naye akapewa fomu ya chadema wale wa chadema wakawekwa reserve after the time jamaa akajitoa tukapoteza CHADEMA okoteni watu saana ila mwana uliyemkuza kumkontein ni rahisi halafu chui pia huvaa ngozi ya kondoo chadema kuweni makini
 
Back
Top Bottom